Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Joël 1.15
Bible en Swahili de l’est


Une invasion dévastatrice

1 Neno la Bwana lililomjia Yoeli, mwana wa Pethueli.
Actes 2.16 Jérémie 1.2 2 Pierre 1.21 Osée 1.1 Ezéchiel 1.3
2 Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu?
Osée 5.1 Joël 2.2 Job 8.8 Matthieu 13.9 Jérémie 30.7
3 Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine.
Deutéronome 6.7 Psaumes 78.3-78.8 Psaumes 44.1 Josué 4.6-4.7 Psaumes 145.4
4 Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.
Joël 2.25 Amos 4.9 Psaumes 105.34 Esaïe 33.4 Exode 10.4
5 Levukeni, enyi walevi, mkalie; Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai; Kwa sababu ya divai mpya; Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu.
Jacques 5.1 Esaïe 24.7-24.11 Amos 6.3-6.7 Joël 1.11 Esaïe 32.10-32.12
6 Maana taifa limepanda juu ya nchi yangu, Lenye nguvu, tena halina hesabu; Meno yake ni kama meno ya simba, Naye ana magego ya simba mkubwa.
Joël 2.25 Esaïe 8.8 Psaumes 107.34 Osée 9.3 Proverbes 30.25-30.27
7 Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe.
Esaïe 5.6 Joël 1.12 Esaïe 24.7 Osée 2.12 Exode 10.15
8 Ombolea kama mwanamwali avaaye magunia Kwa ajili ya mume wa ujana wake.
Esaïe 22.12 Jérémie 3.4 Joël 1.13-1.15 Proverbes 2.17 Malachie 2.15
9 Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimekatiliwa mbali na nyumba ya Bwana; Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, wanaomboleza.
Joël 2.14 Joël 2.17 Joël 1.13 Osée 9.4 Esaïe 61.6
10 Shamba limeharibika, nchi inaomboleza; maana nafaka imeharibika, divai mpya imekauka, mafuta yamepunguka.
Osée 4.3 Osée 9.2 Joël 1.5 Jérémie 12.11 Joël 1.12
11 Tahayarini, enyi wakulima; Pigeni yowe, enyi watunzaji wa mizabibu; Kwa ajili ya ngano na shayiri, Maana mavuno ya mashamba yamepotea.
Jérémie 14.3-14.4 Esaïe 17.11 Jérémie 9.12 Romains 5.5 Amos 5.16
12 Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imekauka katika wanadamu.
Esaïe 16.10 Esaïe 24.11 Joël 1.10 Cantique 2.3 Psaumes 92.12
13 Jikazeni mkaomboleze, enyi makuhani; Pigeni yowe, enyi wahudumu wa madhabahu; Njoni mlale usiku kucha katika magunia, Enyi wahudumu wa Mungu wangu; Kwa kuwa sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimezuiwa katika nyumba ya Mungu wenu.
Jérémie 4.8 Joël 1.8-1.9 1 Rois 21.27 Joël 2.17 Jérémie 9.10
14 Takaseni saumu, iteni kusanyiko la dini, Wazee na wakusanye wenyeji wote wa nchi; Waende nyumbani kwa Bwana, Mungu wenu, Na kumlilia Bwana,
Joël 2.15-2.16 Jonas 3.8 Lévitique 23.36 2 Chroniques 20.13 2 Chroniques 20.3-20.4
15 Ole wake siku hii! Kwa maana siku ya Bwana inakaribia, nayo itakuja kama uangamivu utokao kwake aliye Mwenyezi.
Jérémie 30.7 Sophonie 1.14-1.18 Joël 2.31 Esaïe 13.6-13.9 Joël 2.11
16 Je! Chakula hakikukatiliwa mbali mbele ya macho yetu? Naam, furaha na kicheko mbali na nyumba ya Mungu wetu?
Deutéronome 12.6-12.7 Psaumes 43.4 Joël 1.5-1.9 Esaïe 62.8-62.9 Joël 1.13
17 Mbegu zinaoza chini ya udongo wake; ghala zimeachwa ukiwa; mabanda yamevunjika; kwa maana nafaka imekauka.
Esaïe 17.10-17.11 Genèse 23.16
18 Jinsi wanyama wanavyougua! Makundi ya ng’ombe yamefadhaika, kwa sababu hawana malisho; naam, makundi ya kondoo yamepata mateso.
Jérémie 12.4 Osée 4.3 Jérémie 14.5-14.6 Romains 8.22 Joël 1.20
19 Ee Bwana, nakulilia wewe; Kwa maana moto umeyala malisho ya nyikani, Na miali ya moto imeteketeza miti yote ya mashamba.
Jérémie 9.10 Psaumes 50.15 Amos 7.4 Michée 7.7 Psaumes 91.15
20 Naam, wanyama wa mashamba wanakutwetea wewe; Kwa maana vijito vya maji vimekauka, Na moto umeyateketeza malisho ya nyikani.
Psaumes 104.21 1 Rois 17.7 Job 38.41 1 Rois 18.5 Psaumes 147.9

Cette Bible est dans le domaine public.