1 Sikieni haya, enyi makuhani, sikilizeni, enyi nyumba ya Israeli, tegeni masikio yenu, enyi wa nyumba ya mfalme, kwa kuwa hukumu hii yawahusu ninyi; maana mmekuwa mtego huko Mizpa, na wavu uliotandwa juu ya Tabori.
Osée 9.8  Osée 6.9  Juges 4.6  Osée 4.1  Michée 3.9  
 2 Nao walioasi wameongeza sana ufisadi wao; lakini mimi ndiye awakaripiaye wote pia.
Osée 9.15  Esaïe 29.15  Osée 6.9  Jérémie 6.28  Amos 4.6-4.12  
 3 Mimi namjua Efraimu, wala Israeli hakufichwa nisimwone; maana sasa, Ee Efraimu, umefanya uzinzi; Israeli ametiwa unajisi.
Amos 3.2  1 Rois 12.26-12.33  Osée 5.9  Apocalypse 3.15  Osée 8.11  
 4 Matendo yao hayatawaacha kumgeukia Mungu wao; maana roho ya uzinzi imo ndani yao, wala hawamjui Bwana.
Osée 4.12  1 Jean 2.3-2.4  Psaumes 36.1-36.4  Psaumes 78.8  Osée 4.1  
 5 Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; kwa sababu hiyo, Israeli na Efraimu watajikwaa katika uovu wao. Yuda naye atajikwaa pamoja nao.
Osée 7.10  Ezéchiel 23.31-23.35  Amos 5.2  Proverbes 30.13  Proverbes 11.5  
 6 Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng’ombe wamtafute Bwana; lakini hawatamwona; amejitenga nao.
Michée 6.6-6.7  Proverbes 1.28  Lamentations 3.44  Jérémie 7.4  Jean 7.34  
 7 Wametenda kwa hila juu ya Bwana; maana wamezaa wana wageni; sasa mwezi huu uandamao utawala pamoja na mashamba yao.
Osée 6.7  Jérémie 3.20  Esaïe 48.8  Malachie 2.11-2.15  Esaïe 59.13  
 8 Pigeni tarumbeta katika Gibea, na baragumu katika Rama; pazeni sauti ya hofu katika Beth-Aveni; nyuma yako, Ee Benyamini!
Osée 4.15  Osée 9.9  Jérémie 4.5  1 Samuel 15.34  Joël 2.1  
 9 Efraimu atakuwa ukiwa siku ya kukemewa; katika kabila za Israeli nimetangaza habari itakayotokea halafu bila shaka.
Osée 9.11-9.17  Zacharie 1.6  Esaïe 46.10  Esaïe 28.1-28.4  Osée 13.1-13.3  
 10 Wakuu wa Yuda ni kama watu waondoao alama ya mpaka; nitawamwagia ghadhabu yangu kama maji.
Deutéronome 19.14  Psaumes 93.3-93.4  Deutéronome 27.17  Psaumes 32.6  Psaumes 88.17  
 11 Efraimu ameonewa, amesetwa katika hukumu, kwa sababu alikuwa radhi kufuata ubatili.
Deutéronome 28.33  Michée 6.16  1 Rois 12.26-12.33  2 Rois 15.29  2 Rois 15.16-15.20  
 12 Kwa sababu hiyo mimi nimekuwa kama nondo kwa Efraimu, nimekuwa kama ubovu kwa nyumba ya Yuda.
Esaïe 51.8  Job 13.28  Proverbes 12.4  Marc 9.43-9.48  Jonas 4.7  
 13 Efraimu alipouona ugonjwa wake, na Yuda jeraha yake, ndipo Efraimu alipokwenda kwa Ashuru, akatuma watu kwa mfalme Yarebu; lakini yeye hawezi kuwapoza, wala hatawaponya jeraha yenu.
Osée 7.11  Osée 10.6  Osée 12.1  Jérémie 30.12  2 Rois 15.19  
 14 Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama mwana-simba kwa nyumba ya Yuda; mimi, naam, mimi nitararua, kisha nitakwenda zangu; nitachukulia mbali, wala hapatakuwa na mtu wa kupokonya.Michée 5.8  Psaumes 7.2  Osée 13.7-13.8  Esaïe 5.29  Psaumes 50.22  
 15 Nitakwenda zangu niparudie mahali pangu, hata watakapoungama makosa yao na kunitafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.
Esaïe 26.16  Psaumes 78.34  Psaumes 50.15  Jérémie 29.12-29.14  Jérémie 2.27