Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 6.6
Bible en Swahili de l’est


Données essentielles de la loi

1 Na hii ndiyo sheria, na amri, na hukumu, alizoziamuru Bwana, Mungu wenu, mfundishwe, mpate kuzitenda katika nchi ile mnayoivukia kuimiliki;
Deutéronome 4.1 Deutéronome 12.1 Deutéronome 4.45 Deutéronome 5.31 Lévitique 27.34
2 upate kumcha Bwana, Mungu wako, kushika amri zake zote, na sheria zake, ninazokuamuru, wewe na mwanao, na mwana wa mwanao, siku zote za maisha yako; tena siku zako ziongezwe.
Psaumes 128.1 Ecclésiaste 12.13 Exode 20.20 Psaumes 111.10 Deutéronome 13.4
3 Sikiza basi, Ee Israeli, ukaangalie kuzitenda; upate kufanikiwa, mpate kuongezeka sana, kama Bwana, Mungu wa baba zako, alivyokuahidi, katika nchi ijaayo maziwa na asali.
Exode 3.8 Genèse 15.5 Genèse 22.17 Genèse 28.14 Genèse 26.4
4 Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.
1 Timothée 2.5 Jean 10.30 Marc 12.29-12.32 Esaïe 44.6 Esaïe 45.5-45.6
5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.
Marc 12.30 Luc 10.27 Matthieu 22.37 Deutéronome 4.29 Deutéronome 10.12
6 Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako;
Deutéronome 11.18 Psaumes 37.31 Esaïe 51.7 Colossiens 3.16 Proverbes 7.3
7 nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.
Ephésiens 6.4 Deutéronome 11.19 Deutéronome 4.9-4.10 Exode 12.26-12.27 Deutéronome 6.2
8 Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako.
Exode 13.9 Deutéronome 11.18 Proverbes 6.21 Proverbes 3.3 Proverbes 7.3
9 Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako.
Deutéronome 11.20 Esaïe 57.8 Esaïe 30.8 Exode 12.7 Job 19.23-19.25
10 Tena itakuwa atakapokwisha Bwana, Mungu wako, kukuleta katika nchi aliyowaapia babu zako, Ibrahimu na Isaka na Yakobo, ya kuwa atakupa; miji mikubwa mizuri usiyoijenga wewe,
Josué 24.13 Psaumes 105.44 Néhémie 9.25 Genèse 26.3 Genèse 13.15-13.17
11 na nyumba zimejaa vitu vyema vyote usizojaza wewe, na visima vimefukuliwa usivyofukua wewe, mashamba ya mizabibu na mizeituni usiyoipanda wewe, nawe utakula na kushiba;
Deutéronome 32.15 Matthieu 19.23-19.24 Deutéronome 7.12-7.18 Jérémie 2.31-2.32 Deutéronome 8.10-8.20
12 ndipo ujitunze, usije ukamsahau Bwana aliyekutoa nchi ya Misri, nyumba ya utumwa.
13 Mche Bwana, Mungu wako; ndiye utakayemtumikia, na kuapa kwa jina lake.
Luc 4.8 Deutéronome 10.20 Matthieu 4.10 Psaumes 63.11 Deutéronome 13.4
14 Msifuate miungu mingine katika miungu ya mataifa wawazungukao;
Jérémie 25.6 Deutéronome 8.19 Deutéronome 13.7 1 Jean 5.21 Deutéronome 11.28
15 kwani Bwana, Mungu wako, aliye katikati yako ni Mungu mwenye wivu; isije ikawaka juu yako hasira ya Bwana, Mungu wako, akakuangamiza kutoka juu ya uso wa nchi.
Deutéronome 4.24 Exode 20.5 Deutéronome 7.4 Deutéronome 11.17 Psaumes 90.11
16 Msimjaribu Bwana, Mungu wenu, kama mlivyomjaribu huko Masa.
Luc 4.12 Exode 17.7 Matthieu 4.7 Psaumes 95.8-95.9 Hébreux 3.8-3.9
17 Zishikeni kwa bidii sheria za Bwana, Mungu wenu, na mashuhudizo yake, na amri zake alizokuagiza.
Psaumes 119.4 Deutéronome 11.22 Exode 15.26 1 Corinthiens 15.58 Tite 3.8
18 Nawe fanya yaliyo sawa, na mema, machoni pa Bwana; ili mpate kufanikiwa, nawe upate kuingia na kuimiliki nchi nzuri Bwana aliyowaapia baba zako,
Deutéronome 4.40 Deutéronome 12.25 Deutéronome 5.29 Ezéchiel 18.5 Romains 12.2
19 ya kuwa atawasukumia nje adui zako wote mbele yako, kama alivyosema Bwana.
Nombres 33.52-33.53 Exode 23.28-23.30 Juges 2.1-2.3 Juges 3.1-3.4
20 Na zamani zijazo atakapokuuliza mwanao, akikuambia, N’nini mashuhudizo, na amri, na hukumu, alizowaagiza Bwana, Mungu wetu?
Exode 13.14 Exode 12.26 Josué 4.21-4.24 Josué 4.6-4.7 Proverbes 22.6
21 Ndipo umwambie mwanao, Tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri; Bwana, akatutoa kutoka Misri kwa mkono wa nguvu;
Exode 20.2 Néhémie 9.9-9.10 Psaumes 136.10-136.12 Deutéronome 26.5-26.9 Exode 13.3
22 Bwana akaonya ishara na maajabu, makubwa, mazito, juu ya Misri, na juu ya Farao, na juu ya nyumba yake yote, mbele ya macho yetu;
Psaumes 135.9 Deutéronome 4.34 Deutéronome 1.30 Deutéronome 7.19 Exode 7.1-7.12
23 akatutoa huko ili kututia huku, apate kutupa nchi aliyowaapia baba zetu.
Deutéronome 6.10 Deutéronome 6.18 Deutéronome 1.8 Deutéronome 1.35 Exode 13.5
24 Bwana akatuamuru kuzifanya amri hizi zote, tumche Bwana, Mungu wetu, tuone mema sikuzote ili atuhifadhi hai kama hivi leo.
Psaumes 41.2 Jérémie 32.39 Deutéronome 8.1 Deutéronome 4.1 Deutéronome 8.3
25 Tena itakuwa haki kwetu, tukitunza kufanya maagizo haya yote mbele ya Bwana, Mungu wetu, kama alivyotuagiza.
Deutéronome 24.13 Romains 10.3 Psaumes 106.30-106.31 Romains 10.5-10.6 Galates 3.12

Cette Bible est dans le domaine public.