Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 5.11
Bible en Swahili de l’est


1 Sikieni haya, enyi makuhani, sikilizeni, enyi nyumba ya Israeli, tegeni masikio yenu, enyi wa nyumba ya mfalme, kwa kuwa hukumu hii yawahusu ninyi; maana mmekuwa mtego huko Mizpa, na wavu uliotandwa juu ya Tabori.
Osée 9.8 Osée 6.9 Juges 4.6 Osée 4.1 Osée 9.11-9.17
2 Nao walioasi wameongeza sana ufisadi wao; lakini mimi ndiye awakaripiaye wote pia.
Osée 9.15 Esaïe 29.15 Osée 6.9 Amos 4.6-4.12 Psaumes 140.1-140.5
3 Mimi namjua Efraimu, wala Israeli hakufichwa nisimwone; maana sasa, Ee Efraimu, umefanya uzinzi; Israeli ametiwa unajisi.
Amos 3.2 Osée 5.9 Apocalypse 3.15 Osée 8.11 Deutéronome 33.17
4 Matendo yao hayatawaacha kumgeukia Mungu wao; maana roho ya uzinzi imo ndani yao, wala hawamjui Bwana.
Osée 4.12 1 Jean 2.3-2.4 Psaumes 78.8 Osée 4.1 Jérémie 9.6
5 Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; kwa sababu hiyo, Israeli na Efraimu watajikwaa katika uovu wao. Yuda naye atajikwaa pamoja nao.
Osée 7.10 Ezéchiel 23.31-23.35 Amos 5.2 Proverbes 14.32 Esaïe 3.9
6 Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng’ombe wamtafute Bwana; lakini hawatamwona; amejitenga nao.
Michée 6.6-6.7 Proverbes 1.28 Lamentations 3.44 Jérémie 7.4 Jean 7.34
7 Wametenda kwa hila juu ya Bwana; maana wamezaa wana wageni; sasa mwezi huu uandamao utawala pamoja na mashamba yao.
Osée 6.7 Jérémie 3.20 Esaïe 48.8 Esaïe 59.13 Psaumes 144.11

Punition d’Israël et Juda

8 Pigeni tarumbeta katika Gibea, na baragumu katika Rama; pazeni sauti ya hofu katika Beth-Aveni; nyuma yako, Ee Benyamini!
Osée 4.15 Osée 9.9 1 Samuel 15.34 Joël 2.1 Jérémie 4.5
9 Efraimu atakuwa ukiwa siku ya kukemewa; katika kabila za Israeli nimetangaza habari itakayotokea halafu bila shaka.
Osée 9.11-9.17 Zacharie 1.6 Esaïe 46.10 Esaïe 28.1-28.4 Osée 13.1-13.3
10 Wakuu wa Yuda ni kama watu waondoao alama ya mpaka; nitawamwagia ghadhabu yangu kama maji.
Deutéronome 19.14 Psaumes 93.3-93.4 Deutéronome 27.17 Psaumes 32.6 2 Chroniques 28.16-28.22
11 Efraimu ameonewa, amesetwa katika hukumu, kwa sababu alikuwa radhi kufuata ubatili.
Deutéronome 28.33 Michée 6.16 1 Rois 12.26-12.33 2 Rois 15.16-15.20 Amos 5.11-5.12
12 Kwa sababu hiyo mimi nimekuwa kama nondo kwa Efraimu, nimekuwa kama ubovu kwa nyumba ya Yuda.
Esaïe 51.8 Job 13.28 Proverbes 12.4 Marc 9.43-9.48 Jonas 4.7
13 Efraimu alipouona ugonjwa wake, na Yuda jeraha yake, ndipo Efraimu alipokwenda kwa Ashuru, akatuma watu kwa mfalme Yarebu; lakini yeye hawezi kuwapoza, wala hatawaponya jeraha yenu.
Osée 7.11 Osée 10.6 Osée 12.1 Jérémie 30.12 2 Rois 15.19
14 Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama mwana-simba kwa nyumba ya Yuda; mimi, naam, mimi nitararua, kisha nitakwenda zangu; nitachukulia mbali, wala hapatakuwa na mtu wa kupokonya.
Michée 5.8 Psaumes 7.2 Osée 13.7-13.8 Esaïe 5.29 Psaumes 50.22
15 Nitakwenda zangu niparudie mahali pangu, hata watakapoungama makosa yao na kunitafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.
Esaïe 26.16 Psaumes 78.34 Jérémie 29.12-29.14 Jérémie 2.27 Jérémie 3.13

Cette Bible est dans le domaine public.