Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 5
Bible en Swahili de l’est


1 Sikieni haya, enyi makuhani, sikilizeni, enyi nyumba ya Israeli, tegeni masikio yenu, enyi wa nyumba ya mfalme, kwa kuwa hukumu hii yawahusu ninyi; maana mmekuwa mtego huko Mizpa, na wavu uliotandwa juu ya Tabori.
Osée 9.8 Osée 6.9 Osée 4.1 Juges 4.6 Osée 10.15
2 Nao walioasi wameongeza sana ufisadi wao; lakini mimi ndiye awakaripiaye wote pia.
Osée 9.15 Esaïe 29.15 Osée 6.9 Psaumes 140.1-140.5 Sophonie 3.1-3.2
3 Mimi namjua Efraimu, wala Israeli hakufichwa nisimwone; maana sasa, Ee Efraimu, umefanya uzinzi; Israeli ametiwa unajisi.
Amos 3.2 Osée 8.11 Deutéronome 33.17 Genèse 48.19-48.20 1 Rois 14.14-14.16
4 Matendo yao hayatawaacha kumgeukia Mungu wao; maana roho ya uzinzi imo ndani yao, wala hawamjui Bwana.
Osée 4.12 1 Jean 2.3-2.4 2 Thessaloniciens 2.11-2.12 Jean 3.19-3.20 Jean 16.3
5 Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; kwa sababu hiyo, Israeli na Efraimu watajikwaa katika uovu wao. Yuda naye atajikwaa pamoja nao.
Osée 7.10 Ezéchiel 23.31-23.35 Amos 5.2 Osée 4.5 Proverbes 11.21
6 Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng’ombe wamtafute Bwana; lakini hawatamwona; amejitenga nao.
Michée 6.6-6.7 Proverbes 1.28 Jean 7.34 Ezéchiel 8.6 Proverbes 15.8
7 Wametenda kwa hila juu ya Bwana; maana wamezaa wana wageni; sasa mwezi huu uandamao utawala pamoja na mashamba yao.
Osée 6.7 Jérémie 3.20 Esaïe 48.8 Psaumes 144.11 Néhémie 13.23-13.24

Punition d’Israël et Juda

8 Pigeni tarumbeta katika Gibea, na baragumu katika Rama; pazeni sauti ya hofu katika Beth-Aveni; nyuma yako, Ee Benyamini!
Osée 9.9 Osée 4.15 1 Samuel 15.34 Joël 2.1 Jérémie 4.5
9 Efraimu atakuwa ukiwa siku ya kukemewa; katika kabila za Israeli nimetangaza habari itakayotokea halafu bila shaka.
Zacharie 1.6 Esaïe 46.10 Osée 9.11-9.17 Esaïe 28.1-28.4 Esaïe 48.5
10 Wakuu wa Yuda ni kama watu waondoao alama ya mpaka; nitawamwagia ghadhabu yangu kama maji.
Deutéronome 19.14 Deutéronome 27.17 Psaumes 32.6 Psaumes 93.3-93.4 Luc 6.49
11 Efraimu ameonewa, amesetwa katika hukumu, kwa sababu alikuwa radhi kufuata ubatili.
Deutéronome 28.33 Michée 6.16 1 Rois 12.26-12.33 Amos 5.11-5.12 2 Rois 15.29
12 Kwa sababu hiyo mimi nimekuwa kama nondo kwa Efraimu, nimekuwa kama ubovu kwa nyumba ya Yuda.
Esaïe 51.8 Job 13.28 Marc 9.43-9.48 Jonas 4.7 Esaïe 50.9
13 Efraimu alipouona ugonjwa wake, na Yuda jeraha yake, ndipo Efraimu alipokwenda kwa Ashuru, akatuma watu kwa mfalme Yarebu; lakini yeye hawezi kuwapoza, wala hatawaponya jeraha yenu.
Osée 7.11 Osée 10.6 Osée 12.1 2 Rois 15.19 Osée 8.9
14 Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama mwana-simba kwa nyumba ya Yuda; mimi, naam, mimi nitararua, kisha nitakwenda zangu; nitachukulia mbali, wala hapatakuwa na mtu wa kupokonya.
Psaumes 7.2 Michée 5.8 Osée 13.7-13.8 Psaumes 50.22 Esaïe 5.29
15 Nitakwenda zangu niparudie mahali pangu, hata watakapoungama makosa yao na kunitafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.
Esaïe 26.16 Psaumes 78.34 Jérémie 2.27 Jérémie 3.13 Psaumes 50.15

Cette Bible est dans le domaine public.