Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 19.7
Bible en Swahili de l’est


1 Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.
Proverbes 28.6 Proverbes 15.16 Jacques 2.5-2.6 Proverbes 12.26 Proverbes 14.2
2 Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa; Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.
Proverbes 21.5 Proverbes 29.20 Esaïe 28.16 Esaïe 27.11 Proverbes 25.8
3 Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake; Na moyo wake hununa juu ya Bwana.
Psaumes 37.7 Genèse 4.5-4.14 1 Samuel 22.13-22.23 1 Samuel 15.23 Proverbes 11.3
4 Utajiri huongeza rafiki wengi; Bali maskini hutengwa na rafiki yake.
Proverbes 14.20 Luc 15.13-15.15 Proverbes 19.6-19.7 Proverbes 10.15 Job 6.15-6.23
5 Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Wala asemaye uongo hataokoka.
Exode 23.1 Proverbes 21.28 Proverbes 6.19 Daniel 6.24 Proverbes 19.9
6 Watu wengi watamsihi mkuu ili awafadhili; Na kila mtu ni rafiki yake atoaye tunu.
Proverbes 18.16 Proverbes 17.8 Proverbes 29.26 Proverbes 21.14 Proverbes 16.15
7 Ndugu zote wa maskini humchukia; Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye! Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka.
Psaumes 38.11 Proverbes 19.4 Proverbes 18.23 1 Jean 3.17-3.18 Jacques 2.6
8 Apataye hekima hujipenda nafsi yake; Ashikaye ufahamu atapata mema.
Proverbes 16.20 Proverbes 4.4 Psaumes 19.11 Proverbes 17.16 Ezéchiel 36.26
9 Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Naye asemaye uongo ataangamia.
Proverbes 19.5 Jérémie 29.31-29.32 Esaïe 9.15-9.17 Apocalypse 21.8 2 Thessaloniciens 2.8-2.10
10 Maisha ya anasa hayampasi mpumbavu; Sembuse mtumwa awatawale wakuu.
Proverbes 30.21-30.22 Proverbes 26.1 Esaïe 3.5 2 Samuel 3.24-3.25 Osée 9.1
11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.
Proverbes 16.32 Proverbes 14.29 Jacques 1.19 Colossiens 3.12-3.13 Proverbes 15.18
12 Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; Bali hisani yake kama umande juu ya majani.
Osée 14.5 Proverbes 16.14-16.15 Proverbes 20.2 Proverbes 28.15 Psaumes 133.3
13 Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.
Proverbes 27.15 Proverbes 21.9 Proverbes 10.1 Job 14.19 Proverbes 21.19
14 Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.
Proverbes 18.22 Proverbes 31.10-31.31 2 Corinthiens 12.14 Jacques 1.17 Deutéronome 21.16
15 Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.
Proverbes 23.21 Proverbes 20.13 Proverbes 6.9-6.10 Proverbes 24.33 2 Thessaloniciens 3.10
16 Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake; Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakufa.
Luc 10.28 Proverbes 16.17 Proverbes 13.13 Luc 11.28 1 Corinthiens 7.19
17 Amhurumiaye maskini humkopesha Bwana; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.
Proverbes 28.27 2 Corinthiens 9.6-9.8 Matthieu 25.40 Hébreux 6.10 Ecclésiaste 11.1
18 Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini; Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake.
Proverbes 13.24 Proverbes 29.15 Proverbes 29.17 Proverbes 22.15 Proverbes 23.13-23.14
19 Mtu wa hasira nyingi atachukua adhabu yake, Maana ujapomwokoa huna budi kufanya tena.
Proverbes 22.24-22.25 1 Samuel 20.30-20.31 Proverbes 25.28 Proverbes 29.22 1 Samuel 24.17-24.22
20 Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.
Proverbes 12.15 Psaumes 90.14 Deutéronome 32.29 Proverbes 4.1 Deutéronome 8.16
21 Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.
Proverbes 16.1 Proverbes 16.9 Esaïe 14.24 Psaumes 33.10-33.11 Esaïe 14.26-14.27
22 Haja ya mwanadamu ni hisani yake; Ni afadhali maskini kuliko mwongo.
Marc 14.6-14.8 2 Corinthiens 8.12 2 Corinthiens 8.2-8.3 Tite 1.2 Psaumes 62.9
23 Kumcha Bwana huelekea uhai; Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya.
Matthieu 5.6 Hébreux 13.5-13.6 1 Timothée 4.8 Psaumes 90.14 Proverbes 10.27
24 Mtu mvivu hutia mkono wake sahanini; Ila hataki hata kuupeleka kinywani pake.
Proverbes 15.19 Proverbes 19.15 Proverbes 6.9-6.10 Proverbes 26.13-26.16 Proverbes 12.27
25 Mpige mwenye mzaha, na mjinga atapata busara; Mwonye mwenye ufahamu, naye atatambua maarifa.
Proverbes 21.11 Deutéronome 13.11 Proverbes 17.10 Proverbes 15.5 Apocalypse 3.19
26 Apotezaye mali za babaye na kumfukuza mamaye, Ni mwana aaibishaye, na kuleta lawama.
Proverbes 17.2 Proverbes 30.17 Proverbes 10.5 Luc 15.30 Proverbes 30.11
27 Mwanangu, acha kusikia mafundisho, Ukitaka tu kuyaasi maneno ya maarifa.
Jean 10.5 Marc 7.6-7.14 Marc 4.24 2 Pierre 2.1-2.2 1 Rois 22.22-22.28
28 Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki hukumu, Na vinywa vya wasio haki humeza uovu.
Job 15.16 Job 34.7 Job 20.12-20.13 Osée 4.8 Psaumes 10.11
29 Hukumu zimewekwa tayari kwa wenye mzaha; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu.
Proverbes 26.3 Proverbes 10.13 Proverbes 9.12 Esaïe 29.20 2 Pierre 3.3-3.7

Cette Bible est dans le domaine public.