Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 7.14
Bible en Swahili de l’est


Prière du juste persécuté

1 Bwana, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe, Uniokoe na wote wanaonifuatia, uniponye.
Psaumes 31.15 Habakuk 3.1 Psaumes 146.3-146.6 Daniel 9.4 Psaumes 11.1
2 Asije akaipapura nafsi yangu kama simba, Akiivunja-vunja pasipokuwa na wa kuponya.
Psaumes 50.22 Esaïe 38.13 Psaumes 10.9 1 Pierre 5.8 Psaumes 22.13
3 Bwana, Mungu wangu, ikiwa nimetenda haya, Ikiwa mna uovu mikononi mwangu,
1 Samuel 24.11 2 Samuel 16.7-16.8 Psaumes 59.3 1 Samuel 22.8 1 Samuel 26.18-26.19
4 Ikiwa nimemlipa mabaya Yeye aliyekaa kwangu salama; (Hasha! Nimemponya yeye Aliyekuwa mtesi wangu bila sababu;)
1 Samuel 24.7 Psaumes 109.5 Psaumes 55.20 1 Samuel 26.9-26.17 1 Samuel 26.21
5 Basi adui na anifuatie, Na kuikamata nafsi yangu; Naam, aukanyage uzima wangu, Na kuulaza utukufu wangu mavumbini.
Job 31.38-31.40 Malachie 4.3 Jérémie 17.13 Esaïe 63.3 Psaumes 60.12
6 Bwana uondoke kwa hasira yako; Ujiinue juu ya jeuri ya watesi wangu; Uamke kwa ajili yangu; Umeamuru hukumu.
Psaumes 44.23 Psaumes 3.7 Psaumes 35.23 Esaïe 33.10 Psaumes 59.5
7 Kusanyiko la mataifa na likuzunguke, Na juu yake uketi utawale.
Psaumes 113.5-113.6 Apocalypse 19.2 Apocalypse 18.20 Psaumes 58.10-58.11 Psaumes 138.6
8 Bwana atawaamua mataifa, Bwana, unihukumu mimi, Kwa kadiri ya haki yangu, Sawasawa na unyofu nilio nao.
Psaumes 96.13 Romains 14.10-14.12 Psaumes 98.9 1 Corinthiens 4.4-4.5 2 Corinthiens 1.12
9 Ubaya wao wasio haki na ukome, Lakini umthibitishe mwenye haki. Kwa maana mjaribu mioyo na viuno Ndiye Mungu aliye mwenye haki.
Apocalypse 2.23 Jérémie 11.20 1 Chroniques 28.9 Psaumes 37.23 1 Samuel 16.7
10 Ngao yangu ina Mungu, Awaokoaye wanyofu wa moyo.
Psaumes 125.4 Psaumes 84.11 Proverbes 28.18 Proverbes 11.20 Psaumes 18.1-18.2
11 Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Naam, Mungu aghadhibikaye kila siku.
Nahum 1.6 Nahum 1.2 Psaumes 94.15 Psaumes 7.8 Psaumes 50.6
12 Mtu asiporejea ataunoa upanga wake; Ameupinda uta wake na kuuweka tayari;
Deutéronome 32.41 Esaïe 55.6-55.7 Ezéchiel 33.11 Psaumes 85.4 Actes 3.19
13 Naye amemtengenezea silaha za kufisha, Akifanya mishale yake kuwa ya moto.
Psaumes 45.5 2 Thessaloniciens 1.6 Psaumes 64.3 Deutéronome 32.23 Lamentations 3.12-3.13
14 Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.
Job 15.35 Jacques 1.15 Esaïe 33.11 Job 15.20 Esaïe 59.4-59.5
15 Amechimba shimo, amelichimba chini sana, Akatumbukia katika handaki aliyoifanya!
Job 4.8 Psaumes 35.7-35.8 Psaumes 119.85 Psaumes 141.10 Proverbes 26.27
16 Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.
Esther 9.25 1 Rois 2.32 1 Samuel 23.9 1 Samuel 28.19 Psaumes 37.12-37.13
17 Nitamshukuru Bwana kwa kadiri ya haki yake; Nitaliimbia jina la Bwana aliye juu.
Psaumes 9.2 Psaumes 71.15-71.16 Psaumes 35.28 Psaumes 145.7 Daniel 4.17

Cette Bible est dans le domaine public.