1 Ee Mungu, uisikilize sala yangu, Wala usijifiche nikuombapo rehema.
Psaumes 61.1  Psaumes 17.1  Psaumes 54.1-54.2  Psaumes 86.6  Lamentations 3.8  
 2 Unisikilize na kunijibu, Nimetanga-tanga nikilalama na kuugua.
Esaïe 38.14  Esaïe 59.11  Psaumes 38.6  Psaumes 102.9-102.10  Psaumes 43.2  
 3 Kwa sababu ya sauti ya adui, Kwa sababu ya dhuluma yake yule mwovu. Kwa maana wananitupia uovu, Na kwa ghadhabu wananiudhi.
2 Samuel 16.7-16.8  Psaumes 12.5  Matthieu 26.59  Psaumes 35.11  Psaumes 54.3  
 4 Moyo wangu unaumia ndani yangu, Na hofu za mauti zimeniangukia.
Psaumes 116.3  Psaumes 18.4-18.5  Jean 12.27  Psaumes 102.3-102.5  2 Corinthiens 1.8-1.10  
 5 Hofu na tetemeko limenijia, Na hofu kubwa imenifunikiza.
Psaumes 119.120  Job 21.6  Psaumes 42.6  Luc 22.44  2 Samuel 15.14  
 6 Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa, Ningerukia mbali na kustarehe.
Apocalypse 12.14  Psaumes 139.9  Psaumes 11.1  
 7 Ningekwenda zangu mbali, Ningetua jangwani.
Jérémie 9.2  1 Samuel 27.1  Proverbes 6.4-6.5  2 Samuel 15.14  2 Samuel 17.21-17.22  
 8 Ningefanya haraka kuzikimbia Dhoruba na tufani.
Matthieu 7.25-7.27  Esaïe 17.12-17.13  Esaïe 4.6  Psaumes 18.4  
 9 Ee Bwana, uwaangamize, uzichafue ndimi zao, Maana nimeona dhuluma na fitina katika mji.
Jérémie 6.7  2 Samuel 17.1-17.14  Genèse 11.7-11.9  Matthieu 23.37-23.38  Actes 23.6-23.10  
 10 Mchana na usiku huzunguka kutani mwake; Uovu na taabu zimo ndani yake;
Psaumes 59.14-59.15  Psaumes 59.6  Ezéchiel 9.4  Michée 2.1-2.2  Sophonie 3.1-3.3  
 11 Tamaa mbaya zimo ndani yake; Dhuluma na hila haziondoki mitaani mwake.
Jérémie 5.26-5.27  Psaumes 10.7  Jérémie 9.3-9.5  Psaumes 109.2-109.3  Matthieu 26.4  
 12 Kwa maana aliyetukana si adui; Kama ndivyo, ningevumilia. Aliyejitukuza juu yangu siye anichukiaye; Kama ndivyo, ningejificha asinione.
Psaumes 41.9  Matthieu 26.21-26.23  Jean 13.18  Psaumes 35.26  Jean 18.2-18.3  
 13 Bali ni wewe, mtu mwenzangu, Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana.
2 Samuel 15.12  Psaumes 41.9  2 Samuel 16.23  Jérémie 9.4  Michée 7.5  
 14 Tulipeana shauri tamu; na kutembea Nyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano.Psaumes 42.4  Ezéchiel 33.31  Psaumes 122.1  Esaïe 2.3  
 15 Mauti na iwapate kwa ghafula, Na washuke kuzimu wangali hai, Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao.
Psaumes 59.13  Psaumes 109.6-109.20  Psaumes 9.17  2 Samuel 18.14  Actes 1.25  
 16 Nami nitamwita Mungu, Na Bwana ataniokoa;
Psaumes 109.4  Psaumes 73.28  Psaumes 91.15  Luc 6.11-6.12  Psaumes 50.15  
 17 Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua, Naye ataisikia sauti yangu.
Actes 3.1  Ephésiens 6.18  Psaumes 141.2  1 Thessaloniciens 5.17  Actes 10.30  
 18 Ameiokoa nafsi yangu iwe salama, asinikaribie mtu, Maana walioshindana nami walikuwa wengi.
Psaumes 118.10-118.12  2 Rois 6.16  Psaumes 56.2  Actes 2.33-2.36  2 Chroniques 32.7-32.8  
 19 Mungu atasikia na kuwajibu; Ndiye Yeye akaaye tangu milele. Mageuzi ya mambo hayawapati hao, Kwa hiyo hawamchi Mungu.
Deutéronome 33.27  Apocalypse 6.10-6.11  Colossiens 1.17  Esaïe 36.20  Proverbes 1.32  
 20 Amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye, Amelihalifu agano lake.
Psaumes 7.4  Psaumes 89.34  Actes 12.1  Ezéchiel 17.16-17.19  Psaumes 89.38  
 21 Kinywa chake ni laini kuliko siagi, Bali moyo wake ni vita. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, Bali hayo ni panga wazi.
Psaumes 28.3  Proverbes 5.3-5.4  Psaumes 57.4  Psaumes 59.7  Psaumes 64.3  
 22 Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza, Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.
Psaumes 37.5  1 Pierre 5.7  Matthieu 6.25  Philippiens 4.6-4.7  Psaumes 37.24  
 23 Nawe, Ee Mungu, utawatelemsha, Walifikilie shimo la uharibifu; Watu wa damu na hila hawataishi nusu ya siku zao, Bali mimi nitakutumaini Wewe.
Psaumes 5.6  Proverbes 10.27  Job 15.32  Esaïe 38.17  Psaumes 73.18