Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 7.2
Bible en Swahili de l’est


Réponses à des questions

Sur le mariage et le célibat

1 Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke.
1 Corinthiens 7.8 1 Corinthiens 7.26-7.27 1 Corinthiens 7.37-7.38 Genèse 20.6 Proverbes 6.29
2 Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.
1 Corinthiens 7.9 Proverbes 19.14 Proverbes 5.18-5.19 Proverbes 18.22 1 Corinthiens 6.18
3 Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.
Exode 21.10 1 Pierre 3.7
4 Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.
Marc 10.11-10.12 Osée 3.3 Matthieu 19.9
5 Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.
Exode 19.15 1 Samuel 21.4-21.5 1 Thessaloniciens 3.5 Joël 2.16 Zacharie 12.12-12.14
6 Lakini nasema hayo, kwa kutoa idhini yangu, si kwa amri.
2 Corinthiens 8.8 1 Corinthiens 7.25 1 Corinthiens 7.12 2 Corinthiens 11.17
7 Ila nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu hivi.
1 Corinthiens 9.5 Matthieu 19.11-19.12 1 Corinthiens 12.11 1 Corinthiens 12.4 1 Corinthiens 7.8
8 Lakini nawaambia wale wasiooa bado, na wajane, Ni heri wakae kama mimi nilivyo.
1 Corinthiens 7.1 1 Corinthiens 7.32 1 Corinthiens 7.34-7.35 1 Corinthiens 7.7 1 Corinthiens 7.26-7.27
9 Lakini ikiwa hawawezi kujizuia, na waoe; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa.
1 Timothée 5.14 1 Corinthiens 7.2 1 Timothée 5.11 1 Corinthiens 7.28 1 Corinthiens 7.39
10 Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe;
Matthieu 5.32 Luc 16.18 Malachie 2.14-2.16 Matthieu 19.3-19.9 Marc 10.11-10.12
11 lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.
1 Corinthiens 7.10 Jérémie 3.1 Deutéronome 22.19 Esaïe 50.1 Juges 19.2-19.3
12 Lakini watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache.
2 Corinthiens 11.17 1 Corinthiens 7.6 Esdras 10.11-10.19 Esdras 10.2-10.3 1 Corinthiens 7.25
13 Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.
14 Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.
Tite 1.15 Malachie 2.15-2.16 Romains 11.16 Esaïe 52.1 Actes 10.23
15 Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani.
Romains 14.19 Jacques 2.15 Galates 5.22 Romains 12.18 1 Corinthiens 14.33
16 Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?
Romains 11.14 1 Corinthiens 9.22 Jacques 5.19-5.20 1 Timothée 4.16 Luc 15.10
17 Lakini kama Bwana alivyomgawia kila mtu, kama Mungu alivyomwita kila mtu, na aenende vivyo hivyo. Ndivyo ninavyoagiza katika makanisa yote.
1 Corinthiens 4.17 2 Corinthiens 11.28 2 Corinthiens 8.18 Romains 12.3-12.8 1 Corinthiens 7.20-7.21
18 Je! Mtu fulani ameitwa hali amekwisha kutahiriwa? Asijifanye kana kwamba hakutahiriwa. Mtu fulani ameitwa hali hajatahiriwa bado? Basi asitahiriwe.
Actes 15.24 Actes 15.19 Actes 15.28 Actes 15.5 Actes 15.1-15.2
19 Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu bali kuzihifadhi amri za Mungu.
Galates 6.15 Galates 5.6 Apocalypse 22.14 Colossiens 3.11 Jean 15.14
20 Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa.
1 Corinthiens 7.17 Luc 3.10-3.14 1 Thessaloniciens 4.11 2 Thessaloniciens 3.12 1 Corinthiens 7.21-7.24
21 Je! Uliitwa u mtumwa? Usione ni vibaya lakini kama ukiweza kuwa na uhuru, afadhali kuutumia.
1 Pierre 5.7 Philippiens 4.6 1 Corinthiens 12.13 Philippiens 4.11 1 Timothée 6.1-6.3
22 Kwa maana yeye aliyeitwa katika Bwana hali ya utumwa, ni huru wa Bwana. Vivyo hivyo yeye naye aliyeitwa hali ya uhuru, ni mtumwa wa Kristo.
1 Pierre 2.16 Philémon 1.16 Galates 5.1 Colossiens 4.12 Jude 1.1
23 Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu.
1 Corinthiens 6.20 Lévitique 25.42 1 Pierre 3.18 Tite 2.14 1 Pierre 1.18-1.19
24 Ndugu zangu, kila mtu na akae mbele za Mungu katika hali iyo hiyo aliyoitwa nayo.
1 Corinthiens 7.20 Colossiens 3.23-3.24 1 Samuel 14.45 1 Corinthiens 10.31 Genèse 5.22-5.24
25 Kwa habari za wanawali sina amri ya Bwana, lakini natoa shauri langu, mimi niliyejaliwa kwa rehema za Bwana kuwa mwaminifu.
1 Corinthiens 7.6 1 Corinthiens 4.2 1 Corinthiens 7.12 1 Corinthiens 15.10 1 Corinthiens 7.34
26 Basi, naona hili kuwa jema, kwa ajili ya shida iliyopo, kwamba ni vema mtu akae kama alivyo.
1 Corinthiens 7.8 1 Corinthiens 7.1 Luc 21.23 Matthieu 24.19 Luc 23.28-23.29
27 Je! Umefungwa kwa mke? Usitake kufunguliwa. Umefunguliwa? Usitafute mke.
1 Corinthiens 7.12-7.14 1 Corinthiens 7.20
28 Lakini, kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo.
1 Corinthiens 7.32-7.36 Hébreux 13.4 1 Corinthiens 7.26 2 Corinthiens 1.23
29 Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana;
Romains 13.11-13.12 Jacques 4.13-4.16 1 Corinthiens 7.31 Ecclésiaste 12.13-12.14 Psaumes 39.4-39.7
30 na wale waliao kama hawalii; na wale wafurahio kama hawafurahi; na wale wanunuao, kama hawana kitu.
Apocalypse 7.17 Luc 6.25 Ecclésiaste 3.4 Psaumes 30.5 Jean 16.22
31 Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita.
1 Jean 2.17 1 Pierre 4.7 Psaumes 39.6 1 Corinthiens 9.18 Jacques 4.14
32 Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;
1 Timothée 5.5 Philippiens 4.6 Psaumes 55.22 Matthieu 6.25-6.34 Matthieu 13.22
33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.
1 Pierre 3.7 Luc 12.22 1 Samuel 1.4-1.8 Ephésiens 5.25-5.33 Néhémie 5.1-5.5
34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe.
Romains 12.1-12.2 Philippiens 1.20 Romains 6.13 Luc 10.40-10.42 1 Corinthiens 6.20
35 Nasema hayo niwafaidie, si kwamba niwategee tanzi, bali kwa ajili ya vile vipendezavyo, tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine.
1 Corinthiens 7.36 Matthieu 19.12 1 Corinthiens 7.28 Luc 8.14 1 Corinthiens 7.5-7.9
36 Lakini mtu awaye yote akiona ya kuwa hamtendei mwanamwali wake vipendezavyo, na ikiwa huyo amepita uzuri wa ujana wake, na ikiwapo haja, basi, afanye apendavyo, hatendi dhambi, na awaruhusu waoane.
37 Lakini yeye aliyesimama kwa uthabiti wa moyo wake, hana sharti, lakini aweza kuyatawala mapenzi yake, tena amekusudia moyoni mwake kumlinda mwanamwali wake, atatenda vema.
38 Basi, hivyo na amwozaye mwanamwali wake afanya vema; na yeye asiyemwoza atazidi kufanya vema.
Hébreux 13.4 1 Corinthiens 7.37 1 Corinthiens 7.26 1 Corinthiens 7.8 1 Corinthiens 7.32-7.34
39 Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu.
1 Corinthiens 7.15 Romains 7.2-7.3 1 Corinthiens 7.10 2 Corinthiens 6.14-6.16 Malachie 2.11
40 Lakini heri yeye zaidi akikaa kama alivyo; ndivyo nionavyo mimi, nami nadhani ya kuwa mimi nami nina Roho wa Mungu.
1 Corinthiens 7.25-7.26 1 Corinthiens 7.35 2 Pierre 3.15-3.16 1 Corinthiens 7.6 1 Corinthiens 9.1-9.3

Cette Bible est dans le domaine public.