Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 37.36
Bible en Swahili de l’est


Délivrance d’Ézéchias et de Juda

1 Ikawa mfalme Hezekia aliposikia hayo, alizirarua nguo zake, akajivika nguo za magunia, akaingia katika nyumba ya Bwana.
2 Rois 19.1-19.37 Jonas 3.5-3.6 Esdras 9.5 Job 1.20-1.21 Esaïe 36.22-37.38
2 Akamtuma Eliakimu aliyekuwa msimamizi wa nyumba yake na Shebna, mwandishi, na wazee wa makuhani, wamejivika nguo za magunia, waende kwa Isaya nabii, mwana wa Amozi.
Esaïe 1.1 Joël 1.13 2 Rois 22.12-22.14 Esaïe 37.14 Esaïe 36.3
3 Wakamwambia, Hezekia asema hivi, Siku hii ni siku ya dhiki, na aibu, na matukano; maana watoto wa tayari kuzaliwa, wala hapana nguvu za kuwazaa.
Osée 13.13 Esaïe 66.9 Esaïe 33.2 Esaïe 26.17-26.18 Esaïe 25.8
4 Yamkini Bwana, Mungu wako, atayasikia maneno ya huyo amiri ambaye mfalme wa Ashuru, bwana wake, amemtuma ili amtukane Mungu aliye hai; na Bwana, Mungu wako atayakemea maneno aliyoyasikia; basi, inua dua yako kwa ajili ya mabaki yaliyobakia.
Esaïe 1.9 Esaïe 36.20 Psaumes 106.23 Esaïe 10.22 2 Rois 17.18
5 Basi, watumishi wa mfalme Hezekia wakaenda kwa Isaya.
6 Isaya akawaambia, Mwambieni bwana wenu maneno haya; Bwana asema hivi, Usiyaogope maneno uliyoyasikia, ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana.
Esaïe 7.4 Esaïe 35.4 Josué 11.6 2 Chroniques 20.15-20.20 Esaïe 41.10-41.14
7 Tazama, nitatia roho ndani yake, naye atasikia kivumi, na kurudi hata nchi yake mwenyewe, nami nitamwangusha kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.
Esaïe 37.9 Job 15.21 2 Chroniques 32.21 Esaïe 30.28-30.33 Psaumes 58.9
8 Basi yule amiri akarudi, akamkuta mfalme wa Ashuru anafanya vita juu ya Libna; kwa maana alikuwa amesikia ya kwamba ameondoka, akaacha Lakishi.
Josué 10.29 Nombres 33.20-33.21 Josué 10.31-10.34 Josué 21.13 2 Rois 8.22
9 Naye alisikia habari ya Tirhaka, mfalme wa Kushi, ya kwamba, Ametoka ili kupigana nawe; naye aliposikia hayo, akatuma wajumbe kwa Hezekia, kusema,
Esaïe 20.5 1 Samuel 23.27-23.28 Esaïe 37.7 Esaïe 18.1
10 Mwambieni Hezekia, mfalme wa Yuda, maneno haya, mkisema, Asikudanganye Mungu wako unayemtumaini, akisema, Yerusalemu hautatiwa katika mikono ya mfalme wa Ashuru.
Esaïe 36.15 2 Rois 19.10-19.13 Psaumes 22.8 2 Chroniques 32.7-32.8 Esaïe 36.20
11 Tazama, umesikia habari ya mambo yote, ambayo wafalme wa Ashuru wamezitenda nchi zote, kwa kuziangamiza kabisa je! Utaokoka wewe?
Esaïe 36.18-36.20 2 Rois 17.4-17.6 Esaïe 37.18-37.19 Esaïe 10.7-10.14 Esaïe 14.17
12 Je! Miungu ya mataifa, ambao baba zangu waliwaangamiza, wamewaokoa? Gozani, na Harani, na Resefu, na wana wa Adini waliokuwa katika Telasari?
Genèse 11.31 Actes 7.2 2 Rois 19.12 2 Rois 18.11 2 Rois 17.6
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, na mfalme wa Arpadi, na mfalme wa mji wa Sefarvaimu, wa Hena, na wa Iva?
Jérémie 49.23 Esaïe 36.19 2 Rois 17.30-17.31 2 Rois 18.34 2 Rois 19.13
14 Basi Hezekia akaupokea waraka katika mikono ya wale wajumbe, akausoma; kisha Hezekia akapanda, akaingia katika nyumba ya Bwana, akaukunjua mbele za Bwana.
Psaumes 62.1-62.3 Psaumes 123.1-123.4 1 Rois 9.3 2 Rois 19.14 Psaumes 27.5
15 Hezekia akamwomba Bwana, akisema,
Daniel 9.3-9.4 2 Chroniques 14.11 2 Rois 19.15-19.19 2 Samuel 7.18-7.29 Philippiens 4.6-4.7
16 Ee Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, ukaaye juu ya makerubi, wewe, naam, wewe peke yako, ndiwe Mungu wa falme zote za dunia. Wewe ndiwe uliyeziumba mbingu na nchi.
Psaumes 99.1 Psaumes 86.10 Exode 25.22 Colossiens 1.16 Psaumes 80.1
17 Tega sikio lako, Bwana, usikie; funua macho yako, Bwana, uone; uyasikie maneno ya Senakeribu, aliyopeleka ili kumtukana Mungu aliye hai.
2 Chroniques 6.40 Psaumes 17.6 1 Pierre 3.12 Psaumes 74.22 Esaïe 37.4
18 Ni kweli, Bwana, wafalme wa Ashuru wameziharibu nchi zote, na mashamba yao,
2 Rois 15.29 1 Chroniques 5.26 Nahum 2.11-2.12 2 Rois 16.9 2 Rois 17.6
19 na kuwatupa miungu yao motoni; kwa maana hao hawakuwa miungu, bali kazi ya mikono ya wanadamu; walikuwa miti na mawe, ndiyo sababu wakawaharibu.
Esaïe 44.17 Esaïe 36.18-36.20 Osée 8.6 Jérémie 10.11 Esaïe 26.14
20 Basi sasa, Bwana, Mungu wetu, utuokoe na mkono wake, falme zote za dunia zipate kujua ya kuwa wewe ndiwe Bwana, wewe peke yako.
Psaumes 46.10 1 Rois 18.36-18.37 Ezéchiel 36.23 Malachie 1.11 Esaïe 42.8
21 Ndipo Isaya, mwana wa Amozi, akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akisema, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kwa kuwa umeniomba juu ya Senakeribu, mfalme wa Ashuru,
Psaumes 91.15 Actes 4.31 Esaïe 58.9 2 Samuel 15.31 2 Rois 19.20-19.21
22 tamko alilolitamka Bwana katika habari zake ndilo hili; Bikira, binti Sayuni, anakudharau, anakudhihaki sana; binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake juu yako.
Job 16.4 Zacharie 2.10 Jérémie 14.17 Psaumes 9.14 Lamentations 2.13
23 Ni nani uliyemshutumu na kumtukana? Umeinua sauti yako juu ya nani, na kuinua macho yako juu? Juu ya Mtakatifu wa Israeli.
Ezéchiel 39.7 Exode 9.17 Esaïe 30.11-30.12 Habakuk 1.12-1.13 Psaumes 44.16
24 Umemshutumu Bwana kwa watumishi wako, kwa kuwa umesema, Kwa wingi wa magari yangu nimepanda juu ya vilele vya milima, mpaka mahali pa ndani ya Lebanoni; nami nitaikata mierezi yake mirefu, na misunobari yake mizuri, nami nitaingia ndani ya mahali pake palipoinuka, palipo mbali sana, msitu wa shamba lake lizaalo sana.
Esaïe 14.8 Esaïe 10.18 Daniel 4.30 Esaïe 36.9 Exode 15.9
25 Nimechimba na kunywa maji, na kwa nyayo za miguu yangu nitaikausha mito yote ya Misri.
1 Rois 20.10 Deutéronome 11.10 Esaïe 36.12 2 Rois 19.23-19.24
26 Je! Hukusikia? Ni mimi niliyeyatenda hayo tokea zamani, na kuyafanya tokea siku za kale; nikayatimiza sasa, iwe kazi yako kuangamiza miji yenye boma, ikawe chungu na magofu.
Actes 2.23 1 Pierre 2.8 Actes 4.27-4.28 Esaïe 10.5-10.6 Esaïe 10.15
27 Ndiyo sababu wenyeji wao wakawa hawana nguvu, na kufadhaika, na kuhangaika, wakawa kama majani ya mashamba, kama miche mibichi, kama majani juu ya dari, kama shamba la ngano kabla haijaiva.
Psaumes 129.6 Jérémie 37.10 Jérémie 5.10 Esaïe 40.6-40.8 1 Pierre 1.24
28 Lakini nakujua, kuketi kwako, na kutoka kwako, na kuingia kwako; na ghadhabu yako uliyonighadhibikia.
Proverbes 15.3 Apocalypse 2.13 Psaumes 139.1-139.11 Proverbes 5.21 Jérémie 23.23-23.24
29 Kwa sababu ya kunighadhibikia kwako, na kwa sababu kutakabari kwako kumefika masikioni mwangu, nitatia kulabu yangu katika pua yako, na hatamu yangu midomoni mwako, nami nitakurudisha kwa njia ile ile uliyoijia.
Esaïe 30.28 Ezéchiel 38.4 Esaïe 10.12 Esaïe 37.34 Ezéchiel 29.4
30 Na kwako wewe dalili ndiyo hii; mwaka huu mtakula vitu vimeavyo vyenyewe; na mwaka wa pili mtakula mazao ya mbegu za vitu hivyo; na mwaka wa tatu pandeni mbegu, kavuneni; mkapande mizabibu katika mashamba, mkale matunda yake.
Esaïe 7.21-7.25 1 Rois 13.3-13.5 2 Rois 20.9 Esaïe 38.7 Exode 3.12
31 Na mabaki yaliyookoka, yaliyobakia ya nyumba ya Yuda, yatatia mizizi chini, na kuzaa matunda juu.
Esaïe 27.6 2 Rois 19.30-19.31 Psaumes 80.9 Galates 3.29 Romains 9.27
32 Maana katika Yerusalemu yatatoka mabaki, nao watakaookoka katika mlima Sayuni; wivu wa Bwana wa majeshi utatimiza mambo hayo.
Esaïe 9.7 Esaïe 59.17 2 Rois 19.31 Zacharie 1.14 Joël 2.18
33 Basi, Bwana asema hivi katika habari za mfalme wa Ashuru, Yeye hataingia ndani ya mji huu, wala hatapiga mshale hapa, wala hatakuja mbele yake kwa ngao, wala hatajenga boma juu yake.
Esaïe 33.20 Esaïe 8.7-8.10 Ezéchiel 21.22 2 Rois 19.32-19.35 Luc 19.43-19.44
34 Njia ile ile aliyoijia, kwa njia hiyo atarudi zake, wala hataingia ndani ya mji huu; asema Bwana.
Esaïe 37.29 Proverbes 21.30
35 Nami nitaulinda mji huu, niuokoe kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi, mtumishi wangu.
Esaïe 31.5 Esaïe 38.6 2 Rois 20.6 Esaïe 43.25 1 Rois 15.4
36 Basi malaika wa Bwana alitoka, akaua watu mia na themanini na tano elfu katika kituo cha Waashuri, na watu walipoamka asubuhi na mapema, kumbe, hao walikuwa maiti wote pia.
Esaïe 10.12 2 Rois 19.35 Esaïe 31.8 2 Chroniques 32.21-32.22 Esaïe 10.33-10.34
37 Basi Senakeribu, mfalme wa Ashuru akaenda zake, akarudi Ninawi, akakaa huko.
Jonas 3.3 Jonas 1.2 Nahum 1.1 Esaïe 31.9 Esaïe 37.29
38 Ikawa alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisroki, mungu wake, Adrameleki na Shareza, wanawe, wakampiga kwa upanga; wakakimbilia nchi ya Ararati; naye Esar-hadoni, mwanawe, akamiliki badala yake.
Genèse 8.4 Esdras 4.2 Jérémie 51.27 2 Chroniques 32.19 2 Rois 19.36-19.37

Cette Bible est dans le domaine public.