Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 2.15
Bible en Swahili de l’est


Premier miracle de Jésus en Galilée

1 Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.
Jean 21.2 Jean 4.46 Proverbes 19.14 Jean 1.43 1 Timothée 4.1-4.3
2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
Matthieu 12.19 Matthieu 10.40-10.42 Jean 1.40-1.49 Matthieu 25.45 Hébreux 13.4
3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.
Philippiens 4.6 Jean 11.3 Matthieu 26.28 Ecclésiaste 10.19 Psaumes 104.15
4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.
Jean 8.20 Jean 7.6 Jean 7.30 Jean 13.1 Ecclésiaste 3.1
5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.
Luc 5.5-5.6 Jean 15.14 Genèse 6.22 Actes 9.6 Hébreux 11.8
6 Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.
Jean 3.25 Hébreux 9.10 Hébreux 10.22 Hébreux 6.2 Marc 7.2-7.5
7 Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.
Marc 11.2-11.6 Josué 6.3-6.5 Actes 8.26-8.40 2 Rois 5.10-5.14 Nombres 21.6-21.9
8 Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.
Ecclésiaste 9.6 Jean 2.9 Romains 13.7 Proverbes 3.5-3.6
9 Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,
Jean 4.46 Jean 7.17 Psaumes 119.100
10 akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa.
Apocalypse 7.16-7.17 Luc 16.25 Proverbes 9.1-9.6 Proverbes 9.16-9.18 Psaumes 104.15
11 Mwanzo huo wa ishara Yesu aliufanya huko Kana ya Galilaya, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.
Jean 20.30-20.31 Jean 1.14 Jean 3.2 Jean 6.14 Jean 14.9-14.11
12 Baada ya hayo akashuka mpaka Kapernaumu, yeye na mama yake na ndugu zake na wanafunzi wake; wakakaa huko siku si nyingi.
Matthieu 12.46 Matthieu 4.13 Jean 7.3-7.5 1 Corinthiens 9.5 Actes 1.13-1.14

Jésus dans le temple, à Jérusalem

13 Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; naye Yesu akakwea mpaka Yerusalemu.
Luc 2.41 Jean 11.55 Jean 2.23 Jean 6.4 Exode 12.6-12.14
14 Akaona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng’ombe na kondoo na njiwa, na wenye kuvunja fedha wameketi.
Marc 11.15 Luc 19.45-19.46 Malachie 3.1-3.3 Marc 11.17 Matthieu 21.12-21.13
15 Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng’ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao;
Zacharie 4.6 Jean 18.6 2 Corinthiens 10.4
16 akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara.
Matthieu 21.13 Luc 2.49 Jérémie 7.11 Marc 11.17 Esaïe 56.5-56.11
17 Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, Wivu wa nyumba yako utanila.
Psaumes 69.9 Psaumes 119.139
18 Basi Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara gani utuonyeshayo, kwamba unafanya haya?
Jean 6.30 Marc 8.11 Luc 11.29 Actes 5.28 Luc 20.1-20.2
19 Yesu akajibu, akawaambia, Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha.
Matthieu 27.40 Marc 15.29 Marc 14.58 Matthieu 26.60-26.61 Romains 8.11
20 Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?
21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake.
1 Corinthiens 6.19 1 Corinthiens 3.16 Colossiens 2.9 Jean 1.14 2 Corinthiens 6.16
22 Basi alipofufuka katika wafu, wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa alisema hivi, wakaliamini lile andiko na lile neno alilolinena Yesu.
Jean 12.16 Jean 14.26 Jean 2.17 Luc 24.7-24.8 Jean 16.4
23 Hata alipokuwapo Yerusalemu kwenye sikukuu wakati wa Pasaka, watu wengi waliamini jina lake, walipoziona ishara zake alizozifanya.
Jean 3.2 Luc 8.13 Marc 4.16-4.17 Matthieu 13.20-13.21 Jean 7.31
24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote;
1 Samuel 16.7 Jean 5.42 Jean 6.64 Actes 1.24 Jean 6.15
25 na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.
Jean 13.11 Matthieu 9.4 Jean 6.64 Jean 6.61

Cette Bible est dans le domaine public.