Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 7.7
Bible en Swahili de l’est


Imminence de la punition

1 Tena neno la Bwana likanijia, kusema,
2 Na wewe, mwanadamu, Bwana MUNGU aiambia hivi nchi ya Israeli; Ni mwisho; mwisho umezijia pembe nne za nchi.
Amos 8.2 Amos 8.10 Ezéchiel 7.5-7.6 Lamentations 4.18 Ezéchiel 11.13
3 Sasa mwisho huu unakupata, nami nitakuletea hasira yangu, nitakuhukumu sawasawa na njia zako; nami nitakupatiliza machukizo yako yote.
Ezéchiel 18.30 Ezéchiel 16.38 Ezéchiel 5.13 Ezéchiel 34.20-34.22 Ezéchiel 36.19
4 Jicho langu halitakuachilia, wala sitaona huruma; bali nitakupatiliza njia zako, na machukizo yako yatakuwa katikati yako; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 5.11 Ezéchiel 6.7 Ezéchiel 11.21 Osée 12.2 Ezéchiel 9.10
5 Bwana MUNGU asema hivi; Ni jambo baya, jambo baya la namna ya peke yake; angalia, linakuja.
2 Rois 21.12-21.13 Ezéchiel 5.9 Nahum 1.9 Daniel 9.12 Matthieu 24.21
6 Mwisho umekuja, mwisho huu umekuja; unaamka ukupate; angalia, unakuja.
Zacharie 13.7 Ezéchiel 39.8 Ezéchiel 7.3 Ezéchiel 7.10 2 Pierre 2.5
7 Ajali yako imekujia, wewe ukaaye katika nchi hii; majira yamewadia, siku ile inakaribia; siku ya fujo, wala si ya shangwe milimani.
Esaïe 22.5 Ezéchiel 12.28 Ezéchiel 12.23-12.25 Ezéchiel 7.12 Genèse 19.15
8 Basi hivi karibu nitamwaga ghadhabu yangu juu yako, nitazitimiza hasira zangu juu yako, nami nitakuhukumu sawasawa na njia zako; nami nitakupatiliza machukizo yako yote.
Ezéchiel 14.19 Ezéchiel 9.8 Esaïe 42.25 Ezéchiel 20.21 Nahum 1.6
9 Jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma; nitakupatiliza njia zako na machukizo yako yote yatakuwa katikati yako; nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, napiga.
Galates 6.7 Esaïe 9.13 Apocalypse 20.13 Michée 6.9
10 Angalia, siku hiyo; angalia, inakuja; ajali yako imetokea; fimbo imechanua, kiburi kimechipuka.
Esaïe 10.5 Psaumes 89.32 Ezéchiel 7.6 Proverbes 14.3 Daniel 4.37
11 Udhalimu umeinuka, ukawa fimbo ya uovu; hapana mtu atakayesalia miongoni mwao, wala katika jamii yao, wala kitu katika utajiri wao; wala hakutakuwa kutukuka kati yao.
Sophonie 1.18 Ezéchiel 7.23 Esaïe 59.6-59.8 Psaumes 78.64 Ezéchiel 7.2
12 Majira yamewadia, siku ile inakaribia; huyo anunuaye asifurahi, wala asihuzunike auzaye; maana ghadhabu imewapata wote jamii.
Esaïe 5.13-5.14 Ezéchiel 7.5-7.7 Jacques 5.8-5.9 Ezéchiel 7.10 1 Corinthiens 7.29-7.31
13 Kwa maana auzaye hatakirudia kilichouzwa, wajapokuwa wangali hai; kwa sababu maono haya yawahusu wote jamii; hapana mmoja atakayerudi; wala hapana mtu atakayejitia nguvu katika uovu wa maisha yake.
Lévitique 25.24-25.28 Lévitique 25.31 Ezéchiel 33.26-33.27 Psaumes 52.7 Job 15.25
14 Wamepiga tarumbeta, wameweka vitu vyote tayari; lakini hapana aendaye vitani; maana ghadhabu yangu imewapata wote jamii.
Jérémie 4.5 Ezéchiel 7.11-7.12 Esaïe 24.1-24.7 Jérémie 12.12 Jérémie 51.27
15 Upanga uko nje, na tauni na njaa zimo ndani; yeye aliye nje mashambani atakufa kwa upanga; na yeye aliye ndani ya mji, njaa na tauni zitamla.
Jérémie 14.18 Lamentations 1.20 Ezéchiel 5.12 Ezéchiel 6.12 Jérémie 15.2-15.3
16 Lakini watakaokimbia watakimbia, nao watakuwa juu ya milima kama hua wa bondeni, wote wakilia, kila mmoja katika uovu wake.
Esaïe 38.14 Esaïe 59.11 Esdras 9.15 Esaïe 37.31 Proverbes 5.11-5.14
17 Mikono yote itakuwa dhaifu, na magoti yote yatalegea kama maji.
Ezéchiel 21.7 Hébreux 12.12 Jérémie 6.24 Esaïe 13.7-13.8 Ezéchiel 22.14
18 Tena watajifungia nguo za magunia, na utisho utawafunika; na aibu itakuwa juu ya nyuso zote, na upaa juu ya vichwa vyao vyote.
Esaïe 15.2-15.3 Amos 8.10 Esaïe 3.24 Job 21.6 Ezéchiel 27.31
19 Watatupa fedha yao katika njia kuu za mji, na dhahabu yao itakuwa kama kitu cha unajisi; fedha yao na dhahabu yao hazitaweza kuwaokoa siku ya ghadhabu ya Bwana; hawatajishibisha roho zao, wala hawatajijaza matumbo yao; kwa sababu zilikuwa kwazo la uovu wao.
Sophonie 1.18 Proverbes 11.4 Esaïe 55.2 Esaïe 2.20 Ezéchiel 14.7
20 Na uzuri wa pambo lake, yeye aliuweka katika enzi, lakini wao walifanya sanamu za machukizo yao, na vitu vyao vichukizavyo, ndani yake; ndiyo maana nimeifanya kuwa kama kitu cha unajisi kwao.
Ezéchiel 24.21 Jérémie 7.30 Ezéchiel 8.15-8.16 Esaïe 64.11 Ezéchiel 9.7
21 Nami nitapatia katika mikono ya wageni pawe mateka yao, na katika mikono ya waovu wa duniani pawe mawindo yao, nao watapanajisi.
2 Rois 24.13 Psaumes 74.2-74.8 Jérémie 52.13-52.23 2 Rois 25.13-25.16 2 Chroniques 36.18-36.19
22 Tena nitaugeuza uso wangu usiwaelekee, nao watapatia unajisi mahali pangu pa siri; na wanyang’anyi wataingia humo na kupatia unajisi.
Jérémie 18.17 Psaumes 74.10-74.11 Ezéchiel 39.23-39.24 Psaumes 35.22 Psaumes 74.18-74.23
23 Ufue mnyororo; kwa maana nchi hii imejaa hukumu za damu, nao mji umejaa udhalimu.
Jérémie 27.2 Ezéchiel 9.9 2 Rois 21.16 Ezéchiel 11.6 Osée 4.2
24 Kwa sababu hiyo nitawaleta watu wa mataifa walio wabaya kabisa, nao watazimiliki nyumba zao; tena nitakikomesha kiburi chao wenye nguvu; na mahali pao patakatifu patatiwa unajisi.
Ezéchiel 28.7 Ezéchiel 33.28 Ezéchiel 21.31 Lamentations 5.2 2 Chroniques 7.19-7.20
25 Uharibifu unakuja; nao watatafuta amani, lakini haitapatikana.
Lamentations 4.17-4.18 Esaïe 57.21 Jérémie 8.15-8.16 Ezéchiel 13.16 Michée 1.12
26 Madhara yatakuja juu ya madhara, na habari ya shari juu ya habari ya shari; nao watakwenda kwa nabii kutaka maono; lakini hiyo sheria itampotea kuhani, na mashauri yatawapotea wazee.
Jérémie 4.20 Ezéchiel 14.1 Michée 3.6 Psaumes 74.9 Jérémie 37.17
27 Mfalme ataomboleza, na mkuu atavikwa ukiwa, na mikono ya watu wa nchi itataabika; nitawatenda sawasawa na njia yao; nami nitawahukumu sawasawa na kustahili kwao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Romains 2.5-2.10 Jérémie 52.8-52.11 Ezéchiel 18.30 Ezéchiel 7.4-7.8 Jacques 2.13

Cette Bible est dans le domaine public.