Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 15.12
Bible en Swahili de l’est


Cantique de Moïse et d’Israël

1 Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia Bwana wimbo huu wakanena, na kusema, Nitamwimbia Bwana, kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.
Apocalypse 15.3 Psaumes 106.12 Exode 15.21 Esaïe 51.10-51.11 Juges 5.1-5.31
2 Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.
Esaïe 12.2 Esaïe 25.1 Psaumes 59.17 Psaumes 118.14 Psaumes 18.46
3 Bwana ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lake.
Psaumes 24.8 Psaumes 83.18 Apocalypse 19.11-19.21 Exode 3.15 Esaïe 42.8
4 Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini, Maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.
Exode 14.13-14.28 Exode 14.6-14.7
5 Vilindi vimewafunikiza, Walizama vilindini kama jiwe.
Néhémie 9.11 Exode 15.10 Exode 14.28 Jonas 2.2 Ezéchiel 27.34
6 Bwana, mkono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo, Bwana, mkono wako wa kuume wawaseta-seta adui.
Psaumes 118.15-118.16 Esaïe 51.9 Psaumes 60.5 Psaumes 2.9 Apocalypse 2.27
7 Kwa wingi wa ukuu wako wawaangusha chini wanaokuondokea, Wapeleka hasira yako, nayo huwateketeza kama mabua makavu.
Esaïe 5.24 Deutéronome 33.26 Malachie 4.1 Esaïe 47.14 Esaïe 37.36
8 Kwa upepo wa mianzi ya pua yako maji yalipandishwa, Mawimbi yakasimama juu wima mfano wa chungu, Vilindi vikagandamana ndani ya moyo wa bahari.
Psaumes 78.13 Exode 14.21-14.22 Job 4.9 Habakuk 3.10 Esaïe 11.4
9 Adui akasema, Nitafuatia, nitapata, nitagawanya nyara, Nafsi yangu itashibishwa na wao; Nitaufuta upanga wangu, mkono wangu utawaangamiza.
Juges 5.30 Esaïe 53.12 Exode 14.5 Luc 11.22 Genèse 49.27
10 Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza; Wakazama kama risasi ndani ya maji makuu.
Esaïe 11.15 Exode 14.21 Exode 15.5 Psaumes 147.18 Psaumes 135.7
11 Ee Bwana, katika miungu ni nani aliye kama wewe? Ni nani aliye kama wewe, mtukufu katika utakatifu, Mwenye kuogopwa katika sifa zako, mfanya maajabu?
Apocalypse 4.8 Esaïe 6.3 1 Samuel 2.2 Psaumes 86.8 1 Rois 8.23
12 Ulinyosha mkono wako wa kuume, Nchi ikawameza.
Exode 15.6
13 Wewe kwa rehema zako umewaongoza watu uliowakomboa, Kwa uweza wako uliwaelekeza hata makao yako matakatifu.
Psaumes 77.20 Jérémie 2.6 Psaumes 80.1 Néhémie 9.12 Psaumes 106.9
14 Kabila za watu wamesikia, wanatetemeka, Wakaao Ufilisti utungu umewashika.
Josué 9.24 Josué 2.9-2.10 Nombres 14.14 Deutéronome 2.25 Psaumes 48.6
15 Ndipo majumbe wa Edomu wakashangaa, Watu wa Moabu wenye nguvu tetemeko limewapata, Watu wote wakaao Kanaani wameyeyuka.
Josué 5.1 Josué 2.9 Josué 2.11 Genèse 36.40 Deutéronome 2.4
16 Hofu na woga umewaangukia; Kwa uweza wa mkono wako wanakaa kimya kama jiwe; Hata watakapovuka watu wako, Ee Bwana, Hata watakapovuka watu wako uliowanunua.
Psaumes 74.2 Josué 2.9 1 Samuel 25.37 Deutéronome 2.25 Jérémie 31.11
17 Utawaingiza, na kuwapanda katika mlima wa urithi wako, Mahali pale ulipojifanyia, Ee Bwana, ili upakae, Pale patakatifu ulipopaweka imara, Bwana, kwa mikono yako.
Psaumes 44.2 Psaumes 80.8 Psaumes 78.68-78.69 Jérémie 32.41 Psaumes 132.13-132.14
18 Bwana atatawala milele na milele.
Psaumes 10.16 Psaumes 29.10 Psaumes 146.10 Esaïe 57.15 Daniel 4.3
19 Kwa maana farasi za Farao na magari yake na wapanda farasi wake waliingia ndani ya bahari, Bwana akayarudisha maji ya bahari juu yao; bali wana wa Israeli walikwenda katika nchi kavu katikati ya bahari.
Exode 14.28-14.29 Hébreux 11.29 Exode 14.22-14.23 Proverbes 21.31
20 Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza.
Juges 11.34 1 Samuel 18.6 Nombres 26.59 Psaumes 150.4 Psaumes 68.25
21 Miriamu akawaitikia,Mwimbieni Bwana ,kwa maana ametukuka sana;Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.
Exode 15.1 Psaumes 134.1-134.3 Apocalypse 5.9 Apocalypse 7.10-7.12 2 Chroniques 5.13

Premières étapes dans le désert

L’eau de Mara

22 Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.
Genèse 16.7 Genèse 25.18 1 Samuel 15.7 Exode 3.18
23 Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.
Nombres 33.8 Ruth 1.20
24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?
Exode 16.2 Exode 14.11 Jude 1.16 Exode 17.3-17.4 Philippiens 2.14
25 Naye akamlilia Bwana; Bwana akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, akawaonja huko;
Deutéronome 8.2 Juges 3.4 Exode 14.10 Psaumes 66.10 Deutéronome 8.16
26 akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi Bwana nikuponyaye.
Deutéronome 7.15 Psaumes 103.3 Psaumes 147.3 Exode 23.25 Deutéronome 28.60
27 Wakafikilia Elimu, palipokuwa na chemchemi kumi na mbili, na mitende sabini; wakapanga hapo, karibu na maji.
Nombres 33.9 Ezéchiel 47.12 Apocalypse 22.2 Apocalypse 7.17 Esaïe 12.3

Cette Bible est dans le domaine public.