Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 27.11
Bible en Swahili de l’est


1 Katika siku hiyo Bwana, kwa upanga wake ulio mkali, ulio mkubwa, ulio na nguvu, atamwadhibu lewiathani, nyoka yule mwepesi, na lewiathani, nyoka yule mwenye kuzonga-zonga; naye atamwua yule joka aliye baharini.
Esaïe 51.9 Esaïe 66.16 Psaumes 104.26 Apocalypse 12.3-13.2 Ezéchiel 29.3

Annonce du rétablissement d’Israël

2 Katika siku hiyo; Shamba la mizabibu la mvinyo, liimbieni.
Jérémie 2.21 Nombres 21.17 Matthieu 21.33-21.46 Luc 20.9-20.18 Psaumes 80.8-80.19
3 Mimi, Bwana, nalilinda, Nitalitia maji kila dakika, Asije mtu akaliharibu; Usiku na mchana nitalilinda.
Esaïe 58.11 1 Samuel 2.9 Genèse 9.9 Ezéchiel 34.24 Jean 10.27-10.30
4 Hasira sinayo ndani yangu; Kama mibigili na miiba ingekuwa mbele zangu, Ningepanga vita juu yake, Ningeiteketeza yote pamoja.
Esaïe 10.17 Matthieu 3.12 Hébreux 6.8 2 Samuel 23.6 Esaïe 26.20-26.21
5 Au azishike nguvu zangu, Afanye amani nami; Naam, afanye amani nami.
Job 22.21 Esaïe 25.4 Josué 10.6 Ephésiens 2.16-2.17 Colossiens 1.20-1.21
6 Siku zijazo Yakobo atatia mizizi; Israeli atatoa maua na kuchipuka; Nao watajaza uso wa ulimwengu matunda.
Osée 14.5-14.6 Esaïe 37.31 Esaïe 54.1-54.3 Psaumes 92.13-92.15 Esaïe 60.22
7 Je! Amempiga kama hilo pigo la hao waliompiga, au ameuawa kama walivyouawa wao waliouawa na yeye?
Esaïe 37.36-37.38 Esaïe 10.20-10.25 Nahum 3.19 Jérémie 51.24 Esaïe 14.22-14.23
8 Umemwadhibu kwa kiasi, ulipomfukuza; ukampepeta kwa upepo mkali katika siku ya upepo wa mashariki.
Ezéchiel 19.12 Jérémie 4.11 Jérémie 10.24 Osée 13.15 Jérémie 2.17-2.37
9 Basi, uovu wa Yakobo utatakaswa hivyo, na hayo ndiyo matunda yote ya kumwondolea dhambi yake; afanyapo mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa, hata maashera na sanamu za jua havitasimama tena.
Daniel 11.35 Esaïe 17.8 Romains 11.27 Esaïe 48.10 Hébreux 12.9-12.11
10 Kwa maana mji ulio na boma umekuwa peke yake, makao yaliyoachwa na ukiwa kama jangwa; huko ndiko atakakolisha ndama, na huko ndiko atakakolala, na kuyala matawi yake.
Esaïe 17.2 Esaïe 32.13-32.14 Jérémie 26.18 Jérémie 26.6 Michée 3.12
11 Matawi yake yatakapokauka yatavunjwa; wanawake watakuja na kuyachoma moto; kwa maana hawa si watu wenye akili; kwa sababu hiyo yeye aliyewaumba hatawahurumia, yeye aliyewafanya hatawasamehe.
Esaïe 43.7 Esaïe 44.24 Esaïe 1.3 Esaïe 43.1 Jérémie 8.7
12 Tena itakuwa katika siku hiyo, Bwana atayapiga-piga matunda yake toka gharika ya Mto hata kijito cha Misri, nanyi mtakusanywa mmoja mmoja, enyi wana wa Israeli.
Genèse 15.18 Néhémie 1.9 Esaïe 56.8 Deutéronome 30.3-30.4 Matthieu 18.12-18.14
13 Tena itakuwa katika siku hiyo, tarumbeta kubwa itapigwa, nao waliokuwa karibu na kuangamia katika nchi ya Ashuru watakuja; na hao waliotupwa katika nchi ya Misri; nao watamsujudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.
Matthieu 24.31 Lévitique 25.9 Esaïe 19.23-19.25 1 Chroniques 15.24 Esaïe 11.16

Cette Bible est dans le domaine public.