Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 14.35
Bible en Swahili de l’est


Cause du séjour de quarante ans dans le désert

1 Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule.
Nombres 11.1-11.4 Deutéronome 1.45
2 Kisha wana wa Israeli wote wakamnung’unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili.
Nombres 16.41 Exode 15.24 Exode 17.3 Philippiens 2.14-2.15 Psaumes 106.24
3 Mbona Bwana anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; je! Si afadhali turudi Misri?
Jérémie 9.3 Psaumes 78.40 Nombres 14.31-14.32
4 Wakaambiana, Na tumweke mtu mmoja awe akida, tukarudi Misri.
Deutéronome 17.16 Actes 7.39 Deutéronome 28.68 Hébreux 11.15 Luc 17.32
5 Ndipo Musa na Haruni wakaanguka kifudifudi mbele ya mkutano wa kusanyiko la wana wa Israeli.
Nombres 16.4 Nombres 16.22 Nombres 16.45 Josué 7.10 Daniel 10.9
6 Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao;
Nombres 13.6 Nombres 13.8 Nombres 14.30 2 Rois 18.37 Joël 2.12-2.13
7 wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu.
Deutéronome 1.25 Nombres 13.27 Deutéronome 8.7-8.9 Deutéronome 6.10-6.11
8 Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali.
Deutéronome 10.15 Nombres 13.27 Psaumes 22.8 2 Samuel 22.20 Esaïe 62.4
9 Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope.
Psaumes 74.14 Deutéronome 9.23-9.24 Deutéronome 7.18 Deutéronome 9.7 Nombres 24.8
10 Lakini mkutano wote wakaamuru wapigwe kwa mawe. Ndipo utukufu wa Bwana ukaonekana katika hema ya kukutania, mbele ya wana wa Israeli wote.
Lévitique 9.23 Exode 17.4 Exode 16.10 Exode 24.16-24.17 Matthieu 23.37
11 Bwana akamwuliza Musa, Je! Watu hawa watanidharau hata lini? Wasiniamini hata lini? Nijapokuwa nimefanya ishara hizo zote kati yao.
Psaumes 106.24 Jean 12.37 Psaumes 78.32 Psaumes 78.22 Deutéronome 1.32
12 Nitawapiga kwa tauni, na kuwaondolea urithi wao, nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, kisha yenye nguvu kuliko wao.
Exode 32.10 Nombres 25.9 Nombres 16.46-16.49 Exode 5.3 2 Samuel 24.1
13 Basi Musa akamwambia Bwana, Ndipo Wamisri watasikia habari hiyo; kwa kuwa wewe uliwaleta watu hawa kwa uweza wako, kutoka kati yao;
Psaumes 106.23 Ezéchiel 20.14 Ezéchiel 20.9 Deutéronome 32.27 Josué 7.8-7.9
14 kisha watawaambia wenyeji wa nchi hii; wamesikia wao ya kuwa wewe Bwana u kati ya watu hawa; maana, wewe Bwana waonekana uso kwa uso, na wingu lako lasimama juu yao, kisha wewe watangulia mbele yao, katika nguzo ya wingu mchana, na katika nguzo ya moto usiku.
Exode 15.14 Jean 1.18 Exode 33.11 Josué 2.9-2.10 Genèse 32.30
15 Basi kama wewe ukiwaua watu hawa mfano wa mtu mmoja, ndipo mataifa yaliyosikia habari za sifa zako watakaponena na kusema,
Juges 6.16
16 Ni kwa sababu yeye Bwana hakuweza kuwaleta watu hao kuwatia katika nchi aliyowaapia, kwa ajili ya hayo amewaua nyikani.
Josué 7.9 Deutéronome 9.28 Deutéronome 32.26-32.27 Josué 7.7
17 Basi sasa nakusihi sana, uweza wa Bwana wangu na uwe mkuu, kama ulivyonena, uliposema,
Matthieu 9.6 Michée 3.8 Matthieu 9.8
18 Bwana ni mpole wa hasira, mwingi wa rehema, mwenye kusamehe uovu na makosa, naye hatamfanya mwenye hatia kuwa hana makosa kwa njia yo yote; mwenye kuwapatiliza wana kwa uovu wa baba zao, katika kizazi cha tatu na cha nne.
Exode 34.6-34.7 Exode 20.5 Psaumes 145.8 Jonas 4.2 Psaumes 103.8
19 Nakusihi, usamehe uovu wa watu hawa, kama ukuu wa rehema yako ulivyo, kama ulivyowasamehe watu hawa, tangu huko Misri hata hivi sasa.
Exode 34.9 Psaumes 78.38 Psaumes 106.45 Exode 32.32 Jonas 4.2
20 Bwana akasema, Mimi nimewasamehe kama neno lako lilivyokuwa;
Michée 7.18-7.20 Psaumes 106.23 Jacques 5.16
21 lakini hakika yangu, kama niishivyo, tena kama dunia hii nzima itakavyojawa na utukufu wa Bwana;
Habakuk 2.14 Psaumes 72.19 Deutéronome 32.40 Esaïe 49.18 Matthieu 6.10
22 kwa sababu watu hawa wote, ambao wameuona utukufu wangu na ishara zangu, nilizozitenda huko Misri, na huko jangwani, pamoja na haya wamenijaribu mara hizi kumi, wala hawakuisikiza sauti yangu;
Job 19.3 Psaumes 106.26 Genèse 31.7 Hébreux 3.17-3.18 Exode 17.2
23 hakika yangu hawataiona hiyo nchi niliyowaapia baba zao, wala katika hao wote walionidharau hapana atakayeiona;
Nombres 32.11 Ezéchiel 20.15 Nombres 26.64 Psaumes 106.26 Néhémie 9.23
24 lakini mtumishi wangu Kalebu, kwa kuwa alikuwa na roho nyingine ndani yake, naye ameniandama kwa moyo wote, nitamleta yeye mpaka nchi hiyo aliyoingia; na uzao wake wataimiliki.
Nombres 14.6-14.9 Deutéronome 1.36 Nombres 26.65 Josué 14.6-14.14 1 Chroniques 29.9
25 Basi Mwamaleki na Mkanaani wakaa katika bonde; kesho geukeni, mkaende jangwani kwa njia iendayo Bahari ya Shamu.
Deutéronome 1.40 Nombres 13.29 Psaumes 81.11-81.13 Nombres 14.4 Proverbes 1.31
26 Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
27 Je! Nichukuane na mkutano mwovu huu uninung’unikiao hata lini? Nimesikia manung’uniko ya wana wa Israeli, waninung’unikiayo.
Exode 16.12 Nombres 14.11 1 Corinthiens 10.10 Marc 9.19 Exode 16.28
28 Waambieni, Kama niishivyo, asema Bwana, hakika yangu kama ninyi mlivyonena masikioni mwangu, ndivyo nitakavyowafanyia ninyi;
Nombres 14.21 Nombres 14.23 Hébreux 3.17 Nombres 26.64-26.65 Nombres 14.2
29 mizoga yenu itaanguka katika jangwa hili, na wote waliohesabiwa miongoni mwenu, kama jumla ya hesabu yenu, tangu waliopata umri wa miaka ishirini na zaidi, hao walioninung’unikia,
Nombres 1.45 Hébreux 3.17 Nombres 26.64 1 Corinthiens 10.5 Jude 1.5
30 hakika yangu hamtaingia ninyi katika nchi, ambayo niliinua mkono wangu ya kwamba nitawaketisha humo, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.
Genèse 14.22 Nombres 14.38 Nombres 26.65 Deutéronome 1.36-1.38 Nombres 32.12
31 Lakini Watoto wenu, ambao mlisema watakuwa mateka, ndio nitakaowaleta na kuwatia ndani, nao wataijua nchi ninyi mliyoikataa.
Psaumes 106.24 Deutéronome 1.39 Hébreux 12.16-12.17 Proverbes 1.30 Nombres 26.6
32 Lakini katika habari zenu, mizoga yenu itaanguka katika jangwa hili.
1 Corinthiens 10.5 Nombres 14.29 Hébreux 3.17
33 Kisha watoto wenu watakuwa wachungaji jangwani muda wa miaka arobaini nao watauchukua mzigo wa uasherati wenu, hata mizoga yenu itakapoangamia jangwani.
Ezéchiel 23.35 Psaumes 107.40 Deutéronome 2.14 Nombres 32.13 Nombres 33.38
34 Kwa hesabu ya hizo siku mlizoipeleleza ile nchi, yaani, siku arobaini kila siku kuhesabiwa mwaka, mtayachukua maovu yenu, ndiyo miaka arobaini, nanyi mtakujua kufarikana kwangu.
Nombres 13.25 Ezéchiel 4.6 Daniel 9.24 Nombres 18.23 2 Chroniques 36.21
35 Mimi Bwana nimekwisha nena, hakika yangu ndilo nitakaloutenda mkutano mwovu huu wote, waliokusanyika juu yangu; wataangamia katika nyika hii, nako ndiko Watakakokufa.
Nombres 23.19 Nombres 26.65 Nombres 14.27-14.29 Hébreux 3.19 1 Corinthiens 10.11
36 Kisha hao watu, ambao Musa aliwatuma waipeleleze nchi, waliorudi, na kufanya mkutano wote kumnung’unikia, kwa walivyoleta habari mbaya juu ya nchi,
Nombres 13.31-13.33 Nombres 13.4-13.16
37 watu hao walioileta habari mbaya ya nchi wakafa kwa tauni mbele ya Bwana.
1 Corinthiens 10.10 Hébreux 3.17 Nombres 16.49 Jude 1.5 Nombres 14.12
38 Lakini Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, wakabaki hai miongoni mwa wale watu waliokwenda kuipeleleza nchi.
Nombres 26.65 Josué 14.6-14.10
39 Kisha Musa akawaambia wana wa Israeli wote maneno haya, na hao watu wakaombolea sana.
Exode 33.4 Hébreux 12.17 Proverbes 19.3 Esaïe 26.16 Matthieu 8.12
40 Wakainuka na mapema asubuhi, wakakwea juu ya mlima hata kileleni, wakisema, Tazameni, sisi tupo hapa, nasi tutakwea kwenda mahali Bwana alipotuahidi; kwani tumefanya dhambi.
Deutéronome 1.41 Luc 13.25 Matthieu 26.11-26.12 Matthieu 7.21-7.23 Ecclésiaste 9.3
41 Musa akawaambia, Kwa nini ninyi sasa kuyahalifu maagizo ya Bwana? Maana halitafanikiwa jambo hilo.
2 Chroniques 24.20 Nombres 14.25 Jérémie 2.37 Job 4.9 Jérémie 32.5
42 Msikwee, kwa kuwa Bwana hamo kati yenu; msipigwe na kuangushwa mbele ya adui zenu.
Deutéronome 1.42 Josué 7.12 Psaumes 44.1-44.11 Josué 7.8
43 Kwa kuwa Mwamaleki na Mkanaani wako mbele yenu, nanyi mtaanguka kwa upanga, kwa sababu mmerudi nyuma msimwandame Bwana, kwa hiyo Bwana hatakuwa pamoja nanyi.
Nombres 14.25 Nombres 13.29 Esaïe 63.10 2 Chroniques 15.2 Juges 16.20
44 Lakini walithubutu kukwea mlimani hata kileleni; ila sanduku la agano la Bwana halikutoka humo maragoni, wala Musa hakutoka.
Deutéronome 1.43 Nombres 15.30 Nombres 10.33 1 Samuel 4.3-4.11 Nombres 31.6
45 Ndipo Mwamaleki, na Mkanaani waliokaa huko mlimani, wakatelemka, wakawapiga na kuwaangusha, hata kufikilia Horma.
Nombres 21.3 Juges 1.17 Deutéronome 1.44 Nombres 14.43 Deutéronome 32.30

Cette Bible est dans le domaine public.