Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 2.23
Bible en Swahili de l’est


Premier miracle de Jésus en Galilée

1 Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.
Jean 4.46 Jean 21.2 Proverbes 19.14 Jean 1.43 Genèse 2.18-2.25
2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
Matthieu 25.45 Hébreux 13.4 Colossiens 3.17 Luc 7.34-7.38 1 Corinthiens 10.31
3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.
Ecclésiaste 10.19 Psaumes 104.15 Philippiens 4.6 Jean 11.3 Matthieu 26.28
4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.
Jean 8.20 Jean 7.6 Jean 13.1 Jean 7.30 Jean 12.23
5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.
Actes 9.6 Hébreux 11.8 Luc 6.46-6.49 Hébreux 5.9 Juges 13.14
6 Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.
Jean 3.25 Hébreux 9.10 Marc 7.2-7.5 Ephésiens 5.26 Hébreux 10.22
7 Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.
2 Rois 5.10-5.14 Nombres 21.6-21.9 Marc 14.12-14.17 Jean 2.5 2 Rois 4.2-4.6
8 Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.
Proverbes 3.5-3.6 Ecclésiaste 9.6 Jean 2.9 Romains 13.7
9 Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,
Jean 4.46 Jean 7.17 Psaumes 119.100
10 akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa.
Apocalypse 7.16-7.17 Proverbes 9.1-9.6 Luc 16.25 Cantique 5.1 Genèse 43.34
11 Mwanzo huo wa ishara Yesu aliufanya huko Kana ya Galilaya, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.
Jean 1.14 Jean 20.30-20.31 Jean 3.2 Jean 6.2 Jean 6.30
12 Baada ya hayo akashuka mpaka Kapernaumu, yeye na mama yake na ndugu zake na wanafunzi wake; wakakaa huko siku si nyingi.
Matthieu 12.46 Matthieu 4.13 1 Corinthiens 9.5 Actes 1.13-1.14 Galates 1.19

Jésus dans le temple, à Jérusalem

13 Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; naye Yesu akakwea mpaka Yerusalemu.
Jean 11.55 Luc 2.41 Jean 2.23 Jean 6.4 Deutéronome 16.1-16.8
14 Akaona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng’ombe na kondoo na njiwa, na wenye kuvunja fedha wameketi.
Marc 11.15 Luc 19.45-19.46 Matthieu 21.12-21.13 Deutéronome 14.23-14.26 Malachie 3.1-3.3
15 Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng’ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao;
Zacharie 4.6 Jean 18.6 2 Corinthiens 10.4
16 akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara.
Luc 2.49 Matthieu 21.13 Esaïe 56.5-56.11 Jérémie 7.11 Marc 11.17
17 Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, Wivu wa nyumba yako utanila.
Psaumes 69.9 Psaumes 119.139
18 Basi Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara gani utuonyeshayo, kwamba unafanya haya?
Jean 6.30 Marc 11.27-11.28 Matthieu 21.23 Jean 1.25 Matthieu 12.38-12.42
19 Yesu akajibu, akawaambia, Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha.
Marc 15.29 Matthieu 27.40 Marc 14.58 Romains 8.11 Matthieu 26.60-26.61
20 Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?
21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake.
1 Corinthiens 6.19 Colossiens 2.9 Jean 1.14 1 Corinthiens 3.16 1 Pierre 2.4-2.5
22 Basi alipofufuka katika wafu, wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa alisema hivi, wakaliamini lile andiko na lile neno alilolinena Yesu.
Jean 14.26 Jean 12.16 Jean 2.17 Luc 24.7-24.8 Luc 24.44
23 Hata alipokuwapo Yerusalemu kwenye sikukuu wakati wa Pasaka, watu wengi waliamini jina lake, walipoziona ishara zake alizozifanya.
Jean 3.2 Galates 5.6 Jacques 2.19-2.20 Jean 8.30-8.31 Jean 2.13
24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote;
Jean 6.15 Matthieu 9.4 Jean 16.30 1 Samuel 16.7 Jean 5.42
25 na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.
Jean 13.11 Jean 6.61 Matthieu 9.4 Jean 6.64

Cette Bible est dans le domaine public.