Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 20.13
Bible en Swahili de l’est


1 Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.
Osée 4.11 Proverbes 31.4 Ephésiens 5.18 Esaïe 28.7 1 Corinthiens 6.10
2 Utisho wa mfalme ni kama ngurumo ya simba; Amkasirishaye huitendea dhambi nafsi yake.
Proverbes 8.36 Proverbes 19.12 1 Rois 2.23 Ecclésiaste 10.4 Habakuk 2.10
3 Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana.
Proverbes 17.14 Proverbes 14.29 Proverbes 19.11 Proverbes 16.32 Proverbes 18.6
4 Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.
Proverbes 19.15 Proverbes 10.4 Proverbes 19.24 Proverbes 24.34 Matthieu 25.24-25.28
5 Mashauri ya moyoni ni kama kilindi; Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.
Proverbes 18.4 1 Corinthiens 2.11 Psaumes 64.6
6 Wanadamu hutangaza kila mtu hisani yake mwenyewe; Bali mtu aliye mwaminifu, ni nani awezaye kumpata?
Luc 18.8 Matthieu 6.2 Psaumes 12.1 Luc 18.11 Proverbes 25.14
7 Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake.
Psaumes 112.2 Psaumes 37.26 Proverbes 19.1 2 Corinthiens 1.12 Proverbes 13.22
8 Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu, Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake.
Proverbes 20.26 Proverbes 25.5 Proverbes 16.12 Psaumes 99.4 1 Samuel 23.3-23.4
9 Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu; Nimetakasika dhambi yangu?
1 Rois 8.46 Ecclésiaste 7.20 Job 14.4 2 Chroniques 6.36 Jacques 3.2
10 Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali, Vyote viwili ni chukizo kwa Bwana.
Proverbes 20.23 Proverbes 11.1 Michée 6.10-6.11 Proverbes 16.11 Lévitique 19.35
11 Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake; Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.
Matthieu 7.16 Proverbes 21.8 Proverbes 22.15 Luc 6.43-6.44 Psaumes 58.3
12 Sikio lisikialo, na jicho lionalo, Bwana ndiye aliyeyafanya yote mawili.
Psaumes 94.9 Exode 4.11 Psaumes 119.18 Actes 26.18 Matthieu 13.13-13.16
13 Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.
Proverbes 19.15 Proverbes 6.9-6.11 Proverbes 12.11 Romains 12.11 Romains 13.11
14 Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi; Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.
Ecclésiaste 1.10 1 Thessaloniciens 4.6 Osée 12.7-12.8
15 Dhahabu iko, na marijani tele; Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.
Proverbes 3.15 Proverbes 15.7 Proverbes 8.11 Proverbes 25.12 Ephésiens 4.29
16 Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni; Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.
Proverbes 27.13 Proverbes 23.27 Exode 22.26-22.27 Proverbes 2.16 Proverbes 22.26-22.27
17 Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu; Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.
Proverbes 9.17-9.18 Ecclésiaste 11.9 Hébreux 11.25 Lamentations 3.15-3.16 Genèse 3.6-3.7
18 Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana; Na kwa shauri la akili fanya vita.
Proverbes 24.6 Proverbes 15.22 Luc 14.31 Proverbes 11.14 Juges 9.29
19 Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.
Proverbes 11.13 Romains 16.18 Proverbes 16.29 Proverbes 24.21 Lévitique 19.16
20 Amlaaniye babaye au mamaye, Taa yake itazimika katika giza kuu.
Proverbes 30.11 Exode 21.17 Matthieu 15.4 Lévitique 20.9 Proverbes 30.17
21 Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka, Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.
Proverbes 13.22 Proverbes 28.22 Proverbes 23.4 Proverbes 28.8 Proverbes 28.20
22 Usiseme, Mimi nitalipa mabaya; Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
1 Thessaloniciens 5.15 Romains 12.17-12.19 Proverbes 24.29 1 Pierre 3.9 Proverbes 17.13
23 Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa Bwana; Tena mizani ya hila si njema.
Proverbes 20.10 Osée 12.7 Proverbes 11.1 Amos 8.5 Ezéchiel 45.10
24 Mwenendo wa mtu watoka kwa Bwana; Basi, awezaje mtu kuelewa na njia yake?
Proverbes 16.9 Jérémie 10.23 Psaumes 25.4 Psaumes 25.12 Proverbes 14.8
25 Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu; Na baada ya kuweka nadhiri kuuliza-uliza habari.
Matthieu 5.33 Ecclésiaste 5.4-5.6 Malachie 3.8-3.10 Lévitique 27.30-27.31 Lévitique 22.10-22.15
26 Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki; Naye hulipitisha gurudumo la kupuria juu yao.
Proverbes 20.8 Psaumes 101.5-101.8 Esaïe 28.27-28.28 2 Samuel 4.9-4.12 2 Samuel 12.31
27 Pumzi ya mwanadamu ni taa ya Bwana; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.
1 Corinthiens 2.11 Proverbes 20.30 Hébreux 4.12-4.13 2 Corinthiens 4.2-4.6 Job 32.8
28 Fadhili na uaminifu humhifadhi mfalme, Na kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa fadhili.
Proverbes 29.14 Proverbes 16.12 Proverbes 16.6 Psaumes 21.7 Esaïe 16.5
29 Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.
Proverbes 16.31 Lévitique 19.32 Jérémie 9.23-9.24 1 Jean 2.14
30 Machubuko ya fimbo husafisha uovu, Na mapigo hufikilia ndani ya mtima.
Proverbes 22.15 Proverbes 19.25 Hébreux 12.10 Esaïe 53.5 Esaïe 27.9

Cette Bible est dans le domaine public.