Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 19.9
Bible en Swahili de l’est


Les villes de refuge

1 Bwana, Mungu wako, atakapoyakatilia mbali hayo mataifa yenye nchi akupayo Bwana, Mungu wako, nawe ukawafuata, na kukaa katika miji yao, na katika nyumba zao;
Deutéronome 12.29 Deutéronome 6.10 Deutéronome 17.14 Deutéronome 7.1-7.2 Deutéronome 12.1
2 itenge miji mitatu iwe kwako katikati ya nchi yako, akupayo Bwana, Mungu wako, kuimiliki.
Hébreux 6.18 Exode 21.13 Deutéronome 4.41-4.43 Josué 20.2-20.7 Nombres 35.10-35.15
3 Itengeze njia, igawanye na mipaka ya nchi yako, akurithishayo Bwana, Mungu wako, iwe mafungu matatu, ili kwamba kila mwenye kuua mtu apate kukimbilia huko.
Esaïe 57.14 Esaïe 35.8 Hébreux 12.13 Esaïe 62.10
4 Na hii ndiyo hukumu ya mwenye kuua mtu, atakayekimbilia huko awe hai; atakayemwua mwenziwe pasipo kukusudia, wala hakumchukia tangu hapo;
Nombres 35.15-35.24 Deutéronome 4.42 Esaïe 30.33 Deutéronome 19.6 Josué 3.4
5 kama aingiapo mtu na mwenziwe mwituni kwenda kukata kuni, akapeleka mkono wake na shoka ili kukata mti, likatoka shoka katika mpini, likampiga yule mwenziwe hata akafa; basi na akimbilie katika miji hii mmojawapo awe hai;
Esaïe 32.2 Nombres 35.25 Proverbes 27.12 2 Rois 6.5-6.7
6 asije akaandamiwa mwuaji na mwenye kulipiza kisasi cha damu, moyo wake ukali na hasira, akampata kwa njia kuwa ndefu, akamwua; wala hana haki ya kuuawa, kwa kuwa hakumchukia tangu hapo.
Nombres 35.12 Deutéronome 21.22 2 Samuel 14.7 Jérémie 26.15-26.16 Josué 20.5
7 Kwa sababu hii ninakuamuru, na kukuambia, Ujitengee miji mitatu.
8 Na kama Bwana, Mungu wako, akiueneza mpaka wako kama alivyowaapia baba zako, akakupa na nchi yote aliyoahidi kwamba atawapa baba zako;
Exode 23.31 Genèse 15.18-15.21 Exode 34.24 Deutéronome 12.20 1 Rois 4.21
9 nawe ukiyashika maagizo haya yote nikuagizayo leo, na kuyafanya, kumpenda Bwana, Mungu wako, na kwenda sikuzote katika njia zake, ndipo ujiongezee miji mitatu tena, pamoja na mitatu ile;
Josué 20.7-20.8 Deutéronome 11.22-11.25 Deutéronome 12.32
10 isije ikamwagika damu ya asiye makosa kati ya nchi yako akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi, ikawa na damu juu yako.
Esaïe 59.7 Proverbes 6.17 Matthieu 27.4-27.5 Deutéronome 19.13 Nombres 35.33
11 Lakini mtu awaye yote akimchukia mwenziwe na kumwotea na kumwinukia, akampiga hata akafa; naye akakimbilia miji hii mmojawapo;
Deutéronome 27.24 Nombres 35.16-35.21 Nombres 35.24 Proverbes 28.17 Genèse 9.6
12 ndipo wazee wa mji wake wapeleke ujumbe kumtwaa huko, na kumuua katika mkono wa mwenye kulipiza kisasi cha damu, apate kufa.
1 Rois 2.28-2.34 1 Rois 2.5-2.6
13 Jicho lako lisimhurumie, lakini uondoe damu ya asiye makosa katika Israeli, ili upate kufanikiwa.
1 Rois 2.31 Deutéronome 7.16 Deutéronome 7.2 Deutéronome 21.9 Deutéronome 25.12

Respect des limites et nécessité de témoins

14 Usiiondoe alama ya mpaka wa jirani yako, waliouweka watu wa kale katika urithi wako, utakaorithi ndani ya nchi akupayo Bwana, Mungu wako, uimiliki.
Osée 5.10 Proverbes 22.28 Deutéronome 27.17 Job 24.2 Proverbes 23.10
15 Shahidi mmoja asimwinukie mtu awaye yote kumshuhudia kwa uovu wo wote, wala kwa dhambi yo yote, katika makosa akosayo yo yote; jambo na lithibitishwe kwa vinywa vya mashahidi wawili, au watatu.
2 Corinthiens 13.1 Matthieu 18.16 Nombres 35.30 Deutéronome 17.6 1 Timothée 5.19
16 Shahidi mdhalimu akimwinukia mtu ye yote na kushuhudia juu yake ya upotoe;
Psaumes 27.12 Exode 23.1-23.7 Psaumes 35.11 Actes 6.13 Marc 14.55-14.59
17 ndipo wale watu washindanao kwa mambo yale na wasimame wote wawili mbele za Bwana, mbele ya makuhani na waamuzi watakaokuwapo siku hizo;
Deutéronome 17.9 Deutéronome 21.5 Malachie 2.7 Matthieu 23.2-23.3
18 nao waamuzi na watafute kwa bidii; na tazama, yule shahidi akiwa shahidi wa uongo, naye ametoa ushahidi wa uongo juu ya nduguye;
Deutéronome 13.14 Deutéronome 17.4 2 Chroniques 19.6-19.7 Job 19.16
19 ndipo mtamfanyia kama alivyodhani kumfanyia nduguye; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.
Proverbes 19.5 Proverbes 19.9 Deutéronome 22.24 Daniel 6.24 Deutéronome 24.7
20 Na watakaosalia watasikia na kuogopa, wasifanye tena uovu mfano wa huo katikati yako.
Deutéronome 17.13 Deutéronome 21.21 Deutéronome 13.11 Romains 13.3-13.4 Proverbes 21.11
21 Wala jicho lako lisiwe na huruma; uzima kwa uzima, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.
Deutéronome 19.13 Lévitique 24.17-24.21 Matthieu 5.38-5.39 Exode 21.23-21.25

Cette Bible est dans le domaine public.