1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
1 Pierre 2.5  Romains 6.13  Romains 6.19  Hébreux 13.15-13.16  Romains 12.2  
 2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.
1 Pierre 1.14  2 Corinthiens 5.17  Colossiens 3.10  Ephésiens 4.22-4.24  1 Jean 2.15-2.17  
 3 Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.
Philippiens 2.3-2.8  1 Pierre 4.11  Galates 6.3  1 Pierre 5.5  1 Pierre 4.7  
 4 Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;
1 Corinthiens 12.27  1 Corinthiens 12.4  1 Corinthiens 12.12-12.14  Ephésiens 4.15-4.16  Ephésiens 4.4  
 5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.
1 Corinthiens 10.17  Ephésiens 4.25  1 Corinthiens 12.20  Colossiens 2.19  1 Corinthiens 10.33  
 6 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;
1 Corinthiens 7.7  1 Pierre 4.10-4.11  1 Corinthiens 12.28-12.31  Romains 12.3  1 Corinthiens 14.1  
 7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;
Actes 13.1  Ephésiens 4.11  1 Timothée 4.16  Colossiens 1.28-1.29  Ecclésiaste 12.9  
 8 mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.
2 Corinthiens 9.7  1 Timothée 5.17  1 Corinthiens 12.28  Hébreux 10.25  Actes 13.15  
 9 Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema.
1 Timothée 1.5  1 Pierre 4.8  Psaumes 34.14  Amos 5.15  Psaumes 101.3  
 10 Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu;
Jean 13.34-13.35  Hébreux 13.1  Philippiens 2.3  1 Pierre 2.17  1 Thessaloniciens 4.9  
 11 kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;
Actes 18.25  Hébreux 6.10-6.11  1 Pierre 4.8  1 Pierre 1.22  Ephésiens 6.5-6.8  
 12 kwa tumaini, mkifurahi; katika dhiki, mkisubiri; katika kusali, mkidumu;
Hébreux 10.36  Romains 15.13  Psaumes 16.9-16.11  Psaumes 62.8  1 Pierre 4.13  
 13 kwa mahitaji ya watakatifu, mkifuata ukarimu; katika kukaribisha wageni mkijitahidi.
Hébreux 6.10  2 Corinthiens 9.12  2 Corinthiens 9.1  1 Timothée 3.2  Hébreux 13.16  
 14 Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.
Matthieu 5.44  Luc 6.28  1 Pierre 3.9  1 Thessaloniciens 5.15  Jacques 3.10  
 15 Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao.
1 Corinthiens 12.26  Hébreux 13.3  Philippiens 2.17-2.18  Job 30.25  Psaumes 35.13-35.14  
 16 Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.
1 Pierre 3.8  Romains 15.5  Proverbes 3.7  Jacques 3.13-3.17  Romains 11.25  
 17 Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.
Proverbes 20.22  2 Corinthiens 8.20-8.21  1 Thessaloniciens 5.15  Matthieu 5.39  Philippiens 4.8-4.9  
 18 Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.
Marc 9.50  Romains 14.19  Matthieu 5.9  Galates 5.22  2 Corinthiens 13.11  
 19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.
Deutéronome 32.35  Hébreux 10.30  Proverbes 24.29  Proverbes 20.22  Matthieu 5.39  
 20 Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake.
Proverbes 25.21-25.22  Luc 6.27  Matthieu 5.44  2 Rois 6.22  Exode 23.4-23.5  
 21 Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.1 Pierre 3.9  Proverbes 16.32  Luc 6.27-6.30