Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 6
Bible en Swahili de l’est


Appel à la bonté de Dieu

1 Bwana, usinikemee kwa hasira yako, Wala usinirudi kwa ghadhabu yako.
Psaumes 38.1 1 Chroniques 15.21 Jérémie 46.28 Psaumes 4.1 Psaumes 118.18
2 Bwana, unifadhili, maana ninanyauka; Bwana, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.
Osée 6.1 Nombres 12.13 Psaumes 31.10 Psaumes 30.2 Deutéronome 32.39
3 Na nafsi yangu imefadhaika sana; Na Wewe, Bwana, hata lini?
Psaumes 90.13 Jean 12.27 Proverbes 18.14 Psaumes 31.9-31.10 Psaumes 38.8
4 Bwana urudi, uniopoe nafsi yangu, Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.
Psaumes 17.13 Psaumes 22.20 Psaumes 116.4 Psaumes 80.14 Psaumes 90.13
5 Maana mautini hapana kumbukumbu lako; Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?
Psaumes 115.17 Ecclésiaste 9.10 Psaumes 88.10-88.12 Psaumes 30.9 Jean 9.4
6 Nimechoka kwa kuugua kwangu; Kila usiku nakieleza kitanda changu; Nalilowesha godoro langu kwa machozi yangu.
Psaumes 69.3 Psaumes 42.3 Psaumes 38.9 Job 7.3 Psaumes 39.12
7 Jicho langu limeharibika kwa masumbufu, Na kuchakaa kwa sababu yao wanaoniudhi.
Psaumes 38.10 Job 17.7 Psaumes 88.9 Lamentations 5.17 Psaumes 32.3
8 Ondokeni kwangu, ninyi nyote mtendao uovu; Kwa kuwa Bwana ameisikia sauti ya kilio changu.
Psaumes 119.115 Luc 13.27 Psaumes 3.4 Matthieu 7.23 Psaumes 139.19
9 Bwana ameisikia dua yangu; Bwana atayatakabali maombi yangu.
Psaumes 66.19-66.20 Psaumes 116.1-116.2 Psaumes 138.3 Psaumes 31.22 Psaumes 120.1
10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, Watarudi nyuma, kwa ghafula wataaibika.
Malachie 3.18 Jérémie 20.11 Psaumes 86.17 Psaumes 132.18 Psaumes 35.26

Cette Bible est dans le domaine public.