1 Sikieni haya, enyi makuhani, sikilizeni, enyi nyumba ya Israeli, tegeni masikio yenu, enyi wa nyumba ya mfalme, kwa kuwa hukumu hii yawahusu ninyi; maana mmekuwa mtego huko Mizpa, na wavu uliotandwa juu ya Tabori.
Osée 9.8  Osée 6.9  Osée 4.1  Juges 4.6  Osée 10.15  
 2 Nao walioasi wameongeza sana ufisadi wao; lakini mimi ndiye awakaripiaye wote pia.
Osée 9.15  Esaïe 29.15  Osée 6.9  Psaumes 140.1-140.5  Sophonie 3.1-3.2  
 3 Mimi namjua Efraimu, wala Israeli hakufichwa nisimwone; maana sasa, Ee Efraimu, umefanya uzinzi; Israeli ametiwa unajisi.
Amos 3.2  Osée 8.11  Deutéronome 33.17  Genèse 48.19-48.20  1 Rois 14.14-14.16  
 4 Matendo yao hayatawaacha kumgeukia Mungu wao; maana roho ya uzinzi imo ndani yao, wala hawamjui Bwana.
Osée 4.12  1 Jean 2.3-2.4  2 Thessaloniciens 2.11-2.12  Jean 3.19-3.20  Jean 16.3  
 5 Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; kwa sababu hiyo, Israeli na Efraimu watajikwaa katika uovu wao. Yuda naye atajikwaa pamoja nao.
Osée 7.10  Ezéchiel 23.31-23.35  Amos 5.2  Osée 4.5  Proverbes 11.21  
 6 Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng’ombe wamtafute Bwana; lakini hawatamwona; amejitenga nao.
Michée 6.6-6.7  Proverbes 1.28  Jean 7.34  Ezéchiel 8.6  Proverbes 15.8  
 7 Wametenda kwa hila juu ya Bwana; maana wamezaa wana wageni; sasa mwezi huu uandamao utawala pamoja na mashamba yao.
Osée 6.7  Jérémie 3.20  Esaïe 48.8  Psaumes 144.11  Néhémie 13.23-13.24  
 8 Pigeni tarumbeta katika Gibea, na baragumu katika Rama; pazeni sauti ya hofu katika Beth-Aveni; nyuma yako, Ee Benyamini!
Osée 9.9  Osée 4.15  1 Samuel 15.34  Joël 2.1  Jérémie 4.5  
 9 Efraimu atakuwa ukiwa siku ya kukemewa; katika kabila za Israeli nimetangaza habari itakayotokea halafu bila shaka.
Zacharie 1.6  Esaïe 46.10  Osée 9.11-9.17  Esaïe 28.1-28.4  Esaïe 48.5  
 10 Wakuu wa Yuda ni kama watu waondoao alama ya mpaka; nitawamwagia ghadhabu yangu kama maji.
Deutéronome 19.14  Deutéronome 27.17  Psaumes 32.6  Psaumes 93.3-93.4  Luc 6.49  
 11 Efraimu ameonewa, amesetwa katika hukumu, kwa sababu alikuwa radhi kufuata ubatili.
Deutéronome 28.33  Michée 6.16  1 Rois 12.26-12.33  Amos 5.11-5.12  2 Rois 15.29  
 12 Kwa sababu hiyo mimi nimekuwa kama nondo kwa Efraimu, nimekuwa kama ubovu kwa nyumba ya Yuda.Esaïe 51.8  Job 13.28  Marc 9.43-9.48  Jonas 4.7  Esaïe 50.9  
 13 Efraimu alipouona ugonjwa wake, na Yuda jeraha yake, ndipo Efraimu alipokwenda kwa Ashuru, akatuma watu kwa mfalme Yarebu; lakini yeye hawezi kuwapoza, wala hatawaponya jeraha yenu.
Osée 7.11  Osée 10.6  Osée 12.1  2 Rois 15.19  Osée 8.9  
 14 Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama mwana-simba kwa nyumba ya Yuda; mimi, naam, mimi nitararua, kisha nitakwenda zangu; nitachukulia mbali, wala hapatakuwa na mtu wa kupokonya.
Psaumes 7.2  Michée 5.8  Osée 13.7-13.8  Psaumes 50.22  Esaïe 5.29  
 15 Nitakwenda zangu niparudie mahali pangu, hata watakapoungama makosa yao na kunitafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.
Esaïe 26.16  Psaumes 78.34  Jérémie 2.27  Jérémie 3.13  Psaumes 50.15