Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 12.14
Bible en Swahili de l’est


La vie nouvelle

De nouveaux comportements

1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
1 Pierre 2.5 Romains 6.13 Romains 6.19 Hébreux 13.15-13.16 Romains 12.2
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.
1 Pierre 1.14 2 Corinthiens 5.17 Colossiens 3.10 Ephésiens 4.22-4.24 1 Jean 2.15-2.17
3 Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.
Philippiens 2.3-2.8 Galates 6.3 1 Pierre 4.11 1 Pierre 5.5 1 Pierre 4.7
4 Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;
1 Corinthiens 12.4 1 Corinthiens 12.27 Ephésiens 4.15-4.16 1 Corinthiens 12.12-12.14 Ephésiens 4.4
5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.
1 Corinthiens 10.17 Ephésiens 4.25 1 Corinthiens 12.20 Colossiens 2.19 Ephésiens 1.23
6 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;
1 Corinthiens 7.7 1 Pierre 4.10-4.11 1 Corinthiens 12.28-12.31 Romains 12.3 Ephésiens 4.11
7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;
Actes 13.1 Ephésiens 4.11 2 Timothée 2.24 1 Timothée 2.7 2 Timothée 4.2
8 mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.
2 Corinthiens 9.7 1 Corinthiens 12.28 1 Timothée 5.17 Deutéronome 15.8-15.11 Actes 15.32
9 Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema.
1 Timothée 1.5 1 Pierre 4.8 Psaumes 34.14 Psaumes 101.3 Psaumes 97.10
10 Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu;
Jean 13.34-13.35 Hébreux 13.1 Philippiens 2.3 1 Pierre 2.17 1 Thessaloniciens 4.9
11 kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;
Actes 18.25 Hébreux 6.10-6.11 1 Pierre 4.8 Ephésiens 6.5-6.8 Ephésiens 4.28
12 kwa tumaini, mkifurahi; katika dhiki, mkisubiri; katika kusali, mkidumu;
Hébreux 10.36 Romains 15.13 Psaumes 16.9-16.11 Psaumes 62.8 Actes 1.14
13 kwa mahitaji ya watakatifu, mkifuata ukarimu; katika kukaribisha wageni mkijitahidi.
2 Corinthiens 9.12 2 Corinthiens 9.1 Hébreux 6.10 Hébreux 13.16 1 Timothée 3.2
14 Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.
Matthieu 5.44 Luc 6.28 1 Pierre 3.9 1 Thessaloniciens 5.15 Jacques 3.10
15 Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao.
1 Corinthiens 12.26 Hébreux 13.3 Philippiens 2.17-2.18 Job 30.25 Psaumes 35.13-35.14
16 Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.
1 Pierre 3.8 Proverbes 3.7 Romains 15.5 Jacques 3.13-3.17 Hébreux 13.5
17 Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.
Proverbes 20.22 1 Thessaloniciens 5.15 2 Corinthiens 8.20-8.21 Matthieu 5.39 1 Pierre 3.9
18 Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.
Marc 9.50 Romains 14.19 Matthieu 5.9 Galates 5.22 Hébreux 12.14
19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.
Deutéronome 32.35 Proverbes 24.29 Hébreux 10.30 Proverbes 20.22 Matthieu 5.39
20 Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake.
Proverbes 25.21-25.22 Luc 6.27 Matthieu 5.44 2 Rois 6.22 Exode 23.4-23.5
21 Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.
1 Pierre 3.9 Proverbes 16.32 Luc 6.27-6.30

Cette Bible est dans le domaine public.