Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 12.21
Bible en Swahili de l’est


La vie nouvelle

De nouveaux comportements

1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
1 Pierre 2.5 Romains 6.13 Romains 6.19 Hébreux 13.15-13.16 Romains 12.2
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.
1 Pierre 1.14 2 Corinthiens 5.17 Colossiens 3.10 Ephésiens 4.22-4.24 1 Jean 2.15-2.17
3 Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.
Philippiens 2.3-2.8 1 Pierre 4.11 Galates 6.3 1 Pierre 5.5 1 Pierre 4.7
4 Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;
1 Corinthiens 12.27 1 Corinthiens 12.4 1 Corinthiens 12.12-12.14 Ephésiens 4.15-4.16 Ephésiens 4.4
5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.
1 Corinthiens 10.17 Ephésiens 4.25 1 Corinthiens 12.20 Colossiens 2.19 1 Corinthiens 10.33
6 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;
1 Corinthiens 7.7 1 Pierre 4.10-4.11 1 Corinthiens 12.28-12.31 Romains 12.3 1 Corinthiens 14.1
7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;
Actes 13.1 Ephésiens 4.11 1 Timothée 4.16 Colossiens 1.28-1.29 Ecclésiaste 12.9
8 mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.
2 Corinthiens 9.7 1 Timothée 5.17 1 Corinthiens 12.28 Hébreux 10.25 Actes 13.15
9 Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema.
1 Timothée 1.5 1 Pierre 4.8 Psaumes 34.14 Amos 5.15 Psaumes 101.3
10 Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu;
Jean 13.34-13.35 Hébreux 13.1 Philippiens 2.3 1 Pierre 2.17 1 Thessaloniciens 4.9
11 kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;
Actes 18.25 Hébreux 6.10-6.11 1 Pierre 4.8 1 Pierre 1.22 Ephésiens 6.5-6.8
12 kwa tumaini, mkifurahi; katika dhiki, mkisubiri; katika kusali, mkidumu;
Hébreux 10.36 Romains 15.13 Psaumes 16.9-16.11 Psaumes 62.8 1 Pierre 4.13
13 kwa mahitaji ya watakatifu, mkifuata ukarimu; katika kukaribisha wageni mkijitahidi.
Hébreux 6.10 2 Corinthiens 9.12 2 Corinthiens 9.1 1 Timothée 3.2 Hébreux 13.16
14 Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.
Matthieu 5.44 Luc 6.28 1 Pierre 3.9 1 Thessaloniciens 5.15 Jacques 3.10
15 Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao.
1 Corinthiens 12.26 Hébreux 13.3 Philippiens 2.17-2.18 Job 30.25 Psaumes 35.13-35.14
16 Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.
1 Pierre 3.8 Romains 15.5 Proverbes 3.7 Jacques 3.13-3.17 Romains 11.25
17 Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.
Proverbes 20.22 2 Corinthiens 8.20-8.21 1 Thessaloniciens 5.15 Matthieu 5.39 Philippiens 4.8-4.9
18 Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.
Marc 9.50 Romains 14.19 Matthieu 5.9 Galates 5.22 2 Corinthiens 13.11
19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.
Deutéronome 32.35 Hébreux 10.30 Proverbes 24.29 Proverbes 20.22 Matthieu 5.39
20 Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake.
Proverbes 25.21-25.22 Luc 6.27 Matthieu 5.44 2 Rois 6.22 Exode 23.4-23.5
21 Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.
1 Pierre 3.9 Proverbes 16.32 Luc 6.27-6.30

Cette Bible est dans le domaine public.