Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 10.18
Bible en Swahili de l’est


L’Éternel et les idoles

1 Enyi nyumba ya Israeli, lisikieni neno awaambialo Bwana;
Jérémie 22.2 Osée 4.1 1 Thessaloniciens 2.13 Jérémie 13.15-13.17 Amos 7.16
2 Bwana asema hivi, Msijifunze njia ya mataifa, wala msishangae kwa sababu ya ishara za mbinguni; maana mataifa hushangaa kwa sababu ya ishara hizo.
Lévitique 20.23 Lévitique 18.3 Esaïe 47.12-47.14 Luc 21.25-21.28 Deutéronome 12.30-12.31
3 Maana desturi za watu hao ni ubatili, maana mtu mmoja hukata mti mwituni, kazi ya mikono ya fundi na shoka.
Esaïe 44.9-44.20 Esaïe 45.20 Jérémie 10.8 Romains 1.21 Esaïe 40.19-40.31
4 Huupamba kwa fedha na dhahabu; huukaza kwa misumari na nyundo, usitikisike.
Esaïe 46.7 Esaïe 40.19-40.20 Psaumes 135.15 Psaumes 115.4 Esaïe 41.6-41.7
5 Mfano wao ni mfano wa mtende, kazi ya cherehani, hawasemi; hawana budi kuchukuliwa, kwa sababu hawawezi kwenda. Usiwaogope; kwa maana hawawezi kutenda uovu, wala hawana uwezo wa kutenda mema.
Esaïe 46.7 1 Corinthiens 12.2 Esaïe 41.23-41.24 Habakuk 2.19 Esaïe 46.1
6 Hapana hata mmoja aliye kama wewe, Ee Bwana; wewe ndiwe uliye mkuu, na jina lako ni kuu katika uweza.
Psaumes 96.4 Exode 15.11 Psaumes 48.1 Esaïe 12.6 Deutéronome 33.26
7 Ni nani asiyekucha wewe, Ee mfalme wa mataifa? Maana hii ni sifa yako wewe; kwa kuwa miongoni mwa wenye hekima wote wa mataifa, na katika hali yao ya enzi yote pia, hapana hata mmoja kama wewe.
Apocalypse 15.4 Psaumes 22.28 Jérémie 5.22 1 Corinthiens 1.19-1.20 Psaumes 86.9
8 Lakini wote pia huwa kama wanyama, ni wapumbavu. Haya ni maelezo ya sanamu, ni shina la mti tu.
Esaïe 41.29 Jérémie 10.14 Zacharie 10.2 Habakuk 2.18 Psaumes 115.8
9 Iko fedha iliyofuliwa ikawa mabamba, iliyoletwa kutoka Tarshishi, na dhahabu kutoka Ufazi, kazi ya stadi na ya mikono ya mfua dhahabu; mavazi yao ni rangi ya samawi na urujuani; hayo yote ni kazi ya mafundi yao.
Psaumes 115.4 Daniel 10.5 Esaïe 40.19 1 Rois 10.22 Ezéchiel 27.12
10 Bali Bwana ndiye Mungu wa kweli; Ndiye Mungu aliye hai, Mfalme wa milele; Mbele za ghadhabu yake nchi yatetemeka, Wala mataifa hawawezi kustahimili hasira yake.
Deutéronome 32.4 Nahum 1.6 Esaïe 57.15 Psaumes 31.5 Psaumes 76.7
11 Mtawaambia hivi, Miungu hiyo isiyofanya mbingu na nchi, hiyo itaangamia katika nchi, nayo itatoweka chini ya mbingu.
Psaumes 96.5 Esaïe 2.18 Zacharie 13.2 Sophonie 2.11 Jérémie 10.15
12 Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu.
Job 9.8 Genèse 1.1 Esaïe 40.22 Job 38.4-38.7 Psaumes 78.69
13 Atoapo sauti yake, pana mshindo wa maji mbinguni, Naye hupandisha mawingu toka ncha za nchi; Huifanyia mvua umeme, Huutoa upepo katika hazina zake.
Psaumes 135.7 Job 38.34-38.35 Job 38.22 Psaumes 68.33 Exode 9.23
14 Kila mtu amekuwa kama mnyama, hana maarifa; Kila mfua dhahabu amefedheheshwa na sanamu yake ya kuchonga; Maana sanamu yake ya kuyeyuka ni uongo, Wala hamna pumzi ndani yake.
Esaïe 46.7-46.8 Jérémie 51.17-51.18 Jérémie 10.8 Psaumes 135.16-135.18 Proverbes 30.2
15 Ni ubatili tu, ni kazi za udanganyifu; Wakati wa kujiliwa kwao watapotea.
Esaïe 41.24 Jérémie 14.22 Jérémie 51.18 Jonas 2.8 Zacharie 13.2
16 Yeye, Fungu la Yakobo, siye kama hawa; Maana ndiye aliyeviumba vitu vyote; Na Israeli ni kabila ya urithi wake; Bwana wa majeshi ndilo jina lake.
Deutéronome 32.9 Jérémie 32.18 Psaumes 74.2 Jérémie 31.35 Jérémie 51.19

L’approche de la punition

17 Haya! Kusanya bidhaa yako katika nchi, wewe ukaaye katika mazingiwa.
Ezéchiel 12.3-12.12 Jérémie 6.1 Jérémie 21.13 Michée 2.10 Matthieu 24.15
18 Maana Bwana asema hivi, Tazama, wakati huu nitawatupa wenyeji wa nchi hii kama kwa kombeo, nitawataabisha, wapate kuona taabu.
1 Samuel 25.29 Deutéronome 28.63-28.64 Zacharie 1.6 Jérémie 15.1-15.2 Jérémie 16.13
19 Ole wangu, kwa sababu ya jeraha yangu! Pigo langu laumia; lakini nalisema, Kweli, ni huzuni yangu mimi, nami sina budi kuivumilia.
Michée 7.9 Psaumes 39.9 Jérémie 14.17 Lamentations 3.39-3.40 Jérémie 4.31
20 Hema yangu umetekwa nyara, kamba zangu zote zimekatika; watoto wangu wameniacha na kwenda zao, pia hawako. Hapana mtu atakayenitandikia tena hema yangu, na kuyatundika mapazia yangu.
Jérémie 4.20 Jérémie 31.15 Esaïe 54.2 Job 7.8 Esaïe 49.20-49.22
21 Kwa sababu wachungaji wamekuwa kama wanyama, wala hawakuuliza kwa Bwana; basi hawakufanikiwa, na makundi yao yote yametawanyika.
Jérémie 12.10 Ezéchiel 34.2-34.10 Zacharie 10.3 Esaïe 56.10-56.12 Ezéchiel 22.25-22.30
22 Sauti imesikiwa, Tazama, inakuja; mshindo mkuu kutoka nchi ya kaskazini, ili kuifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa, makao ya mbweha.
Jérémie 9.11 Habakuk 1.6-1.9 Jérémie 4.6 Jérémie 6.22 Jérémie 5.15
23 Ee Bwana, najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.
Proverbes 20.24 Proverbes 16.1 Psaumes 37.23 Psaumes 119.116-119.117 Psaumes 17.5
24 Ee Bwana, unirudi kwa haki; si kwa hasira yako, usije ukaniangamiza.
Psaumes 6.1 Psaumes 38.1 Jérémie 30.11 Habakuk 3.2 Esaïe 40.23
25 Hasira yako uwamwagie mataifa wasiokujua, na jamaa zao wasioliitia jina lako; kwa maana wamemla Yakobo, naam, wamemla kabisa na kumwangamiza, na kuyafanya makao yake kuwa ukiwa.
Psaumes 79.6-79.7 Jérémie 8.16 Psaumes 14.4 Job 18.21 Jérémie 50.17

Cette Bible est dans le domaine public.