Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 19.12
Bible en Swahili de l’est


1 Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.
Proverbes 28.6 1 Samuel 25.17 Esaïe 59.3 Psaumes 26.11 Matthieu 12.31-12.34
2 Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa; Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.
Proverbes 21.5 Proverbes 29.20 Osée 4.6 Ecclésiaste 7.9 Proverbes 1.16
3 Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake; Na moyo wake hununa juu ya Bwana.
Psaumes 37.7 1 Rois 20.42-20.43 Genèse 3.6-3.12 2 Rois 6.33 Esaïe 8.21-8.22
4 Utajiri huongeza rafiki wengi; Bali maskini hutengwa na rafiki yake.
Proverbes 14.20 Proverbes 19.6-19.7 Luc 15.13-15.15 Job 6.15-6.23 Job 19.13-19.17
5 Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Wala asemaye uongo hataokoka.
Exode 23.1 Proverbes 21.28 Proverbes 6.19 Daniel 6.24 Proverbes 19.9
6 Watu wengi watamsihi mkuu ili awafadhili; Na kila mtu ni rafiki yake atoaye tunu.
Proverbes 17.8 Proverbes 29.26 Proverbes 18.16 Proverbes 21.14 Romains 6.23
7 Ndugu zote wa maskini humchukia; Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye! Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka.
Psaumes 38.11 Proverbes 19.4 Proverbes 18.23 Proverbes 14.20 Psaumes 88.18
8 Apataye hekima hujipenda nafsi yake; Ashikaye ufahamu atapata mema.
Proverbes 16.20 Proverbes 3.18 1 Pierre 3.10 Proverbes 8.35-8.36 Jean 12.25
9 Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Naye asemaye uongo ataangamia.
Proverbes 19.5 1 Timothée 4.1-4.2 Apocalypse 19.20 Apocalypse 22.15 2 Pierre 2.1-2.3
10 Maisha ya anasa hayampasi mpumbavu; Sembuse mtumwa awatawale wakuu.
Proverbes 30.21-30.22 Proverbes 26.1 Jacques 4.9 Esther 3.15 1 Samuel 25.36
11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.
Proverbes 16.32 Proverbes 14.29 Colossiens 3.12-3.13 Proverbes 15.18 Jacques 1.19
12 Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; Bali hisani yake kama umande juu ya majani.
Osée 14.5 Proverbes 16.14-16.15 Proverbes 28.15 Psaumes 133.3 Proverbes 20.2
13 Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.
Proverbes 27.15 Proverbes 21.9 Proverbes 10.1 Proverbes 21.19 Proverbes 25.24
14 Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.
Proverbes 18.22 2 Corinthiens 12.14 Jacques 1.17 Proverbes 31.10-31.31 Proverbes 13.22
15 Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.
Proverbes 20.13 Proverbes 23.21 Proverbes 6.9-6.10 2 Thessaloniciens 3.10 Proverbes 24.33
16 Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake; Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakufa.
Luc 10.28 Proverbes 16.17 Proverbes 13.13 Luc 11.28 1 Jean 3.22
17 Amhurumiaye maskini humkopesha Bwana; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.
Proverbes 28.27 2 Corinthiens 9.6-9.8 Matthieu 25.40 Hébreux 6.10 Ecclésiaste 11.1
18 Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini; Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake.
Proverbes 13.24 Proverbes 29.15 Proverbes 22.15 Proverbes 23.13-23.14 Proverbes 29.17
19 Mtu wa hasira nyingi atachukua adhabu yake, Maana ujapomwokoa huna budi kufanya tena.
1 Samuel 24.17-24.22 1 Samuel 26.21-26.25 2 Samuel 16.5-16.6 1 Samuel 22.7-22.23 Proverbes 22.24-22.25
20 Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.
Proverbes 12.15 Psaumes 37.37 Proverbes 1.8 Proverbes 8.34-8.35 Proverbes 2.1-2.9
21 Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.
Proverbes 16.9 Proverbes 16.1 Esaïe 14.24 Psaumes 33.10-33.11 Esaïe 14.26-14.27
22 Haja ya mwanadamu ni hisani yake; Ni afadhali maskini kuliko mwongo.
Marc 14.6-14.8 Psaumes 62.9 Proverbes 19.1 1 Chroniques 29.17 Marc 12.41-12.44
23 Kumcha Bwana huelekea uhai; Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya.
Matthieu 5.6 Hébreux 13.5-13.6 Proverbes 10.27 Philippiens 4.11-4.12 Proverbes 14.26-14.27
24 Mtu mvivu hutia mkono wake sahanini; Ila hataki hata kuupeleka kinywani pake.
Proverbes 15.19 Proverbes 12.27 Proverbes 24.30-24.34 Marc 14.20 Psaumes 74.11
25 Mpige mwenye mzaha, na mjinga atapata busara; Mwonye mwenye ufahamu, naye atatambua maarifa.
Proverbes 21.11 Deutéronome 13.11 Proverbes 15.5 Apocalypse 3.19 Deutéronome 21.21
26 Apotezaye mali za babaye na kumfukuza mamaye, Ni mwana aaibishaye, na kuleta lawama.
Proverbes 30.17 Proverbes 10.5 Proverbes 17.2 Proverbes 17.25 Proverbes 28.14
27 Mwanangu, acha kusikia mafundisho, Ukitaka tu kuyaasi maneno ya maarifa.
1 Rois 22.22-22.28 Deutéronome 13.1-13.4 Matthieu 7.15 Apocalypse 2.2 1 Jean 4.1
28 Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki hukumu, Na vinywa vya wasio haki humeza uovu.
Job 15.16 Job 34.7 Job 20.12-20.13 Esaïe 28.14-28.18 1 Rois 21.10
29 Hukumu zimewekwa tayari kwa wenye mzaha; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu.
Proverbes 26.3 Proverbes 10.13 Proverbes 9.12 Esaïe 28.22 Proverbes 18.6

Cette Bible est dans le domaine public.