Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Michée 2
Bible en Swahili de l’est


Péché et jugement d’Israël

1 Ole wao wakusudiao mambo maovu, na kutenda mabaya vitandani mwao! Kunapopambazuka asubuhi huyafanya, kwa sababu ya katika uwezo wa mikono yao.
Psaumes 36.4 Deutéronome 28.32 Genèse 31.29 Nahum 1.11 Esaïe 32.7
2 Nao hutamani mashamba, na kuyashika; na nyumba pia, nao huzichukua; nao humwonea mtu na nyumba yake, naam, mtu na urithi wake.
Esaïe 5.8 Amos 8.4 Jérémie 22.17 1 Timothée 6.10 2 Rois 9.26
3 Basi Bwana asema hivi, Angalia, nakusudia jambo baya juu ya jamaa hii, ambalo hamtazitoa shingo zenu, wala hamtakwenda kwa kiburi; kwa maana ni wakati mbaya.
Jérémie 8.3 Amos 5.13 Esaïe 2.11-2.12 Jérémie 18.11 Lamentations 2.17
4 Siku hiyo watatunga mithali juu yenu, na kuomboleza kwa maombolezo ya huzuni nyingi, na kusema, Sisi tumeangamizwa kabisa; Yeye analibadili fungu la watu wangu; Jinsi anavyoniondolea hilo! Awagawia waasi mashamba yetu.
Habakuk 2.6 Jérémie 9.17-9.21 Jérémie 9.10 Deutéronome 28.29 Michée 1.15
5 Kwa hiyo hutakuwa na mtu atakayeitupa kamba kwa kura katika mkutano wa Bwana.
Josué 18.4 Deutéronome 32.8 Josué 18.10 Deutéronome 23.2 Deutéronome 23.8
6 Msitabiri, ndivyo watabirivyo; wasiyatabiri mambo haya; lawama hazikomi.
Amos 2.12 Esaïe 30.10 Actes 7.51 Actes 4.17 Jérémie 26.8-26.9
7 Je! Litasemwa neno hili, enyi nyumba ya Yakobo, Roho ya Bwana imepunguzwa? Je! Haya ni matendo yake? Je! Maneno yangu hayamfai yeye aendaye kwa unyofu?
Psaumes 15.2 Psaumes 84.11 Esaïe 50.2 Jérémie 15.16 Esaïe 59.1-59.2
8 Lakini siku hizi mmeinuka kama adui za watu wangu; mwaipokonya joho iliyo juu ya nguo za hao wapitao salama kama watu wasiopenda vita.
Psaumes 120.6-120.7 2 Samuel 20.19 Psaumes 55.20 2 Chroniques 28.5-28.8 Esaïe 9.21
9 Wanawake wa watu wangu mwawatupa nje ya nyumba zao nzuri; watoto wao wachanga mwawanyang’anya utukufu wangu milele.
Ezéchiel 39.21 Habakuk 2.14 Psaumes 72.19 2 Corinthiens 3.18 Joël 3.6
10 Ondokeni, mwende zenu; maana hapa sipo mahali pa raha yenu; kwa sababu ya uchafu mtaangamizwa, naam, kwa maangamizo mazito sana.
Deutéronome 12.9 Psaumes 106.38 Lévitique 18.24-18.28 Jérémie 3.2 2 Chroniques 7.20
11 Mtu akienda kwa roho ya uongo, akinena maneno ya uongo, akisema, Nitakutabiria habari ya mvinyo na kileo; mtu huyu atakuwa nabii wao watu hawa.
Jérémie 5.31 Esaïe 30.10-30.11 Michée 3.5 Philippiens 3.19 2 Corinthiens 11.13-11.15

Promesse de rassemblement

12 Hakika nitakukusanya, Ee Yakobo, nyote pia; Bila shaka nitawakusanya waliobaki wa Israeli; Nitawaweka pamoja kama kondoo wa Bozra; Kama kundi la kondoo kati ya malisho yao; Watafanya mvumo kwa wingi wa watu;
Michée 4.6-4.7 Ezéchiel 36.37 Jérémie 31.7-31.10 Zacharie 9.14-9.15 Ezéchiel 34.11
13 Avunjaye amekwea juu mbele yao; Wamebomoa mahali, wakapita mpaka langoni, Wakatoka nje huko; Mfalme wao naye amepita akiwatangulia, Naye Bwana ametangulia mbele yao.
Esaïe 52.12 Apocalypse 7.17 Osée 3.5 Esaïe 45.1-45.2 Esaïe 42.13-42.16

Cette Bible est dans le domaine public.