Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 37.24
Bible en Swahili de l’est


Réunion d’Israël et de Juda

1 Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanichukua nje katika roho ya Bwana, akaniweka chini, katikati ya bonde; nalo limejaa mifupa;
Ezéchiel 1.3 Jérémie 8.2 Ezéchiel 33.22 Ezéchiel 3.22 Luc 4.1
2 akanipitisha karibu nayo pande zote; na tazama, palikuwa na mifupa mingi katika ule uwanda! Nayo, tazama, ilikuwa mikavu sana.
Psaumes 141.7 Ezéchiel 37.11 Deutéronome 11.30
3 Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe.
Jean 11.25-11.26 Deutéronome 32.39 Jean 5.21 Hébreux 11.19 1 Samuel 2.6
4 Akaniambia tena, Toa unabii juu ya mifupa hii, uiambie, Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Bwana.
Jean 5.28-5.29 Ezéchiel 36.1 Jean 5.25 Jérémie 22.29 Jean 2.5
5 Bwana MUNGU aiambia mifupa hii maneno haya; Tazama, nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi.
Genèse 2.7 Psaumes 104.29-104.30 Ezéchiel 37.14 Ephésiens 2.5 Jean 20.22
6 Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na kuwafunika ngozi, na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Joël 2.27 Joël 3.17 Ezéchiel 35.9 Ezéchiel 34.27 Ezéchiel 39.6
7 Basi nikatoa unabii kama nilivyoamriwa; hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu; na tazama, tetemeko la nchi, na ile mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe.
Actes 4.19 1 Rois 19.11-19.13 Actes 5.20-5.29 Actes 2.37 Actes 16.26-16.29
8 Nikatazama, kumbe! Kulikuwa na mishipa juu yake, nyama ikatokea juu yake, ngozi ikaifunika juu yake; lakini haikuwamo pumzi ndani yake.
9 Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa, wapate kuishi.
Jean 3.8 Psaumes 104.30 Ezéchiel 37.14 Ezéchiel 37.5 Cantique 4.16
10 Basi nikatabiri kama alivyoniamuru; pumzi ikawaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno.
Apocalypse 11.11 Psaumes 104.30 Apocalypse 20.4-20.5
11 Kisha akaniambia, Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli; tazama, wao husema, Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yametupotea; tumekatiliwa mbali kabisa.
Ezéchiel 39.25 Ezéchiel 36.10 Psaumes 141.7 Lamentations 3.54 Psaumes 77.7-77.9
12 Basi tabiri, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitafunua makaburi yenu, na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli.
Esaïe 26.19 Osée 13.14 Esaïe 66.14 Amos 9.14-9.15 Ezéchiel 37.25
13 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu, enyi watu wangu.
Psaumes 126.2-126.3 Ezéchiel 16.62 Ezéchiel 37.6
14 Nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi, nami nitawawekeni katika nchi yenu, nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, nimesema hayo, na kuyatimiza, asema Bwana.
Ezéchiel 36.27 Joël 2.28-2.29 Ezéchiel 39.29 Ezéchiel 17.24 Esaïe 32.15
15 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
16 Na wewe mwanadamu, twaa kijiti kimoja; ukaandike juu yake, Kwa Yuda, na kwa wana wa Israeli wenzake; kisha, twaa kijiti cha pili; ukaandike juu yake, Kwa Yusufu, kijiti cha Efraimu, na kwa nyumba yote ya Israeli wenzake;
2 Chroniques 15.9 2 Chroniques 10.19 Nombres 17.2-17.3 2 Chroniques 10.17 1 Rois 12.16-12.20
17 ukaviunge pamoja kwa ajili yako hiki na hiki viwe kijiti kimoja, viwe kimoja katika mkono wako.
Esaïe 11.13 Jérémie 50.4 Osée 1.11 Ezéchiel 37.22-37.24 Sophonie 3.9
18 Na wana wa watu wangu watakapokuambia, wakisema, Je! Hutatuonyesha maana ya mambo hayo utendayo?
Ezéchiel 12.9 Ezéchiel 24.19 Ezéchiel 20.49 Ezéchiel 17.12
19 Waambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitakitwaa kijiti cha Yusufu, kilicho mkononi mwa Efraimu, na kabila za Israeli wenzake, nami nitawaweka pamoja nacho, yaani, pamoja na kijiti cha Yuda, na kuvifanya kuwa kijiti kimoja; navyo vitakuwa kimoja mkononi mwangu.
Zacharie 10.6 Ezéchiel 37.16-37.17 1 Chroniques 9.1-9.3 Colossiens 3.11 Ephésiens 2.13-2.14
20 Navyo vijiti, ambavyo uliandika juu yake, vitakuwa mkononi mwako mbele ya macho yao.
Ezéchiel 12.3 Nombres 17.6-17.9 Osée 12.10
21 Ukawaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitawatwaa wana wa Israeli toka kati ya mataifa walikokwenda, nami nitawakusanya pande zote, na kuwaleta katika nchi yao wenyewe;
Ezéchiel 36.24 Abdias 1.17-1.21 Esaïe 43.5-43.6 Jérémie 23.8 Jérémie 16.15
22 nami nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo, juu ya milima ya Israeli; na mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote; wala hawatakuwa tena mataifa mawili, wala hawatagawanyikana kuwa falme mbili tena, hata milele.
Ezéchiel 37.24 Jérémie 3.18 Jérémie 50.4 Osée 1.11 Ezéchiel 34.23-34.24
23 Wala hawatajitia uchafu tena kwa vinyago vyao, wala kwa vitu vyao vichukizavyo, wala kwa makosa yao mojawapo; lakini nitawaokoa, na kuwatoa katika makao yao yote, ambayo wamefanya dhambi ndani yake, nami nitawatakasa; basi watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
Ezéchiel 36.28-36.29 Jérémie 31.33 Jérémie 32.38-32.39 Psaumes 68.20 Ephésiens 5.26-5.27
24 Na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mfalme juu yao, nao wote watakuwa na mchungaji mmoja; nao wataenenda katika hukumu zangu, na kuzishika amri zangu, na kuzitenda.
Esaïe 40.11 Osée 3.5 Ezéchiel 37.22 Jérémie 23.5 Ezéchiel 36.27
25 Nao watakaa katika nchi niliyompa Yakobo, mtumishi wangu, walimokaa baba zenu; nao watakaa humo, wao na watoto wao, na watoto wa watoto wao, milele; na Daudi, mtumishi wangu, atakuwa mkuu wao milele.
Amos 9.15 Ezéchiel 28.25 Ezéchiel 37.24 Joël 3.20 Ezéchiel 37.26
26 Tena nitafanya agano la amani pamoja nao; litakuwa agano la milele pamoja nao; nami nitawaweka na kuwazidisha, na patakatifu pangu nitapaweka katikati yao milele.
Esaïe 55.3 Ezéchiel 34.25 Ezéchiel 36.10 Ezéchiel 43.7 Jérémie 30.19
27 Tena maskani yangu itakuwa pamoja nao; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Jean 1.14 Ezéchiel 37.23 Apocalypse 21.3 Ezéchiel 11.20 Colossiens 2.9-2.10
28 Na mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, mimi niwatakasaye Israeli, patakatifu pangu patakapokuwa katikati yao milele.
Ezéchiel 20.12 Exode 31.13 Ezéchiel 36.23 Ezéchiel 39.7 Jean 17.17-17.19

Cette Bible est dans le domaine public.