Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 7.4
Bible en Swahili de l’est


Prière du juste persécuté

1 Bwana, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe, Uniokoe na wote wanaonifuatia, uniponye.
Psaumes 31.15 Habakuk 3.1 Psaumes 18.28 Josué 14.8 Psaumes 146.3-146.6
2 Asije akaipapura nafsi yangu kama simba, Akiivunja-vunja pasipokuwa na wa kuponya.
Psaumes 50.22 Esaïe 38.13 2 Timothée 4.17 Psaumes 10.9 1 Pierre 5.8
3 Bwana, Mungu wangu, ikiwa nimetenda haya, Ikiwa mna uovu mikononi mwangu,
1 Samuel 24.11 2 Samuel 16.7-16.8 Psaumes 59.3 Job 16.17-16.19 1 Samuel 22.8
4 Ikiwa nimemlipa mabaya Yeye aliyekaa kwangu salama; (Hasha! Nimemponya yeye Aliyekuwa mtesi wangu bila sababu;)
1 Samuel 24.7 Psaumes 109.5 Psaumes 55.20 Jérémie 18.20-18.21 1 Samuel 26.9-26.17
5 Basi adui na anifuatie, Na kuikamata nafsi yangu; Naam, aukanyage uzima wangu, Na kuulaza utukufu wangu mavumbini.
Psaumes 44.5 Job 31.38-31.40 Malachie 4.3 Jérémie 17.13 Esaïe 63.3
6 Bwana uondoke kwa hasira yako; Ujiinue juu ya jeuri ya watesi wangu; Uamke kwa ajili yangu; Umeamuru hukumu.
Psaumes 44.23 Psaumes 3.7 Psaumes 35.23 Esaïe 33.10 Psaumes 68.1-68.2
7 Kusanyiko la mataifa na likuzunguke, Na juu yake uketi utawale.
Apocalypse 16.5-16.7 Psaumes 113.5-113.6 Apocalypse 19.2 Apocalypse 18.20 Psaumes 58.10-58.11
8 Bwana atawaamua mataifa, Bwana, unihukumu mimi, Kwa kadiri ya haki yangu, Sawasawa na unyofu nilio nao.
Psaumes 96.13 Romains 14.10-14.12 Psaumes 98.9 1 Thessaloniciens 2.10 1 Corinthiens 4.4-4.5
9 Ubaya wao wasio haki na ukome, Lakini umthibitishe mwenye haki. Kwa maana mjaribu mioyo na viuno Ndiye Mungu aliye mwenye haki.
Jérémie 11.20 Apocalypse 2.23 1 Chroniques 28.9 Psaumes 37.23 1 Samuel 16.7
10 Ngao yangu ina Mungu, Awaokoaye wanyofu wa moyo.
Psaumes 125.4 Proverbes 2.21 Psaumes 84.11 Proverbes 28.18 Proverbes 11.20
11 Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Naam, Mungu aghadhibikaye kila siku.
Nahum 1.6 Nahum 1.2 Psaumes 94.15 Psaumes 50.6 Psaumes 7.8
12 Mtu asiporejea ataunoa upanga wake; Ameupinda uta wake na kuuweka tayari;
Deutéronome 32.41 Esaïe 34.5 Esaïe 55.6-55.7 Ezéchiel 33.11 Psaumes 85.4
13 Naye amemtengenezea silaha za kufisha, Akifanya mishale yake kuwa ya moto.
Psaumes 45.5 Apocalypse 16.6 2 Thessaloniciens 1.6 Psaumes 64.3 Deutéronome 32.23
14 Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.
Jacques 1.15 Job 15.35 Esaïe 33.11 Job 15.20 Esaïe 59.4-59.5
15 Amechimba shimo, amelichimba chini sana, Akatumbukia katika handaki aliyoifanya!
Job 4.8 Psaumes 35.7-35.8 Psaumes 119.85 Psaumes 141.10 Proverbes 26.27
16 Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.
Esther 9.25 1 Rois 2.32 Malachie 2.3-2.5 1 Samuel 23.9 1 Samuel 28.19
17 Nitamshukuru Bwana kwa kadiri ya haki yake; Nitaliimbia jina la Bwana aliye juu.
Psaumes 9.2 Psaumes 71.15-71.16 Actes 7.48 Psaumes 35.28 Psaumes 145.7

Cette Bible est dans le domaine public.