Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 7.16
Bible en Swahili de l’est


Prière du juste persécuté

1 Bwana, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe, Uniokoe na wote wanaonifuatia, uniponye.
Psaumes 31.15 Habakuk 3.1 Psaumes 43.4 1 Pierre 1.21 Psaumes 30.12-31.1
2 Asije akaipapura nafsi yangu kama simba, Akiivunja-vunja pasipokuwa na wa kuponya.
Esaïe 38.13 Psaumes 50.22 Psaumes 17.12 Job 10.7 Osée 13.7-13.8
3 Bwana, Mungu wangu, ikiwa nimetenda haya, Ikiwa mna uovu mikononi mwangu,
1 Samuel 24.11 Psaumes 59.3 2 Samuel 16.7-16.8 Psaumes 66.18 1 Samuel 20.8
4 Ikiwa nimemlipa mabaya Yeye aliyekaa kwangu salama; (Hasha! Nimemponya yeye Aliyekuwa mtesi wangu bila sababu;)
1 Samuel 24.7 Psaumes 109.5 Psaumes 55.20 Genèse 44.4 1 Samuel 22.14
5 Basi adui na anifuatie, Na kuikamata nafsi yangu; Naam, aukanyage uzima wangu, Na kuulaza utukufu wangu mavumbini.
Psaumes 60.12 Job 31.5-31.10 Job 40.12-40.13 Job 16.15 Psaumes 49.12
6 Bwana uondoke kwa hasira yako; Ujiinue juu ya jeuri ya watesi wangu; Uamke kwa ajili yangu; Umeamuru hukumu.
Psaumes 44.23 Psaumes 35.23 Psaumes 3.7 Esaïe 33.10 Psaumes 76.8-76.9
7 Kusanyiko la mataifa na likuzunguke, Na juu yake uketi utawale.
Psaumes 138.6 Psaumes 48.11 Psaumes 93.4 Esaïe 57.15 Apocalypse 11.17-11.18
8 Bwana atawaamua mataifa, Bwana, unihukumu mimi, Kwa kadiri ya haki yangu, Sawasawa na unyofu nilio nao.
Romains 14.10-14.12 Psaumes 96.13 Psaumes 98.9 2 Corinthiens 1.12 Psaumes 43.1
9 Ubaya wao wasio haki na ukome, Lakini umthibitishe mwenye haki. Kwa maana mjaribu mioyo na viuno Ndiye Mungu aliye mwenye haki.
Apocalypse 2.23 Jérémie 11.20 Psaumes 37.23 1 Chroniques 28.9 Jérémie 20.12
10 Ngao yangu ina Mungu, Awaokoaye wanyofu wa moyo.
Psaumes 125.4 Genèse 15.1 Psaumes 112.2 Job 8.6 Psaumes 89.18
11 Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Naam, Mungu aghadhibikaye kila siku.
Psaumes 94.15 Nahum 1.6 Nahum 1.2 Psaumes 50.6 Psaumes 7.8
12 Mtu asiporejea ataunoa upanga wake; Ameupinda uta wake na kuuweka tayari;
Deutéronome 32.41 Actes 3.19 Ezéchiel 21.23 Matthieu 3.10 Ezéchiel 18.30
13 Naye amemtengenezea silaha za kufisha, Akifanya mishale yake kuwa ya moto.
Psaumes 45.5 Lamentations 3.12-3.13 Psaumes 11.2 Deutéronome 32.42 Habakuk 3.11
14 Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.
Jacques 1.15 Job 15.35 Esaïe 33.11 Job 15.20 Esaïe 59.4-59.5
15 Amechimba shimo, amelichimba chini sana, Akatumbukia katika handaki aliyoifanya!
Job 4.8 Psaumes 119.85 Psaumes 141.10 Proverbes 26.27 Psaumes 35.7-35.8
16 Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.
Esther 9.25 1 Rois 2.32 Psaumes 36.4 Psaumes 36.12 1 Samuel 26.10
17 Nitamshukuru Bwana kwa kadiri ya haki yake; Nitaliimbia jina la Bwana aliye juu.
Psaumes 9.2 Psaumes 71.15-71.16 Daniel 4.25 Daniel 4.34 Psaumes 98.2

Cette Bible est dans le domaine public.