Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Joël 1.17
Bible en Swahili de l’est


Une invasion dévastatrice

1 Neno la Bwana lililomjia Yoeli, mwana wa Pethueli.
Actes 2.16 Jérémie 1.2 Ezéchiel 1.3 2 Pierre 1.21 Osée 1.1
2 Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu?
Osée 5.1 Joël 2.2 Job 8.8 Jérémie 30.7 Matthieu 13.9
3 Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine.
Deutéronome 6.7 Psaumes 78.3-78.8 Psaumes 145.4 Exode 13.14 Josué 4.21-4.22
4 Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.
Joël 2.25 Amos 4.9 Esaïe 33.4 Exode 10.4 Psaumes 78.46
5 Levukeni, enyi walevi, mkalie; Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai; Kwa sababu ya divai mpya; Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu.
Jacques 5.1 Esaïe 24.7-24.11 Esaïe 32.10-32.12 Joël 3.3 Luc 21.34-21.36
6 Maana taifa limepanda juu ya nchi yangu, Lenye nguvu, tena halina hesabu; Meno yake ni kama meno ya simba, Naye ana magego ya simba mkubwa.
Joël 2.25 Psaumes 107.34 Osée 9.3 Proverbes 30.25-30.27 Apocalypse 9.7-9.10
7 Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe.
Esaïe 5.6 Joël 1.12 Exode 10.15 Habakuk 3.17 Jérémie 8.13
8 Ombolea kama mwanamwali avaaye magunia Kwa ajili ya mume wa ujana wake.
Esaïe 22.12 Proverbes 2.17 Malachie 2.15 Amos 8.10 Jacques 5.1
9 Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimekatiliwa mbali na nyumba ya Bwana; Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, wanaomboleza.
Joël 2.17 Joël 2.14 Joël 1.13 Osée 9.4 Esaïe 61.6
10 Shamba limeharibika, nchi inaomboleza; maana nafaka imeharibika, divai mpya imekauka, mafuta yamepunguka.
Osée 4.3 Osée 9.2 Joël 1.5 Jérémie 12.11 Jérémie 48.33
11 Tahayarini, enyi wakulima; Pigeni yowe, enyi watunzaji wa mizabibu; Kwa ajili ya ngano na shayiri, Maana mavuno ya mashamba yamepotea.
Jérémie 14.3-14.4 Esaïe 17.11 Jérémie 9.12 Romains 5.5 Amos 5.16
12 Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imekauka katika wanadamu.
Esaïe 24.11 Esaïe 16.10 Cantique 2.3 Joël 1.10 Psaumes 92.12
13 Jikazeni mkaomboleze, enyi makuhani; Pigeni yowe, enyi wahudumu wa madhabahu; Njoni mlale usiku kucha katika magunia, Enyi wahudumu wa Mungu wangu; Kwa kuwa sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimezuiwa katika nyumba ya Mungu wenu.
Jérémie 4.8 Joël 1.8-1.9 Joël 2.17 Jérémie 9.10 Jonas 3.5-3.8
14 Takaseni saumu, iteni kusanyiko la dini, Wazee na wakusanye wenyeji wote wa nchi; Waende nyumbani kwa Bwana, Mungu wenu, Na kumlilia Bwana,
Joël 2.15-2.16 Jonas 3.8 Lévitique 23.36 2 Chroniques 20.13 2 Chroniques 20.3-20.4
15 Ole wake siku hii! Kwa maana siku ya Bwana inakaribia, nayo itakuja kama uangamivu utokao kwake aliye Mwenyezi.
Jérémie 30.7 Joël 2.31 Esaïe 13.6-13.9 Joël 2.11 Ezéchiel 7.2-7.12
16 Je! Chakula hakikukatiliwa mbali mbele ya macho yetu? Naam, furaha na kicheko mbali na nyumba ya Mungu wetu?
Deutéronome 12.6-12.7 Psaumes 43.4 Joël 1.13 Esaïe 3.7 Amos 4.6-4.7
17 Mbegu zinaoza chini ya udongo wake; ghala zimeachwa ukiwa; mabanda yamevunjika; kwa maana nafaka imekauka.
Esaïe 17.10-17.11 Genèse 23.16
18 Jinsi wanyama wanavyougua! Makundi ya ng’ombe yamefadhaika, kwa sababu hawana malisho; naam, makundi ya kondoo yamepata mateso.
Jérémie 12.4 Osée 4.3 Jérémie 14.5-14.6 1 Rois 18.5 Romains 8.22
19 Ee Bwana, nakulilia wewe; Kwa maana moto umeyala malisho ya nyikani, Na miali ya moto imeteketeza miti yote ya mashamba.
Psaumes 50.15 Jérémie 9.10 Amos 7.4 Michée 7.7 Philippiens 4.6-4.7
20 Naam, wanyama wa mashamba wanakutwetea wewe; Kwa maana vijito vya maji vimekauka, Na moto umeyateketeza malisho ya nyikani.
Psaumes 104.21 1 Rois 17.7 1 Rois 18.5 Psaumes 147.9 Psaumes 145.15

Cette Bible est dans le domaine public.