Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 61.5
Bible en Swahili de l’est


Le salut proclamé

1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.
Luc 4.18-4.19 Luc 7.22 Esaïe 42.7 Matthieu 11.5 Psaumes 147.3
2 Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;
Matthieu 5.4 Esaïe 34.8 Esaïe 57.18 Luc 4.19 Jérémie 31.13
3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe.
Jérémie 17.7-17.8 Esaïe 61.10 Psaumes 45.7 Jean 16.20 Psaumes 30.11
4 Nao watajenga mahali pa kale palipoharibiwa, watapainua mahali palipokuwa ukiwa zamani, watatengeneza miji iliyoharibiwa, mahali palipoachwa kizazi baada ya kizazi.
Esaïe 58.12 Esaïe 49.6-49.8 Ezéchiel 36.23-36.26 Ezéchiel 36.33-36.36 Amos 9.14-9.15
5 Na wageni watasimama na kulisha makundi yenu, na watu wa kabila nyingine watakuwa wakulima wenu, na watunzaji wa mizabibu yenu.
Esaïe 14.1-14.2 Esaïe 60.10-60.14 Ephésiens 2.12-2.20
6 Bali ninyi mtaitwa makuhani wa Bwana; watu watawaiteni wahudumu wa Mungu wetu; mtakula utajiri wa mataifa, na kujisifia utukufu wao.
Exode 19.6 Esaïe 60.5-60.7 Esaïe 66.21 1 Pierre 2.9 1 Pierre 2.5
7 Badala ya aibu yenu mtapata maradufu, na badala ya fedheha wataifurahia sehemu yao; basi katika nchi yao watamiliki maradufu; furaha yao itakuwa ya milele.
Esaïe 40.2 Zacharie 9.12 Psaumes 16.11 2 Thessaloniciens 2.16 Esaïe 60.19-60.20
8 Maana mimi, Bwana, naipenda hukumu ya haki, nauchukia wivi na uovu; nami nitawalipa malipo katika kweli, nitaagana nao agano la milele.
Esaïe 55.3 Psaumes 11.7 Jérémie 32.40 Genèse 17.7 Psaumes 25.8-25.12
9 Na kizazi chao kitajulikana katika mataifa, na uzao wao katika kabila za watu; wote wawaonao watakiri ya kuwa wao ni kizazi kilichobarikiwa na Bwana.
Esaïe 44.3 Psaumes 115.14 Zacharie 8.13 Romains 11.16-11.24 Genèse 22.18
10 Nitafurahi sana katika Bwana, nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu, amenifunika vazi la haki, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu.
Apocalypse 19.7-19.8 Esaïe 49.18 Apocalypse 21.2 Psaumes 132.16 Psaumes 132.9
11 Maana kama nchi itoavyo machipuko yake, na kama bustani ioteshavyo vitu vilivyopandwa ndani yake; ndivyo Bwana MUNGU atakavyootesha haki na sifa mbele ya mataifa yote.
Esaïe 60.18 Psaumes 85.11 Psaumes 72.3 Esaïe 62.7 Psaumes 72.16

Cette Bible est dans le domaine public.