Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 19.6
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko;
1 Corinthiens 16.12 Actes 18.1 1 Corinthiens 1.12 Actes 18.19-18.21 Actes 18.23-18.28
2 akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia.
Jean 7.39 Actes 2.17 1 Corinthiens 6.19 Actes 10.44 1 Samuel 3.7
3 Akawauliza, Basi mlibatizwa kwa ubatizo gani? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana.
Actes 18.25 Matthieu 28.19 Matthieu 3.1-3.17 1 Corinthiens 12.13 Actes 8.16
4 Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu.
Jean 1.7 Jean 1.27 Marc 1.1-1.12 Luc 1.76-1.79 Actes 11.16
5 Waliposikia haya wakabatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
Actes 8.16 Actes 8.12 1 Corinthiens 10.2 Actes 2.38 1 Corinthiens 1.13-1.15
6 Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.
Actes 2.4 Actes 6.6 Marc 16.17 2 Timothée 1.6 1 Corinthiens 12.8-12.11
7 Na jumla yao walipata wanaume kumi na wawili.
8 Akaingia ndani ya sinagogi, akanena kwa ushujaa kwa muda wa miezi mitatu, akihojiana na watu, na kuwavuta katika mambo ya ufalme wa Mungu.
Actes 1.3 Actes 28.23 Actes 18.4 Actes 17.1-17.3 Actes 9.20-9.22
9 Lakini wengine walikaidi, wakakataa kuamini, wakiitukana ile Njia mbele ya mkutano; basi, akaondoka akawaacha, akawatenga wanafunzi, akahojiana na watu kila siku katika darasa ya mtu mmoja, jina lake Tirano.
Actes 9.2 Actes 19.23 Actes 14.4 Actes 13.45-13.46 Esaïe 8.14
10 Mambo haya yakaendelea kwa muda wa miaka miwili, hata wote waliokaa Asia wakalisikia neno la Bwana, Wayahudi kwa Wayunani.
Actes 20.31 2 Timothée 1.15 Actes 16.6 Actes 19.8 Colossiens 3.11
11 Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida;
Actes 5.12 Romains 15.18-15.19 Hébreux 2.4 Actes 16.18 Jean 14.12
12 hata wagonjwa wakaletewa leso na nguo zilizotoka mwilini mwake, magonjwa yao yakawaondokea, pepo wachafu wakawatoka.
Actes 5.15 2 Rois 13.20-13.21 2 Rois 4.29-4.31 Marc 16.17
13 Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo.
Matthieu 12.27 Luc 11.19 Marc 9.38 Marc 5.7 Matthieu 26.63
14 Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, kuhani mkuu, waliofanya hivyo.
15 Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani?
Marc 5.9-5.13 Marc 1.34 Luc 4.33-4.35 Marc 1.24 Genèse 3.1-3.5
16 Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.
Marc 5.3-5.4 Marc 5.15 Luc 8.29 Luc 8.35
17 Habari hii ikajulikana na Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawaingia wote, na jina la Bwana Yesu likatukuzwa.
Actes 5.11 Actes 5.5 2 Thessaloniciens 1.12 Philippiens 1.20 Luc 1.65
18 Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao.
Matthieu 3.6 Ezéchiel 36.31 Ezéchiel 16.63 Lévitique 16.21 Lévitique 26.40
19 Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu.
Genèse 35.4 Esaïe 8.19 Exode 7.11 Matthieu 5.29-5.30 Actes 13.8
20 Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu.
Actes 12.24 Actes 6.7 Esaïe 55.11 2 Thessaloniciens 3.1
21 Mambo hayo yalipokwisha kumalizika, Paulo akaazimu rohoni mwake, akiisha kupita katika Makedonia na Akaya, aende Yerusalemu, akisema, Baada ya kuwako huko, yanipasa kuuona na Rumi pia.
Actes 20.22 Actes 20.16 Actes 18.21 Actes 23.11 Romains 1.13
22 Akatuma watu wawili miongoni mwa wale waliomtumikia kwenda Makedonia, nao ni Timotheo na Erasto, yeye mwenyewe akakaa katika Asia kitambo.
Romains 16.23 2 Timothée 4.20 Actes 16.1 Actes 18.5 Actes 13.5
23 Wakati huo kukatukia ghasia si haba katika habari ya Njia ile.
Actes 19.9 Actes 24.22 Actes 9.2 2 Corinthiens 1.8-1.10 Actes 18.26
24 Kwa maana mtu mmoja, jina lake Demetrio, mfua fedha, aliyekuwa akifanya vihekalu vya fedha vya Artemi, alikuwa akiwapatia mafundi faida nyingi.
Actes 16.16 Esaïe 56.11-56.12 1 Timothée 6.9-6.10 Actes 16.19 Actes 19.27-19.28
25 Akawakusanya hao, pamoja na wengine wenye kazi ile ile, akasema, Enyi wanaume, mnajua ya kuwa utajiri wetu hutoka katika kazi hii.
Actes 16.19 Osée 12.7-12.8 2 Pierre 2.3 Apocalypse 18.3 Osée 4.8
26 Tena mnaona na kusikia ya kwamba si katika Efeso tu, bali katika Asia yote pia Paulo huyo ameshawishi watu wengi na kuwageuza nia zao, akisema ya kwamba hiyo inayofanywa kwa mikono siyo miungu.
Actes 17.29 1 Corinthiens 8.4 Esaïe 44.10-44.20 Deutéronome 4.28 Actes 19.10
27 Si kwamba kazi hii yetu ina hatari ya kudharauliwa tu; bali na hekalu la mungu mke aliye mkuu, Artemi, kuhesabiwa si kitu, na kuondolewa utukufu wake, ambaye Asia yote pia na walimwengu wote humwabudu.
Matthieu 23.13 1 Timothée 6.5 Actes 19.21 Apocalypse 13.3 1 Jean 5.19
28 Waliposikia haya wakajaa ghadhabu, wakapiga kelele, wakisema, Artemi wa Waefeso ni mkuu.
Apocalypse 13.4 Actes 18.19 Actes 19.34-19.35 Actes 16.19-16.24 Jérémie 50.38
29 Mji wote ukajaa ghasia, wakaenda mbio wakaingia mahali pa michezo kwa nia moja, wakiisha kuwakamata Gayo na Aristarko, watu wa Makedonia waliosafiri pamoja na Paulo.
Actes 20.4 Philémon 1.24 Colossiens 4.10 Actes 27.2 1 Corinthiens 1.14
30 Na Paulo alipotaka kuingia kati ya watu, wanafunzi hawakumwacha aingie.
2 Samuel 18.2-18.3 2 Samuel 21.17 Actes 21.39 Actes 17.22-17.31 Actes 14.14-14.18
31 Na baadhi ya wakuu wa Asia, walio rafiki zake, wakatuma watu kwake, wakimsihi asijihudhurishe nafsi yake ndani ya mahali pa michezo.
Actes 16.6 Actes 19.10 Proverbes 16.7 Actes 21.12
32 Basi wengine walikuwa wakilia hivi na wengine hivi; kwa maana ule mkutano ulikuwa umechafuka-chafuka, na wengi wao hawakuijua sababu ya kukusanyika kwao pamoja.
Actes 21.34 Matthieu 11.7-11.9 Actes 19.29 Actes 19.40 Luc 7.24-7.26
33 Wakamtoa Iskanda katika mkutano, Wayahudi wakimweka mbele ya watu. Iskanda akawapungia mkono, akitaka kujitetea mbele ya wale watu.
Actes 12.17 Luc 1.22 1 Timothée 1.20 2 Timothée 4.14 Actes 24.10
34 Lakini walipotambua ya kuwa yeye ni Myahudi, wakapiga kelele wote pia kwa sauti moja kwa muda wa kama saa mbili, wakisema, Artemi wa Waefeso ni mkuu.
Actes 19.28 Romains 2.22 1 Rois 18.26 Matthieu 6.7 Actes 19.26
35 Na karani wa mji alipokwisha kuwatuliza watu, akasema, Enyi wanaume wa Efeso, ni mtu gani asiyejua ya kuwa mji wa Efeso ni mtunzaji wa hekalu la Artemi, aliye mkuu, na wa kitu kile kilichoanguka kutoka mbinguni?
Actes 14.12-14.13 Actes 18.19 Actes 19.26 Ephésiens 2.12 2 Thessaloniciens 2.10-2.11
36 Basi kwa kuwa mambo haya hayawezi kukanushwa, imewapasa kutulia; msifanye neno la haraka haraka.
Proverbes 14.29 Actes 5.35-5.39 Proverbes 25.8
37 Kwa maana mmewaleta watu hawa, wasioiba vitu vya hekalu wala kumtukana mungu mke wetu.
Romains 2.22 1 Corinthiens 10.32 2 Corinthiens 6.3 Actes 25.8
38 Basi ikiwa Demetrio na mafundi walio pamoja naye wana neno juu ya mtu, baraza ziko, na maliwali wako; na washitakiane.
Actes 13.7 Deutéronome 17.8 1 Corinthiens 6.1 Actes 18.14
39 Bali mkitafuta neno lo lote katika mambo mengine, yatatengenezwa katika kusanyiko lililo halali.
40 Kwa maana tuna hatari ya kushitakiwa kwa ajili ya matata haya ya leo, ambayo hayana sababu; na katika neno hilo, hatutaweza kujiudhuru kwa mkutano huu.
Actes 21.38 1 Rois 1.41 Matthieu 26.5 Actes 20.1 Actes 21.31
41 Alipokwisha kusema haya akauvunja mkutano.
Proverbes 15.1-15.2 Ecclésiaste 9.17 Psaumes 65.7 2 Corinthiens 1.8-1.10

Cette Bible est dans le domaine public.