Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 45.11
Bible en Swahili de l’est


1 Haya ndiyo Bwana amwambiayo Koreshi, masihi wake,ambaye nimemshika mkono wake wa kuume,ili kutiisha mataifa mbele yake, nami nitalegeza viuno vya wafalme; ili kufungua milango mbele yake, hata malango hayatafungwa.
Esaïe 42.6 Esaïe 44.28 Esaïe 41.13 Psaumes 73.23 Jérémie 51.11
2 Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukata-kata mapingo ya chuma;
Psaumes 107.16 Esaïe 40.4 Luc 3.5 Jérémie 51.30 Esaïe 42.16
3 nami nitakupa hazina za gizani, na mali zilizofichwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni Bwana, nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli.
Jérémie 50.37 Esaïe 43.1 Exode 33.12 Esaïe 48.15 Exode 33.17
4 Kwa ajili ya Yakobo, mtumishi wangu, na Israeli, mteule wangu, nimekuita kwa jina lako; nimekupa jina la sifa; ijapokuwa hukunijua.
Actes 17.23 Esaïe 41.8-41.9 Esaïe 44.1 Esaïe 43.3-43.4 Jérémie 50.17-50.20
5 Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine; zaidi yangu mimi hapana Mungu; nitakufunga mshipi ijapokuwa hukunijua;
Esaïe 44.8 Psaumes 18.39 Esaïe 46.9 Esaïe 22.21 Psaumes 18.32
6 ili wapate kujua toka maawio ya jua, na toka magharibi, ya kuwa hapana mwingine zaidi ya mimi; Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine.
Malachie 1.11 Psaumes 46.10 Esaïe 45.5 Esaïe 37.20 Psaumes 102.15-102.16
7 Mimi naiumba nuru, na kulihuluku giza; mimi nafanya suluhu, na kuhuluku ubaya; Mimi ni Bwana, niyatendaye hayo yote.
Amos 3.6 Ecclésiaste 7.13-7.14 Amos 4.13 Nahum 1.8 Psaumes 75.7
8 Dondokeni, enyi mbingu, toka juu, Mawingu na yamwage haki; Nchi na ifunuke, ili kutoa wokovu, Nayo itoe haki ikamee pamoja; Mimi, Bwana, nimeiumba.
Esaïe 61.11 Psaumes 72.6 Joël 3.18 Osée 10.12 1 Corinthiens 3.6-3.9
9 Ole wake ashindanaye na Muumba wake! Kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je! Udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unafanya nini? Au kazi yako, Hana mikono?
Romains 9.20-9.21 Esaïe 29.16 Esaïe 64.8 Esaïe 10.15 Jérémie 50.24
10 Ole wake amwambiaye baba yake, Wazaa nini? Au mwanamke, Una utungu wa nini?
Hébreux 12.9 Deutéronome 27.16 Malachie 1.6
11 Bwana, Mtakatifu wa Israeli, na Muumba wake, asema hivi; Niulize habari za mambo yatakayokuja; mambo ya wana wangu, na habari ya kazi ya mikono yangu; haya! Niagizeni.
Marc 11.24 Esaïe 43.7 Esaïe 29.23 Jérémie 31.9 Esaïe 48.17
12 Mimi nimeiumba dunia, nimemhuluku mwanadamu juu yake; Mimi, naam, mikono yangu mimi, imezitanda mbingu, na jeshi lake lote nimeliamuru.
Esaïe 42.5 Genèse 2.1 Néhémie 9.6 Esaïe 44.24 Esaïe 45.18
13 Mimi nimemwinua katika haki, nami nitazinyosha njia zake zote; ataujenga mji wangu, naye atawaacha huru watu wangu waliohamishwa, si kwa kulipwa fedha, wala kwa kupewa zawadi, asema Bwana wa majeshi.
Esaïe 41.2 Esaïe 41.25 Esaïe 49.25 2 Chroniques 36.22-36.23 1 Pierre 1.18-1.19

Bénédictions universelles

14 Bwana asema hivi, Kazi ya Misri, na bidhaa ya Kushi, na Waseba, watu walio warefu, watakujilia, nao watakuwa wako; watakufuata; watakuja katika minyororo; wataanguka chini mbele yako, watakuomba, wakisema, Hakika Mungu yu ndani yako; wala hapana mwingine, hapana Mungu tena.
Esaïe 49.23 Jérémie 16.19 Zacharie 8.20-8.23 1 Corinthiens 14.25 Esaïe 61.5-61.6
15 Hakika wewe u Mungu ujifichaye nafsi yako, Ee Mungu wa Israeli, Mwokozi.
Esaïe 57.17 Psaumes 44.24 Esaïe 8.17 Esaïe 43.3 Jean 13.7
16 Watatahayarika, naam, watafadhaika, wote pia; wale wafanyao sanamu wataingia fadhaa pamoja.
Esaïe 44.9 Esaïe 42.17 Esaïe 44.11 Psaumes 97.7 Jérémie 10.14-10.15
17 Bali Israeli wataokolewa na Bwana kwa wokovu wa milele; ninyi hamtatahayarika, wala kufadhaika, milele na milele.
Romains 10.11 Psaumes 25.3 Esaïe 54.4 1 Pierre 2.6 Esaïe 49.23
18 Maana Bwana, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine.
Esaïe 42.5 Psaumes 115.16 Genèse 1.2 Ezéchiel 36.10-36.12 Genèse 1.26
19 Sikusema kwa siri, katika mahali pa nchi ya giza; sikuwaambia wazao wa Yakobo; Nitafuteni bure; Mimi, Bwana, nasema haki; nanena mambo ya adili.
Esaïe 48.16 2 Chroniques 15.2 Amos 5.4 Esaïe 63.1 Malachie 3.13-3.14
20 Jikusanyeni mje; na kukaribia pamoja, ninyi wa mataifa mliookoka; hawana maarifa wale wachukuao mti wa sanamu yao ya kuchonga; wamwombao mungu asiyeweza kuokoa.
Esaïe 43.9 Jérémie 10.5 Esaïe 46.1 Psaumes 115.8 Jérémie 50.28
21 Hubirini, toeni habari; naam, na wafanye mashauri pamoja; ni nani aliyeonyesha haya tangu zamani za kale? Ni nani aliyeyahubiri hapo zamani? Si mimi, Bwana? Wala hapana Mungu zaidi ya mimi; Mungu mwenye haki, mwokozi; hapana mwingine zaidi ya mimi.
Esaïe 45.5 Esaïe 43.11 Esaïe 43.9 Esaïe 41.22-41.23 Esaïe 44.7-44.8
22 Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.
Jean 6.40 Hébreux 12.2 Zacharie 12.10 2 Chroniques 20.12 Michée 7.7
23 Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.
Philippiens 2.10 Romains 14.10-14.12 Psaumes 63.11 Esaïe 55.11 Hébreux 6.13-6.18
24 Mmoja ataniambia, Kwa Bwana, peke yake, iko haki na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika.
Esaïe 41.11 Esaïe 26.4 Jérémie 23.5-23.6 Psaumes 21.8-21.9 Apocalypse 22.17
25 Katika Bwana wazao wote wa Israeli watapewa haki, na kutukuka.
Esaïe 41.16 Esaïe 45.24 Esaïe 45.19 Galates 6.14 2 Corinthiens 10.17

Cette Bible est dans le domaine public.