1 Siku hizo Hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na Isaya nabii, mwana wa Amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona.
2 Samuel 17.23  2 Chroniques 32.24  2 Rois 20.1-20.11  Esaïe 38.1-38.8  Esaïe 1.1  
 2 Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana,
Psaumes 50.15  Matthieu 6.6  1 Rois 8.30  Psaumes 91.15  
 3 akasema, Ee Bwana, kumbuka haya, nakusihi, kwamba nimekwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.
Néhémie 13.14  1 Chroniques 29.19  Psaumes 6.8  Psaumes 32.2  1 Rois 2.4  
 4 Ikawa, neno la Bwana likamjia Isaya, kusema, 
5 Enenda ukamwambie Hezekia, Bwana, Mungu wa Daudi, baba yako, asema hivi, Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama, nitaziongeza siku zako, kiasi cha miaka kumi na mitano.
2 Rois 18.2  Matthieu 22.32  1 Chroniques 17.2-17.4  Luc 1.13  Psaumes 39.12  
 6 Nami nitakuokoa wewe, na mji huu, na mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitaulinda mji huu.
Esaïe 37.35  2 Timothée 4.17  Esaïe 31.4-31.5  Esaïe 12.6  2 Chroniques 32.22  
 7 Jambo hili liwe ishara kwako, itokayo kwa Bwana, ya kuwa Bwana atalitimiza jambo hili alilolisema;
Juges 6.37-6.39  Esaïe 37.30  Esaïe 38.22  Esaïe 7.11-7.14  Genèse 9.13  
 8 Tazama, nitakirudisha nyuma kivuli madaraja kumi, ambayo kilishuka juu ya duara ya Ahazi kwa sababu ya jua. Basi jua likarudi madaraja kumi katika hiyo duara, ambayo limekwisha kushuka.
2 Chroniques 32.24  2 Rois 20.9-20.11  2 Chroniques 32.31  Josué 10.12-10.14  Matthieu 16.1  
 9 Haya ndiyo maandiko ya Hezekia, mfalme wa Yuda, alipokuwa hawezi, naye akapona ugonjwa wake.
2 Chroniques 29.30  Esaïe 12.1-12.6  Psaumes 116.1-116.4  Psaumes 107.17-107.22  Exode 15.1-15.21  
 10 Nalisema, Katika usitawi wa siku zangu nitakwenda kuingia malango ya kuzimu; Nimenyimwa mabaki ya miaka yangu.
2 Corinthiens 1.9  Psaumes 102.24  Job 7.7  Psaumes 107.18  Job 6.11  
 11 Nalisema, Sitamwona Bwana, yeye Bwana, katika nchi ya walio hai; Sitamwona mwanadamu tena pamoja na hao wakaao duniani.
Psaumes 27.13  Psaumes 6.4-6.5  Psaumes 116.8-116.9  Job 35.14-35.15  Psaumes 31.22  
 12 Kao langu limeondolewa kabisa, limechukuliwa kama hema ya mchungaji; Nimekunja maisha yangu kama mfumaji; atanikatilia mbali na kitanda cha mfumi; Tangu mchana hata usiku wanimaliza.
Hébreux 1.12  Psaumes 73.14  2 Corinthiens 5.1  Job 17.1  Job 7.3-7.7  
 13 Nalijituliza hata asubuhi; kama simba, aivunja mifupa yangu yote; Tangu mchana hata usiku wanimaliza.Daniel 6.24  Psaumes 51.8  Job 16.12-16.14  1 Corinthiens 11.30-11.32  Osée 5.14  
 14 Kama mbayuwayu au korongo ndivyo nilivyolia; Naliomboleza kama hua; macho yangu yamedhoofu kwa kutazama juu; Ee Bwana, nimeonewa, na uwe mdhamini wangu.
Esaïe 59.11  Ezéchiel 7.16  Psaumes 119.122-119.123  Job 30.29  Nahum 2.7  
 15 Niseme nini? Yeye amenena nami, na yeye mwenyewe ametenda hayo; Nitakwenda polepole miaka yangu yote, kwa sababu ya uchungu wa nafsi yangu.
1 Rois 21.27  Job 7.11  Job 10.1  Jean 12.27  2 Rois 4.27  
 16 Ee Bwana, kwa mambo hayo watu huishi; Na uhai wa roho yangu u katika hayo yote; Kwa hiyo uniponye na kunihuisha.
Deutéronome 8.3  Matthieu 4.4  Psaumes 71.20  Psaumes 119.25  2 Corinthiens 4.17  
 17 Tazama; nalikuwa na uchungu mwingi kwa ajili ya amani yangu; Lakini kwa kunipenda umeniokoa na shimo la uharibifu; Kwa maana umezitupa dhambi zangu zote nyuma yako.
Esaïe 43.25  Jérémie 31.34  Psaumes 86.13  Psaumes 30.3  Jonas 2.6  
 18 Kwa kuwa kuzimu hakuwezi kukusifu; mauti haiwezi kukuadhimisha; Wale washukao shimoni hawawezi kuitarajia kweli yako.
Ecclésiaste 9.10  Psaumes 6.5  Psaumes 30.9  Nombres 16.33  Proverbes 14.32  
 19 Aliye hai, naam, aliye hai, ndiye atakayekusifu, kama mimi leo; Baba atawajulisha watoto kweli yako.
Deutéronome 6.7  Deutéronome 4.9  Psaumes 78.3-78.6  Psaumes 145.4  Genèse 18.19  
 20 Bwana yu tayari kunipa wokovu. Basi, kwa vinubi tutaziimba nyimbo zangu, Siku zote za maisha yetu nyumbani mwa Bwana.
Psaumes 9.13-9.14  Psaumes 66.13-66.15  Psaumes 33.2  Psaumes 145.2  Psaumes 30.11-30.12  
 21 Maana Isaya amesema, Na watwae mkate wa tini, wakauweke juu ya jipu, naye atapona.
Marc 7.33  2 Rois 20.7-20.8  Jean 9.6  
 22 Tena Hezekia alikuwa amesema, Iko ishara gani ya kunionyesha ya kuwa nitapanda niingie nyumbani mwa Bwana?
Psaumes 84.10-84.12  Psaumes 84.1-84.2  Jean 5.14  Psaumes 118.18-118.19  Psaumes 122.1