Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Thessaloniciens 4.2
Bible en Swahili de l’est


Appel à la sainteté

1 Iliyobaki, ndugu, tunakusihini na kuwaonya kwamba mwenende katika Bwana Yesu; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza Mungu, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana.
Colossiens 1.10 2 Thessaloniciens 1.3 Philippiens 1.9 Colossiens 2.6 Hébreux 13.16
2 Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu.
Ezéchiel 3.17 Matthieu 28.20 2 Thessaloniciens 3.10 2 Thessaloniciens 3.6 1 Corinthiens 9.21
3 Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;
1 Pierre 4.2 1 Thessaloniciens 5.23 Colossiens 3.5 Ephésiens 5.17 Romains 12.2
4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;
1 Corinthiens 7.9 1 Pierre 3.7 1 Corinthiens 7.2 1 Corinthiens 6.15 Romains 12.1
5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu.
Galates 4.8 Romains 1.26 2 Thessaloniciens 1.8 Actes 17.30-17.31 1 Corinthiens 15.34
6 Mtu asimpunje ndugu yake wala kumkosa katika jambo hili; kwa sababu Bwana ndiye alipizaye kisasi cha haya yote; kama tulivyowaambia kwanza, tukashuhudia sana.
Romains 12.19 Hébreux 13.4 Ephésiens 4.28 1 Corinthiens 6.7-6.9 Romains 13.4
7 Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.
Ephésiens 1.4 Lévitique 11.44 1 Thessaloniciens 2.3 Ephésiens 2.10 1 Pierre 1.14-1.16
8 Basi yeye anayekataa, hakatai mwanadamu bali Mungu, anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.
1 Jean 3.24 Luc 10.16 1 Samuel 8.7 Jean 12.48 Romains 5.5
9 Katika habari ya upendano, hamna haja niwaandikie; maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana.
1 Jean 3.11 Romains 12.10 1 Jean 3.23 1 Thessaloniciens 5.1 Hébreux 13.1
10 Kwa maana mnafanya neno hili kwa ndugu wote walio katika Makedonia yote. Lakini twawasihi, ndugu, mzidi sana.
1 Thessaloniciens 3.12 1 Thessaloniciens 1.7 2 Thessaloniciens 1.3 Philippiens 3.13-3.15 Philippiens 1.9
11 Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza;
Ephésiens 4.28 1 Pierre 4.15 1 Pierre 3.4 Ecclésiaste 4.6 1 Timothée 2.2
12 ili mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote.
Marc 4.11 Colossiens 4.5 Romains 13.13 1 Timothée 3.7 Romains 12.17

Résurrection des croyants et retour du Seigneur

13 Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
Ephésiens 2.12 2 Pierre 3.4 Daniel 12.2 Jean 11.11-11.13 Actes 7.60
14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.
Romains 8.11 2 Corinthiens 4.13-4.14 Apocalypse 1.18 1 Thessaloniciens 4.13 Philippiens 3.20-3.21
15 Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.
1 Corinthiens 15.51-15.53 2 Corinthiens 4.14 Psaumes 119.147-119.148 Matthieu 17.25 Psaumes 88.13
16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
Apocalypse 1.7 Matthieu 24.30-24.31 Matthieu 16.27 1 Corinthiens 15.51-15.52 2 Thessaloniciens 1.7
17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
Apocalypse 11.12 1 Corinthiens 15.52 Jean 14.3 Jean 12.26 Apocalypse 7.14-7.17
18 Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
1 Thessaloniciens 5.14 1 Thessaloniciens 5.11 Hébreux 10.24-10.25 Luc 21.28 Hébreux 12.12

Cette Bible est dans le domaine public.