Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 38.12
Bible en Swahili de l’est


Maladie et guérison d’Ézéchias

1 Siku hizo Hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na Isaya nabii, mwana wa Amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona.
2 Samuel 17.23 2 Chroniques 32.24 2 Rois 20.1-20.11 Esaïe 38.1-38.8 Esaïe 37.21
2 Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana,
Matthieu 6.6 1 Rois 8.30 Psaumes 91.15 Psaumes 50.15
3 akasema, Ee Bwana, kumbuka haya, nakusihi, kwamba nimekwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.
Néhémie 13.14 1 Chroniques 29.19 Psaumes 6.8 Psaumes 32.2 Psaumes 16.8
4 Ikawa, neno la Bwana likamjia Isaya, kusema,
5 Enenda ukamwambie Hezekia, Bwana, Mungu wa Daudi, baba yako, asema hivi, Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama, nitaziongeza siku zako, kiasi cha miaka kumi na mitano.
2 Rois 18.2 2 Chroniques 34.3 Apocalypse 7.17 Actes 27.24 Psaumes 56.8
6 Nami nitakuokoa wewe, na mji huu, na mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitaulinda mji huu.
Esaïe 37.35 Esaïe 31.4-31.5 Esaïe 12.6 2 Chroniques 32.22 2 Timothée 4.17
7 Jambo hili liwe ishara kwako, itokayo kwa Bwana, ya kuwa Bwana atalitimiza jambo hili alilolisema;
Juges 6.37-6.39 Esaïe 37.30 Esaïe 7.11-7.14 Genèse 9.13 Juges 6.17-6.22
8 Tazama, nitakirudisha nyuma kivuli madaraja kumi, ambayo kilishuka juu ya duara ya Ahazi kwa sababu ya jua. Basi jua likarudi madaraja kumi katika hiyo duara, ambayo limekwisha kushuka.
2 Rois 20.9-20.11 2 Chroniques 32.31 Josué 10.12-10.14 Matthieu 16.1 2 Chroniques 32.24
9 Haya ndiyo maandiko ya Hezekia, mfalme wa Yuda, alipokuwa hawezi, naye akapona ugonjwa wake.
Esaïe 12.1-12.6 Psaumes 116.1-116.4 Psaumes 107.17-107.22 Exode 15.1-15.21 Osée 6.1-6.2
10 Nalisema, Katika usitawi wa siku zangu nitakwenda kuingia malango ya kuzimu; Nimenyimwa mabaki ya miaka yangu.
2 Corinthiens 1.9 Psaumes 102.24 Psaumes 107.18 Job 6.11 Job 17.11-17.16
11 Nalisema, Sitamwona Bwana, yeye Bwana, katika nchi ya walio hai; Sitamwona mwanadamu tena pamoja na hao wakaao duniani.
Psaumes 27.13 Psaumes 116.8-116.9 Job 35.14-35.15 Psaumes 31.22 Ecclésiaste 9.5-9.6
12 Kao langu limeondolewa kabisa, limechukuliwa kama hema ya mchungaji; Nimekunja maisha yangu kama mfumaji; atanikatilia mbali na kitanda cha mfumi; Tangu mchana hata usiku wanimaliza.
Psaumes 73.14 2 Corinthiens 5.1 Hébreux 1.12 Jacques 4.14 Psaumes 102.11
13 Nalijituliza hata asubuhi; kama simba, aivunja mifupa yangu yote; Tangu mchana hata usiku wanimaliza.
Daniel 6.24 Psaumes 51.8 1 Corinthiens 11.30-11.32 Osée 5.14 Psaumes 50.22
14 Kama mbayuwayu au korongo ndivyo nilivyolia; Naliomboleza kama hua; macho yangu yamedhoofu kwa kutazama juu; Ee Bwana, nimeonewa, na uwe mdhamini wangu.
Esaïe 59.11 Ezéchiel 7.16 Psaumes 119.122-119.123 Job 30.29 Nahum 2.7
15 Niseme nini? Yeye amenena nami, na yeye mwenyewe ametenda hayo; Nitakwenda polepole miaka yangu yote, kwa sababu ya uchungu wa nafsi yangu.
1 Rois 21.27 Job 7.11 Job 10.1 Jean 12.27 2 Rois 4.27
16 Ee Bwana, kwa mambo hayo watu huishi; Na uhai wa roho yangu u katika hayo yote; Kwa hiyo uniponye na kunihuisha.
Deutéronome 8.3 Psaumes 71.20 Psaumes 119.25 2 Corinthiens 4.17 Esaïe 64.5
17 Tazama; nalikuwa na uchungu mwingi kwa ajili ya amani yangu; Lakini kwa kunipenda umeniokoa na shimo la uharibifu; Kwa maana umezitupa dhambi zangu zote nyuma yako.
Esaïe 43.25 Jérémie 31.34 Psaumes 86.13 Psaumes 30.3 Jonas 2.6
18 Kwa kuwa kuzimu hakuwezi kukusifu; mauti haiwezi kukuadhimisha; Wale washukao shimoni hawawezi kuitarajia kweli yako.
Ecclésiaste 9.10 Psaumes 30.9 Psaumes 6.5 Nombres 16.33 Proverbes 14.32
19 Aliye hai, naam, aliye hai, ndiye atakayekusifu, kama mimi leo; Baba atawajulisha watoto kweli yako.
Deutéronome 6.7 Deutéronome 4.9 Psaumes 78.3-78.6 Genèse 18.19 Joël 1.3
20 Bwana yu tayari kunipa wokovu. Basi, kwa vinubi tutaziimba nyimbo zangu, Siku zote za maisha yetu nyumbani mwa Bwana.
Psaumes 66.13-66.15 Psaumes 33.2 Psaumes 145.2 Psaumes 30.11-30.12 Psaumes 51.15
21 Maana Isaya amesema, Na watwae mkate wa tini, wakauweke juu ya jipu, naye atapona.
2 Rois 20.7-20.8 Jean 9.6 Marc 7.33
22 Tena Hezekia alikuwa amesema, Iko ishara gani ya kunionyesha ya kuwa nitapanda niingie nyumbani mwa Bwana?
Psaumes 84.1-84.2 Jean 5.14 Psaumes 118.18-118.19 Psaumes 122.1 2 Rois 20.8

Cette Bible est dans le domaine public.