Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 14.19
Bible en Swahili de l’est


La sécheresse

1 Neno la Bwana lililomjia Yeremia, katika habari ya ukosefu wa mvua.
Jérémie 17.8
2 Yuda huomboleza, Na malango yake yamelegea; Wameketi chini wamevaa kaniki; Na kilio cha Yerusalemu kimepaa juu.
Esaïe 3.26 Jérémie 8.21 1 Samuel 5.12 Lamentations 4.8-4.9 Zacharie 7.13
3 Na wakuu wao huwatuma watoto wao kwenye maji; Nao hufika visimani wasione maji; Hurudi, na vyombo vyao ni vitupu; Wametahayarika na kufadhaika, Na kuvifunika vichwa vyao.
2 Samuel 15.30 Psaumes 40.14 2 Rois 18.31 Amos 4.8 Jérémie 2.13
4 Kwa sababu ya nchi iliyopasuka, Kwa kuwa mvua haikunyesha katika nchi, Wenye kulima wametahayarika, Na kuvifunika vichwa vyao.
Joël 1.19-1.20 Joël 1.11 Deutéronome 28.23-28.24 Jérémie 3.3 Lévitique 26.19-26.20
5 Naam, kulungu naye uwandani amezaa, Akamwacha mwanawe kwa kuwa hapana majani.
Psaumes 29.9 Esaïe 15.6 Job 39.1-39.4
6 Na punda-mwitu husimama juu ya vilele vya milima, Hutwetea pumzi kama mbwa-mwitu; Macho yao hayaoni sawasawa, Kwa kuwa hapana majani.
Jérémie 2.24 Job 39.5-39.6 Joël 1.18 1 Samuel 14.29 Lamentations 5.17
7 Ijapokuwa maovu yetu yanatushuhudia, lakini utende wewe kwa ajili ya jina lako, Ee Bwana, maana kurudi nyuma kwetu ni kwingi; tumekutenda dhambi.
Psaumes 25.11 Osée 5.5 Jérémie 14.20-14.21 Esaïe 59.12 Jérémie 5.6
8 Wewe uliye tumaini la Israeli, wewe uliye Mwokozi wake wakati wa taabu, kwa nini wewe umekuwa kama mtu akaaye katika nchi, hali ya mgeni, na kama mtu mwenye kusafiri, ageukaye upande ili kukaa usiku mmoja tu?
Jérémie 17.13 Psaumes 50.15 Esaïe 43.3 Esaïe 43.11 Psaumes 37.39-37.40
9 Kwa nini wewe umekuwa kama mtu aliyesituka, kama shujaa asiyeweza kuokoa? Lakini wewe, Bwana, u katikati yetu, nasi tunaitwa kwa jina lako; usituache.
Esaïe 63.19 Esaïe 59.1 Psaumes 46.5 Jérémie 15.16 Exode 29.45-29.46
10 Bwana awaambia watu hawa hivi, Hivyo ndivyo walivyopenda kutanga-tanga; hawakuizuia miguu yao; basi, Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao, atawapatiliza dhambi zao.
Osée 9.9 Psaumes 119.101 Osée 8.13 Jérémie 6.20 Amos 5.22

Les prétendus prophètes

11 Naye Bwana akaniambia, Usiwaombee watu hawa wapate heri.
Jérémie 7.16 Jérémie 11.14 Exode 32.10 Jérémie 15.1 Exode 32.32-32.34
12 Wafungapo, mimi sitasikia kilio chao; na watoapo sadaka za kuteketezwa na sadaka ya unga, sitazitakabali; bali nitawaangamiza kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni.
Jérémie 6.20 Ezéchiel 8.18 Michée 3.4 Proverbes 1.28 Jérémie 11.11
13 Ndipo nikasema, Aa, Bwana, MUNGU! Tazama, manabii huwaambia, Hamtauona upanga, wala hamtakuwa na njaa; bali nitawapa amani iliyo thabiti mahali hapa.
Jérémie 6.14 Jérémie 23.17 Jérémie 4.10 Jérémie 8.11 Jérémie 28.2-28.5
14 Ndipo Bwana akaniambia, Hao manabii wanatabiri uongo kwa jina langu mimi; mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao; wanawapeni unabii wa maono ya uongo, na uaguzi, na neno la ubatili, na hadaa ya mioyo yao.
Jérémie 29.8-29.9 Ezéchiel 12.24 Michée 3.11 Jérémie 27.9-27.10 Lamentations 2.14
15 Basi, kwa hiyo Bwana asema hivi, Kwa habari za manabii wanaotabiri kwa jina langu, wala mimi sikuwatuma, lakini husema, Upanga na njaa havitaingia katika nchi hii; Kwa upanga na njaa manabii hao wataangamizwa.
Ezéchiel 14.10 Jérémie 5.12-5.13 Jérémie 6.15 Jérémie 29.20-29.21 Apocalypse 19.20
16 Na watu hao, waliopewa unabii na wao, watatupwa nje katika njia kuu za Yerusalemu kwa sababu ya upanga na njaa; wala hawatakuwa na mtu wa kuwazika, wao na wake zao, na wana wao, na binti zao; maana nitamwaga uovu wao wenyewe juu yao.
Jérémie 15.2-15.3 Psaumes 79.2-79.3 Jérémie 7.33 Proverbes 1.31 Jérémie 18.21
17 Nawe utawaambia neno hili, Macho yangu na yatiririke machozi, usiku na mchana, wala yasikome; kwa maana bikira, binti ya watu wangu, amevunjika mavunjiko makuu, kwa jeraha isiyoponyeka.
Jérémie 9.1 Jérémie 8.21 Lamentations 1.15-1.16 Jérémie 13.17 Lamentations 2.13
18 Nikitoka kwenda shambani, tazama, wako huko waliouawa kwa upanga! Na nikiingia mjini, tazama, wamo humo wanaougua kwa sababu ya njaa! Maana nabii na kuhani, wote wawili, huenda huko na huko katika nchi, wala hawana maarifa.
Ezéchiel 7.15 Lamentations 1.20 Jérémie 8.10 Jérémie 52.6-52.7 Jérémie 5.31

Perplexité de Jérémie

19 Je! Umemkataa Yuda kabisa? Roho yako imeichukia Sayuni? Mbona umetupiga, tusiwe na dawa ya kutuponya? Tulitazamia amani, lakini hayakuja mema yo yote, tulitazamia wakati wa kupona, na tazama, kufadhaika tu!
Jérémie 8.15 Lamentations 5.22 Jérémie 6.30 Jérémie 15.18 1 Thessaloniciens 5.3
20 Ee Bwana, tunakiri uovu wetu, na ubaya wa baba zetu; maana tumekutenda dhambi.
Psaumes 32.5 Néhémie 9.2 Jérémie 3.25 Lévitique 26.40-26.42 Psaumes 106.6-106.48
21 Usituchukie, kwa ajili ya jina lako; usikifedheheshe kiti cha enzi cha utukufu wako, kumbuka, usilivunje agano ulilofanya nasi.
Jérémie 14.7 Psaumes 106.45 Jérémie 3.17 Jérémie 17.12 Daniel 9.15-9.19
22 Je! Katika vitu vya ubatili vya mataifa, kiko kitu kiwezacho kuleta mvua? Je! Mbingu zaweza kutoa manyunyu? Je! Si wewe, Ee Bwana, Mungu wetu? Kwa sababu hiyo tutakungoja; kwa kuwa wewe umevifanya vitu hivi vyote.
Esaïe 30.23 Jérémie 5.24 Psaumes 135.7 Deutéronome 32.21 Esaïe 41.29

Cette Bible est dans le domaine public.