Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 30.6
Bible en Swahili de l’est


L’autel des parfums

1 Nawe fanya madhabahu ya kufukizia uvumba; utaifanyiza kwa mti wa mshita.
Apocalypse 8.3 Exode 37.25-37.28 Exode 40.5 Lévitique 4.7 2 Chroniques 26.16
2 Urefu wake utakuwa dhiraa moja, na upana wake dhiraa moja; itakuwa mraba; na kwenda juu kwake dhiraa mbili; pembe zake zitakuwa za kitu kimoja nayo.
Exode 27.2
3 Nawe utaifunikiza dhahabu safi juu yake, na mbavu zake kando kando, na pembe zake; nawe utaifanyia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
Exode 25.11 Exode 25.24
4 Kisha utaifanyia pete mbili za dhahabu, chini ya ukingo wake katika mbavu zake mbili, katika pande zake mbili utazifanya; nazo zitakuwa mahali pa kuitia miti ya kuichukulia.
Exode 25.27 Exode 25.12 Exode 25.14 Exode 27.4 Exode 27.7
5 Na ile miti utaifanya kwa mti wa mshita, na kuifunikiza dhahabu safi.
Exode 25.27 Exode 25.13
6 Nawe utaitia mbele ya lile pazia lililo karibu na sanduku la ushuhuda mbele ya kiti cha rehema kilicho juu ya ushuhuda, hapo nitakapokutana nawe.
Exode 25.21-25.22 Hébreux 4.16 Lévitique 16.13 Hébreux 9.3-9.5 Exode 30.36
7 Na Haruni atafukiza uvumba wa manukato juu yake; kila siku asubuhi atakapozitengeneza zile taa, ataufukiza.
1 Samuel 2.28 1 Chroniques 23.13 Luc 1.9 Exode 27.20-27.21 Exode 30.34
8 Na Haruni atakapoziwasha zile taa wakati wa jioni, ataufukiza, uwe uvumba wa daima mbele za Bwana katika vizazi vyenu vyote.
Hébreux 9.24 Romains 8.34 1 Thessaloniciens 5.17 Exode 12.6 Hébreux 7.25
9 Hamtafukiza juu yake uvumba mgeni, wala sadaka ya kuteketezwa, wala sadaka ya unga, wala hamtamimina juu yake sadaka ya kinywaji.
Lévitique 10.1
10 Naye Haruni atafanya upatanisho juu ya pembe zake mara moja kila mwaka; kwa damu ya ile sadaka ya dhambi ya kufanya upatanisho, mara moja kila mwaka ataifanyia upatanisho, katika vizazi vyenu vyote; ni takatifu sana kwa Bwana.
Lévitique 16.18 Lévitique 23.27 Hébreux 9.7 Lévitique 16.5-16.6 Hébreux 9.22-9.23

Le rachat des personnes

11 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
12 Utakapowahesabu wana wa Israeli, kama itakavyotokea hesabu yao, ndipo watakapompa Bwana kila mtu ukombozi kwa ajili ya roho yake, hapo utakapowahesabu; ili kwamba yasiwe maradhi kati yao, hapo utakapowahesabu.
Nombres 31.50 Exode 38.25-38.26 Matthieu 20.28 Psaumes 49.7 2 Chroniques 24.6
13 Nacho watakachotoa ni hiki, kila mtu apitaye kwa wale waliohesabiwa atatoa nusu shekeli kwa kuiandama shekeli ya mahali patakatifu; (shekeli ni gera ishirini;) nusu shekeli kwa sadaka ya Bwana.
Lévitique 27.25 Nombres 3.47 Ezéchiel 45.12 Exode 38.26 Matthieu 27.24
14 Kila mtu apitaye kwa wale waliohesabiwa tangu huyo ambaye umri wake ni miaka ishirini, au zaidi, atatoa hiyo sadaka ya Bwana.
Nombres 26.2 Nombres 1.20 Nombres 1.18 Nombres 32.11 Nombres 14.29
15 Matajiri hawataleta zaidi, wala maskini hawataleta kilichopungua, katika hiyo nusu shekeli, watakapotoa hiyo sadaka ya Bwana, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya roho zenu.
Ephésiens 6.9 Proverbes 22.2 Lévitique 17.11 2 Samuel 21.3 Colossiens 3.25
16 Nawe utapokea hizo fedha za upatanisho mikononi mwa hao wana wa Israeli, na kuziweka kwa ajili ya utumishi wa hema ya kukutania; ili kwamba ziwe ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli mbele ya Bwana, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya roho zenu.
Exode 38.25-38.31 Nombres 16.40 Luc 22.19 Néhémie 10.32-10.33 Exode 12.14

La cuve en bronze

17 Bwana akanena na Musa, na kumwambia
18 Fanya na birika la shaba, na tako lake la shaba, ili kuogea; nawe utaliweka kati ya hema ya kukutania na madhabahu, nawe utalitia maji.
Exode 38.8 Exode 40.7 1 Rois 7.38 Exode 40.30-40.32 Zacharie 13.1
19 Na Haruni na wanawe wataosha mikono yao na miguu yao humo;
Esaïe 52.11 Psaumes 26.6 Exode 40.31-40.32 Hébreux 10.22 Jean 13.8-13.10
20 hapo waingiapo ndani ya hema ya kukutania; watajiosha majini, ili wasife; au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike, kumteketezea Bwana sadaka ya moto;
1 Samuel 6.19 Actes 5.5 Exode 12.15 Lévitique 10.1-10.3 Psaumes 89.7
21 basi wataosha mikono yao na miguu yao ili kwamba wasife; na neno hili litakuwa amri kwao milele, kwake yeye na kwa wazao wake katika vizazi vyao vyote.
Exode 28.43 Exode 27.21

L’huile sainte et le parfum

22 Kisha Bwana akasema na Musa, na kumwambia,
23 Jitwalie manukato yaliyo bora, manemane mbichi shekeli mia tano, na mdalasini wenye harufu nzuri nusu ya kiasi hicho, yaani, shekeli mia mbili na hamsini, na kane shekeli mia mbili na hamsini,
Ezéchiel 27.19 Cantique 4.14 Ezéchiel 27.22 Jérémie 6.20 Exode 37.29
24 na kida shekeli mia tano, kwa kuiandama shekeli ya mahali patakatifu, na mafuta ya zeituni kiasi cha vibaba vitano;
Psaumes 45.8 Exode 29.40 Nombres 3.47 Lévitique 19.36 Nombres 15.5
25 nawe utayafanya mafuta ya kutiwa matakatifu, marhamu iliyochanganywa kwa kazi ya ustadi ya mtengezaji manukato; yatakuwa ni mafuta matakatifu ya kutiwa.
Exode 37.29 Psaumes 89.20 Nombres 35.25 Psaumes 133.2 Exode 40.9
26 Nawe utaipaka hema ya kukutania kwa mafuta hayo, na hilo sanduku la ushuhuda,
Nombres 7.1 1 Jean 2.27 Exode 40.9-40.15 Lévitique 8.10-8.12 Nombres 7.10
27 na hiyo meza, na vyombo vyake vyote, na kinara cha taa, na vyombo vyake, na madhabahu ya kufukizia uvumba,
28 na madhabahu ya kuteketezea sadaka, pamoja na vyombo vyake vyote, na birika, na tako lake.
29 Nawe utavitakasa vitu hivyo, ili viwe vitakatifu sana; tena kila kivigusacho vyombo vile kitakuwa kitakatifu.
Exode 29.37 Matthieu 23.17 Lévitique 6.18 Matthieu 23.19
30 Nawe utawatia mafuta Haruni na wanawe, na kuwatakasa, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Lévitique 8.12 Lévitique 8.30 Exode 28.3 Exode 40.15 Exode 29.7-29.37
31 Nawe utanena na wana wa Israeli na kuwaambia, Haya yatakuwa ni mafuta matakatifu ya kutiwa kwa ajili yangu mimi katika vizazi vyenu vyote.
Psaumes 89.20 Lévitique 8.12 Lévitique 21.10 Exode 37.29
32 Hayatamiminwa katika kiwiliwili cha binadamu, wala msifanye mengine mfano wa haya kama yalivyoungwa kwa viungo vyake; ni matakatifu, na kwenu ninyi yatakuwa matakatifu.
Exode 30.25 Matthieu 7.6 Exode 30.37-30.38 Lévitique 21.10
33 Mtu awaye yote atakayechanganya mafuta mfano wa haya, au mtu awaye yote atakayetia mafuta haya juu ya mgeni, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake.
Exode 30.38 Genèse 17.14 Exode 12.15 Lévitique 23.29 Lévitique 17.9
34 Bwana akamwambia Musa, Jitwalie manukato mazuri, yaani, natafi, na shekelethi, na kelbena; viungo vya manukato vizuri pamoja na ubani safi; vitu hivyo vyote na viwe vya kipimo kimoja;
Exode 25.6 Exode 37.29 Lévitique 2.1 1 Chroniques 9.29-9.30 Exode 30.23
35 nawe utafanya uvumba wa vitu hivyo, manukato ya kazi ya ustadi wa mtengenazaji manukato, yatakuwa yamekolea, safi, matakatifu;
Lévitique 2.13 Exode 30.25 Cantique 3.6 Cantique 1.3 Jean 12.3
36 nawe baadhi yake utayaponda sana, na kuyaweka mbele ya ushuhuda ndani ya hema ya kukutania, hapo nitakapokutana nawe; nayo yatakuwa kwenu matakatifu sana.
Exode 25.22 Lévitique 16.2 Exode 16.34 Exode 29.42-29.43 Exode 30.6
37 Na uvumba utakaofanya, hamtajifanyia uvumba wenye viungo sawasawa na uvumba huo; utakuwa kwenu mtakatifu kwa ajili ya Bwana.
Exode 30.32-30.33 Lévitique 2.3 Exode 29.37
38 Mtu ye yote atakayefanya mfano wa huo, ili kuunusa, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake.
Exode 30.33

Cette Bible est dans le domaine public.