Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 91.7
Bible en Swahili de l’est


La protection pleinement suffisante de Dieu

1 Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.
Psaumes 32.7 Psaumes 36.7 Psaumes 17.8 Psaumes 31.20 Esaïe 32.2
2 Nitasema, Bwana ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini.
Psaumes 18.2 Psaumes 142.5 Esaïe 12.2 Esaïe 26.3-26.4 Psaumes 48.14
3 Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo.
Psaumes 124.7 Psaumes 141.9 Psaumes 91.6 Job 5.10-5.22 Ecclésiaste 9.12
4 Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao.
Psaumes 17.8 Psaumes 57.1 Deutéronome 32.11 Psaumes 35.2 Genèse 15.1
5 Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,
Esaïe 43.2 Job 5.19-5.27 Hébreux 13.6 Psaumes 3.5-3.6 Proverbes 28.1
6 Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri,
Exode 12.29-12.30 Psaumes 121.5-121.6 Matthieu 24.6-24.7 Nombres 16.48 2 Rois 19.35
7 Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! Hata hivyo hautakukaribia wewe.
Josué 14.10 Nombres 14.37-14.38 Genèse 7.23 Exode 12.12-12.13 Psaumes 32.6
8 Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki.
Psaumes 37.34 Proverbes 3.25-3.26 Psaumes 58.10-58.11 Psaumes 92.11 Malachie 1.5
9 Kwa kuwa Wewe Bwana ndiwe kimbilio langu; Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.
Psaumes 71.3 Psaumes 90.1 Psaumes 142.4-142.5 Psaumes 146.5-146.6 Psaumes 91.1-91.2
10 Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.
Proverbes 12.21 Deutéronome 7.15 Romains 8.25 Psaumes 121.7 Job 5.24
11 Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.
Psaumes 34.7 Luc 4.10-4.11 Hébreux 1.14 Proverbes 3.6 Psaumes 71.3
12 Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
Esaïe 63.9 Proverbes 3.23 Psaumes 37.24 Matthieu 4.6 Job 5.23
13 Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.
Luc 10.19 Daniel 6.22 Marc 16.18 Romains 3.13 1 Samuel 17.37
14 Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.
Jean 14.23 Psaumes 9.10 Jean 16.27 Jacques 1.12 Romains 8.28
15 Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;
1 Samuel 2.30 2 Corinthiens 1.9-1.10 Psaumes 10.17 Psaumes 50.15 Jérémie 33.3
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu.
Psaumes 21.4 Psaumes 50.23 Proverbes 3.2 Proverbes 3.16 Deutéronome 6.2

Cette Bible est dans le domaine public.