Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Michée 5.8
Bible en Swahili de l’est


Naissance et règne du Messie

1 Sasa utajikusanya vikosi vikosi, Ee binti wa vikosi; yeye amemhusuru; watampiga mwamuzi wa Israeli shavuni mwake kwa fimbo.
Lamentations 3.30 Esaïe 33.22 Job 16.10 Actes 23.2 Jean 18.22
2 Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.
Matthieu 2.6 Jean 7.42 Esaïe 11.1 Zacharie 9.9 Esaïe 9.6-9.7
3 Kwa sababu hiyo atawatoa, hata wakati wa kuzaa kwake aliye na utungu; ndipo hayo mabaki ya nduguze watawarudia wana wa Israeli.
Osée 11.8 Michée 4.9-4.10 Michée 7.13 Esaïe 10.20-10.21 Michée 4.7
4 Naye atasimama, na kulisha kundi lake kwa nguvu za Bwana, kwa enzi ya jina la Bwana, Mungu wake; nao watakaa; maana sasa atakuwa mkuu hata miisho ya dunia.
Michée 7.14 Luc 1.32 Psaumes 72.8 Esaïe 52.10 Zacharie 9.10
5 Na mtu huyu atakuwa amani yetu; wakati Mwashuri atakapoingia katika nchi yetu, na kuyakanyaga majumba yetu, hapo mtaondokesha wachungaji saba juu yake, na wakuu wanane.
Zacharie 9.10 Luc 2.14 Esaïe 8.7-8.10 Ecclésiaste 11.2 Jean 16.33
6 Nao wataiharibu nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake; naye atatuokoa na Mwashuri, atakapoingia katika nchi yetu, na kukanyaga ndani ya mipaka yetu.
Genèse 10.8-10.11 Esaïe 14.25 2 Rois 19.32-19.35 2 Chroniques 33.11 Esaïe 10.5-10.12
7 Na hayo mabaki ya Yakobo yatakuwa kati ya kabila nyingi mfano wa umande utokao kwa Bwana, mfano wa manyunyu katika manyasi; yasiyomngojea mtu, wala kuwakawilia wanadamu.
Michée 5.3 Deutéronome 32.2 Osée 14.5 Esaïe 44.3 Psaumes 110.3
8 Na hayo mabaki ya Yakobo yatakuwa kati ya mataifa, kati ya kabila nyingi, mfano wa simba kati ya wanyama wa msituni, kama mwana-simba kati ya makundi ya kondoo, ambaye, akiwa anapita katikati, hukanyaga-kanyaga na kurarua-rarua, wala hakuna wa kuokoa.
Michée 4.13 Psaumes 50.22 Zacharie 10.5 Osée 5.14 Esaïe 41.15-41.16
9 Mkono wako na uinuliwe juu ya adui zako, na adui zako wote wakauliwe mbali.
Esaïe 26.11 Psaumes 21.8 Esaïe 37.36 Luc 19.27 Apocalypse 19.13-19.21
10 Kisha itakuwa katika siku hiyo, asema Bwana, nitawakatilia mbali farasi zako watoke kati yako, nami nitayaharibu magari yako ya vita;
Zacharie 9.10 Osée 14.3 Psaumes 20.7-20.8 Osée 1.7 Esaïe 2.7
11 nami nitaikatilia mbali miji ya nchi yako, na ngome zako zote nitaziangusha;
Esaïe 2.12-2.17 Amos 5.9 Ezéchiel 38.11 Osée 10.14 Esaïe 6.11
12 nami nitakatilia mbali uchawi, usiwe mkononi mwako; wala hutakuwa tena na watu wenye kutabana;
Deutéronome 18.10-18.12 Esaïe 27.9 Esaïe 2.18 Apocalypse 19.20 Esaïe 2.6-2.8
13 nami nitakatilia mbali sanamu zako na nguzo zako, zitoke kati yako; wala hutaiabudu tena kazi ya mikono yako.
Ezéchiel 6.9 Osée 14.8 Zacharie 13.2 Osée 14.3 Esaïe 2.8
14 Nami nitayang’oa maashera yenu, yasiwe kati yako; nami nitaiangamiza miji yako.
Exode 34.13
15 Nami nitajilipiza kisasi katika hasira na ghadhabu juu ya mataifa wasiosikiliza.
Michée 5.8 Psaumes 149.7 2 Thessaloniciens 1.8 Esaïe 65.12

Cette Bible est dans le domaine public.