Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Colossiens 4.6
Bible en Swahili de l’est


1 Ninyi akina bwana, wapeni watumwa wenu yaliyo haki na ya adili, mkijua ya kuwa ninyi nanyi mna Bwana mbinguni.
Ephésiens 6.8-6.20 Lévitique 25.39-25.43 Matthieu 24.48-24.51 Luc 16.1-16.13 Néhémie 5.5-5.13

Dernières instructions

2 Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani;
1 Thessaloniciens 5.17-5.18 Luc 18.1 Philippiens 4.6 Ephésiens 6.18 Romains 12.12
3 mkituombea na sisi pia, kwamba Mungu atufungulie mlango kwa lile neno lake, tuinene siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake nimefungwa,
Ephésiens 6.19-6.20 Apocalypse 3.7-3.8 Philippiens 1.7 Actes 14.27 2 Timothée 2.9
4 ili niidhihirishe, kama inipasavyo kunena.
2 Corinthiens 4.1-4.4 Ephésiens 6.20 Actes 5.29 1 Corinthiens 2.4-2.5 Colossiens 4.6
5 Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.
Ephésiens 5.15-5.17 1 Thessaloniciens 4.12 1 Timothée 3.7 Jacques 3.13 Romains 16.19
6 Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.
1 Pierre 3.15 Ephésiens 4.29 Marc 9.50 Colossiens 3.16 Matthieu 5.13

Salutations

7 Tikiko, ndugu mpendwa, mtumishi mwaminifu, mjoli wangu katika Bwana, atawaarifu mambo yangu yote;
2 Timothée 4.12 Actes 20.4 Colossiens 4.9 Ephésiens 6.21-6.23 Philippiens 2.25
8 ambaye nimemtuma kwenu kwa sababu iyo hiyo, ili mjue mambo yetu, naye akawafariji mioyo yenu;
Ephésiens 6.22 Colossiens 2.2 1 Corinthiens 4.17 1 Thessaloniciens 4.18 1 Thessaloniciens 5.14
9 pamoja na Onesimo, ndugu mwaminifu, mpendwa, aliye mtu wa kwenu. Hao watawaarifu mambo yote ya hapa petu.
Philémon 1.10-1.19 Colossiens 4.7
10 Aristarko, aliyefungwa pamoja nami, awasalimu; na Marko, mjomba wake Barnaba, ambaye mmepokea maagizo kwa habari yake; akifika kwenu mkaribisheni.
Actes 19.29 2 Timothée 4.11 Actes 27.2 Actes 12.12 Actes 20.4
11 Na Yesu aitwaye Yusto; hao ni watu wa tohara. Tena hao peke yao ni watendaji wa kazi pamoja nami kwa ajili ya ufalme wa Mungu; nao walikuwa faraja kwangu.
Actes 11.2 Philippiens 4.3 Colossiens 4.7 1 Thessaloniciens 3.7 Galates 2.7-2.8
12 Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu.
Philémon 1.23 Romains 15.30 Colossiens 1.7 Colossiens 1.28 Matthieu 5.48
13 Maana namshuhudia kwamba ana juhudi nyingi kwa ajili yenu, na kwa ajili ya hao walioko Laodikia, na kwa ajili ya hao walioko Hierapoli.
Colossiens 2.1 Apocalypse 3.14-3.18 2 Corinthiens 8.3 Apocalypse 1.11 Colossiens 4.15-4.16
14 Luka, yule tabibu mpendwa, na Dema, wanawasalimu.
Philémon 1.24 2 Timothée 4.10-4.11
15 Wasalimuni ndugu walioko Laodikia, na Nimfa, na kanisa lililo katika nyumba yake.
Romains 16.5 Philémon 1.2 1 Corinthiens 16.9
16 Waraka huu ukiisha kusomwa kwenu fanyeni kwamba usomwe katika kanisa la Walaodikia pia; na ule wa Laodikia usomwe na ninyi.
1 Thessaloniciens 5.27 2 Thessaloniciens 3.14
17 Mwambieni Arkipo, Iangalie sana huduma ile uliyopewa katika Bwana, ili uitimize.
Philémon 1.2 2 Timothée 4.1-4.5 1 Timothée 6.11-6.14 1 Timothée 6.20 Nombres 18.5
18 Salamu yangu mimi Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe. Kumbukeni kufungwa kwangu. Neema na iwe pamoja nanyi.
Hébreux 13.3 2 Timothée 4.22 1 Corinthiens 16.21 1 Timothée 6.21 Hébreux 13.25

Cette Bible est dans le domaine public.