Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 16.36
Bible en Swahili de l’est


Les cailles et la manne

1 Kisha wakasafiri kutoka Elimu, na mkutano wote wa wana wa Israeli wakafikilia bara ya Sini, iliyoko kati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili baada ya kutoka kwao nchi ya Misri.
Nombres 33.10-33.12 Exode 15.27 Exode 17.1 Ezéchiel 30.15-30.16
2 Na mkutano mzima wa wana wa Israeli ukawanung’unikia Musa na Haruni, huko barani;
Exode 15.24 1 Corinthiens 10.10 Psaumes 106.25 Psaumes 106.13 Exode 14.11
3 wana wa Israeli wakawaambia, Laiti tungalikufa kwa mkono wa Bwana katika nchi ya Misri, hapo tulipoketi karibu na zile sufuria za nyama, tulipokula vyakula hata kushiba; kwani mmetutoa huko na kututia katika bara hii, ili kutuua kwa njaa kusanyiko hili lote.
Lamentations 4.9 Nombres 11.4-11.5 Exode 17.3 Nombres 20.3-20.5 Nombres 14.2
4 Ndipo Bwana akamwambia Musa, Tazama, mimi nitawanyeshea ninyi mvua ya mkate kutoka mbinguni; na hao watu watatoka nje na kuokota kila siku sehemu ya siku; ili nipate kuwajaribu, kwamba watakwenda katika sheria yangu, ama sivyo.
Exode 15.25 Psaumes 78.24-78.25 Psaumes 105.40 1 Corinthiens 10.3 Deutéronome 8.16
5 Kisha itakuwa siku ya sita, ya kwamba watayaandaa hayo watakayoleta ndani, nayo yatakuwa ni mara mbili kuliko wayaokotayo kila siku.
Lévitique 25.21-25.22 Exode 35.2-35.3 Exode 16.22-16.23
6 Musa na Haruni wakawaambia wana wote wa Israeli, Jioni ndipo mtakapojua ya kuwa Bwana amewaleta kutoka nchi ya Misri;
Exode 6.7 Nombres 16.28 Nombres 16.30 Exode 16.12-16.13 Esaïe 63.11-63.12
7 na asubuhi ndipo mtakapouona utukufu wa Bwana; kwa kuwa yeye asikia manung’uniko yenu mliyomnung’unikia Bwana; na sisi tu nani, hata mkatunung’unikia?
Nombres 16.11 Esaïe 35.2 Esaïe 40.5 Exode 16.10 Exode 40.34
8 Musa akasema, Ndilo litakalokuwa, hapo Bwana atakapowapa nyama wakati wa jioni mle, na asubuhi mikate hata mkakinai; kwa kuwa Bwana asikia manung’uniko yenu mliyomnung’unikia yeye; na sisi tu nani? Manung’uniko yenu hayakuwa juu yetu sisi, ila juu ya Bwana.
Romains 13.2 1 Samuel 8.7 Luc 10.16 Nombres 14.27 1 Thessaloniciens 4.8
9 Musa akamwambia Haruni, Haya, sema na mkutano wote wa wana wa Israeli, Njoni karibu mbele ya Bwana; kwa kuwa yeye ameyasikia manung’uniko yenu.
Nombres 16.16 Exode 16.2 Exode 16.8
10 Ilikuwa Haruni aliponena na huo mkutano wote wa wana wa Israeli, wakaangalia upande wa bara, na tazama, utukufu wa Bwana ukaonekana katika hilo wingu.
Exode 16.7 Nombres 16.19 Nombres 16.42 Exode 40.34-40.38 Lévitique 9.6
11 Bwana akasema na Musa, akinena,
12 Nimeyasikia manung’uniko ya wana wa Israeli; haya sema nao, ukinena, Wakati wa jioni mtakula nyama, na wakati wa asubuhi mtashiba mkate; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Joël 3.17 Exode 6.7 Ezéchiel 39.22 Exode 7.17 Ezéchiel 34.30
13 Ikawa wakati wa jioni, kware wakakaribia, wakakifunikiza kituo; na wakati wa asubuhi umande ulikuwa juu ya nchi pande zote za kituo.
Nombres 11.9 Psaumes 78.27-78.28 Psaumes 105.40 Nombres 11.31-11.33
14 Na ulipoinuka ule umande uliokuwa juu ya nchi, kumbe! Juu ya uso wa bara kitu kidogo kilichoviringana, kidogo kama sakitu juu ya nchi.
Nombres 11.7-11.9 Psaumes 105.40 Psaumes 78.24 Néhémie 9.15 Exode 16.31
15 Wana wa Israeli walipokiona, wakaambiana, Nini hiki? Maana hawakujua ni kitu gani. Musa akawaambia, Ndio mkate ambao Bwana amewapa ninyi, mle.
Exode 16.4 Exode 16.31 Deutéronome 8.3 Jean 6.58 Josué 5.12
16 Neno hili ndilo aliloagiza Bwana, Okoteni ninyi kitu hicho kila mtu kama ulaji wake ulivyo; kichwa pishi,kama hesabu ya watu wenu ilivyo ;ndivyo mtakavyotwaa,kila mtu kwa ajili ya hao walioko hemani mwake.
Exode 16.36 Exode 16.18 Exode 16.32-16.33
17 Wana wa Israeli wakafanya hivyo, wakaokota wengine zaidi, wengine kupungua.
18 Nao walipoipima kwa pishi, yeye aliyekuwa ameokota kingi hakubakiwa na kitu, na yeye aliyekuwa ameokota kichache hakupungukiwa; wakaokota kila mtu kama ulaji wake ulivyokuwa.
2 Corinthiens 8.14-8.15
19 Musa akawaambia, Mtu awaye yote asikisaze hata asubuhi.
Exode 12.10 Exode 23.18 Matthieu 6.34 Exode 16.23
20 Lakini hawakumsikiza Musa; wengine miongoni mwao wakakisaza hata asubuhi, nacho kikaingia mabuu na kutoa uvundo; Musa akawakasirikia sana.
Jacques 5.2-5.3 Marc 10.14 Hébreux 13.5 Matthieu 6.19 Luc 12.15
21 Basi wakaokota asubuhi baada ya asubuhi, kila mtu kama ulaji wake ulivyokuwa; na hapo jua lilipokuwa ni kali, kikayeyuka.
Matthieu 6.33 Ecclésiaste 12.1 Ecclésiaste 9.10 2 Corinthiens 6.2 Proverbes 6.6-6.11
22 Basi ikawa siku ya sita wakaokota kile chakula sehemu maradufu, kila mtu pishi mbili; na wazee wote wa mkutano wakaenda na kumwambia Musa.
Exode 16.5 Lévitique 25.12 Exode 16.16 Exode 34.31 Lévitique 25.22
23 Akawaambia, Ndilo neno alilonena Bwana Kesho ni starehe takatifu, Sabato takatifu kwa Bwana; okeni mtakachooka, na kutokosa mtakachotokosa; na hicho kitakachowasalia jiwekeeni kilindwe hata asubuhi.
Lévitique 23.3 Exode 31.15 Exode 20.8-20.11 Apocalypse 1.10 Luc 23.56
24 Basi wakakiweka hata asubuhi, kama Musa alivyowaagiza; nacho hakikutoa uvundo wala kuingia mabuu.
Exode 16.20 Exode 16.33
25 Musa akasema, Haya, kuleni hiki leo; kwa kuwa leo ni Sabato ya Bwana; leo hamtakiona nje barani.
Exode 16.23 Néhémie 9.14 Exode 16.29
26 Siku sita mtaokota; lakini siku ya saba ni Sabato, siku hiyo hakitapatikana.
Ezéchiel 46.1 Deutéronome 5.13 Exode 20.9-20.11 Luc 13.14
27 Ikawa siku ya saba wengine wakatoka kwenda kukiokota, wasikione.
Proverbes 20.4
28 Bwana akamwambia Musa, Mtakataa kuyashika maagizo yangu na sheria zangu hata lini?
Psaumes 78.10 Psaumes 106.13 2 Rois 17.14 Ezéchiel 20.13 Jérémie 4.14
29 Angalieni, kwa kuwa Bwana amewapa ninyi hiyo Sabato, kwa sababu hii huwapa siku ya sita chakula cha siku mbili; kaeni kila mtu mahali pake, mtu awaye yote asiondoke mahali pake kwa siku ya saba.
Esaïe 58.13-58.14 Exode 31.13 Luc 23.56 Néhémie 9.14 Ezéchiel 20.12
30 Basi hao watu wakapumzika kwa siku ya saba.
Lévitique 23.3 Deutéronome 5.12-5.14 Hébreux 4.9
31 Na nyumba ya Israeli wakakiita jina lake Mana; nacho kilikuwa mfano wa chembe za mtama, nyeupe; na tamu yake ilikuwa kama tamu ya maandazi membamba yaliyoandaliwa kwa asali.
Exode 16.15 Nombres 11.6-11.9 Cantique 2.3
32 Musa akasema, Hili ni neno Bwana aliloliamuru, Pishi moja ya kitu hicho na kiwekwe kwa ajili ya vizazi vyenu; ili kwamba wao wapate kukiona kile chakula nilichowalisha ninyi barani, hapo nilipowaleta kutoka nchi ya Misri.
Hébreux 2.1 Psaumes 105.5 Psaumes 111.4-111.5 Psaumes 103.1-103.2 Luc 22.19
33 Basi Musa akamwambia Haruni, Twaa kopo, ukatie pishi moja ya hiyo Mana ndani yake, uiweke mbele ya Bwana, ilindwe kwa ajili ya vizazi vyenu.
Hébreux 9.4
34 Kama vile Bwana alivyomwagizia Musa ndivyo Haruni alivyoiweka hapo mbele ya Ushahidi, ili ilindwe.
Exode 25.21 Exode 25.16 Nombres 17.10 Exode 40.20 Exode 27.21
35 Na wana wa Israeli walikula Mana muda wa miaka arobaini, hata walipofikilia nchi iliyo na watu, wakala ile Mana, hata walipofikilia mipakani mwa nchi ya Kanaani.
Néhémie 9.20-9.21 Josué 5.12 Deutéronome 8.2-8.3 Néhémie 9.15 Psaumes 78.24-78.25
36 Hiyo omeri ni sehemu kumi ya efa.
Exode 16.16 Exode 16.32-16.33

Cette Bible est dans le domaine public.