Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 5.15
Bible en Swahili de l’est


1 Sikieni haya, enyi makuhani, sikilizeni, enyi nyumba ya Israeli, tegeni masikio yenu, enyi wa nyumba ya mfalme, kwa kuwa hukumu hii yawahusu ninyi; maana mmekuwa mtego huko Mizpa, na wavu uliotandwa juu ya Tabori.
Osée 9.8 Osée 6.9 Osée 4.1 Juges 4.6 1 Rois 14.7-14.16
2 Nao walioasi wameongeza sana ufisadi wao; lakini mimi ndiye awakaripiaye wote pia.
Osée 9.15 Esaïe 29.15 Osée 6.9 Jérémie 11.18-11.19 Jérémie 5.3
3 Mimi namjua Efraimu, wala Israeli hakufichwa nisimwone; maana sasa, Ee Efraimu, umefanya uzinzi; Israeli ametiwa unajisi.
Amos 3.2 Hébreux 4.13 Amos 5.12 Osée 5.11 Osée 6.4
4 Matendo yao hayatawaacha kumgeukia Mungu wao; maana roho ya uzinzi imo ndani yao, wala hawamjui Bwana.
Osée 4.12 1 Jean 2.3-2.4 Jérémie 9.24 Osée 4.6 Psaumes 36.1-36.4
5 Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; kwa sababu hiyo, Israeli na Efraimu watajikwaa katika uovu wao. Yuda naye atajikwaa pamoja nao.
Osée 7.10 Amos 5.2 Ezéchiel 23.31-23.35 Esaïe 59.12 2 Rois 17.19-17.20
6 Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng’ombe wamtafute Bwana; lakini hawatamwona; amejitenga nao.
Michée 6.6-6.7 Proverbes 1.28 Lamentations 3.44 Jérémie 7.4 Jean 7.34
7 Wametenda kwa hila juu ya Bwana; maana wamezaa wana wageni; sasa mwezi huu uandamao utawala pamoja na mashamba yao.
Osée 6.7 Jérémie 3.20 Esaïe 48.8 Psaumes 144.7 Osée 2.4

Punition d’Israël et Juda

8 Pigeni tarumbeta katika Gibea, na baragumu katika Rama; pazeni sauti ya hofu katika Beth-Aveni; nyuma yako, Ee Benyamini!
Osée 4.15 Osée 9.9 Jérémie 4.5 1 Samuel 15.34 Joël 2.1
9 Efraimu atakuwa ukiwa siku ya kukemewa; katika kabila za Israeli nimetangaza habari itakayotokea halafu bila shaka.
Osée 9.11-9.17 Zacharie 1.6 Esaïe 46.10 Esaïe 28.1-28.4 Amos 7.9
10 Wakuu wa Yuda ni kama watu waondoao alama ya mpaka; nitawamwagia ghadhabu yangu kama maji.
Deutéronome 19.14 Deutéronome 27.17 Psaumes 32.6 Psaumes 93.3-93.4 Psaumes 88.17
11 Efraimu ameonewa, amesetwa katika hukumu, kwa sababu alikuwa radhi kufuata ubatili.
Michée 6.16 Deutéronome 28.33 1 Rois 12.26-12.33 Amos 5.11-5.12 2 Rois 15.29
12 Kwa sababu hiyo mimi nimekuwa kama nondo kwa Efraimu, nimekuwa kama ubovu kwa nyumba ya Yuda.
Esaïe 51.8 Job 13.28 Jonas 4.7 Esaïe 50.9 Proverbes 12.4
13 Efraimu alipouona ugonjwa wake, na Yuda jeraha yake, ndipo Efraimu alipokwenda kwa Ashuru, akatuma watu kwa mfalme Yarebu; lakini yeye hawezi kuwapoza, wala hatawaponya jeraha yenu.
Osée 7.11 Osée 12.1 Osée 10.6 Jérémie 30.12 2 Rois 15.19
14 Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama mwana-simba kwa nyumba ya Yuda; mimi, naam, mimi nitararua, kisha nitakwenda zangu; nitachukulia mbali, wala hapatakuwa na mtu wa kupokonya.
Michée 5.8 Psaumes 7.2 Osée 13.7-13.8 Esaïe 5.29 Psaumes 50.22
15 Nitakwenda zangu niparudie mahali pangu, hata watakapoungama makosa yao na kunitafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.
Psaumes 78.34 Esaïe 26.16 Psaumes 50.15 Jérémie 29.12-29.14 Jérémie 2.27

Cette Bible est dans le domaine public.