Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 55.13
Bible en Swahili de l’est


Confiance du psalmiste trahie par un ami

1 Ee Mungu, uisikilize sala yangu, Wala usijifiche nikuombapo rehema.
Psaumes 61.1 Lamentations 3.8 Psaumes 84.8 Psaumes 5.1 Psaumes 143.7
2 Unisikilize na kunijibu, Nimetanga-tanga nikilalama na kuugua.
Esaïe 38.14 Esaïe 59.11 Psaumes 102.9-102.10 Psaumes 43.2 Psaumes 13.1-13.2
3 Kwa sababu ya sauti ya adui, Kwa sababu ya dhuluma yake yule mwovu. Kwa maana wananitupia uovu, Na kwa ghadhabu wananiudhi.
2 Samuel 16.7-16.8 Psaumes 54.3 2 Samuel 15.3 Psaumes 17.9 Psaumes 27.12
4 Moyo wangu unaumia ndani yangu, Na hofu za mauti zimeniangukia.
Psaumes 116.3 Psaumes 18.4-18.5 2 Corinthiens 1.8-1.10 Psaumes 69.20 Hébreux 5.7
5 Hofu na tetemeko limenijia, Na hofu kubwa imenifunikiza.
Psaumes 119.120 Job 21.6 Ezéchiel 7.18 Esaïe 21.4 Job 23.15-23.16
6 Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa, Ningerukia mbali na kustarehe.
Apocalypse 12.14 Psaumes 139.9 Psaumes 11.1
7 Ningekwenda zangu mbali, Ningetua jangwani.
Jérémie 9.2 2 Samuel 17.21-17.22 Jérémie 37.12 1 Samuel 27.1 Proverbes 6.4-6.5
8 Ningefanya haraka kuzikimbia Dhoruba na tufani.
Esaïe 4.6 Matthieu 7.25-7.27 Esaïe 17.12-17.13 Psaumes 18.4
9 Ee Bwana, uwaangamize, uzichafue ndimi zao, Maana nimeona dhuluma na fitina katika mji.
Jérémie 6.7 Actes 23.6-23.10 Jean 7.45-7.53 Jérémie 23.14 2 Samuel 15.31
10 Mchana na usiku huzunguka kutani mwake; Uovu na taabu zimo ndani yake;
Psaumes 59.14-59.15 Michée 2.1-2.2 Sophonie 3.1-3.3 Osée 7.6 2 Samuel 17.1-17.2
11 Tamaa mbaya zimo ndani yake; Dhuluma na hila haziondoki mitaani mwake.
Psaumes 10.7 Jérémie 5.26-5.27 Matthieu 26.4 Actes 7.51-7.52 Psaumes 5.9
12 Kwa maana aliyetukana si adui; Kama ndivyo, ningevumilia. Aliyejitukuza juu yangu siye anichukiaye; Kama ndivyo, ningejificha asinione.
Psaumes 41.9 Jean 13.18 Psaumes 35.26 Matthieu 26.21-26.23 Psaumes 38.16
13 Bali ni wewe, mtu mwenzangu, Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana.
2 Samuel 15.12 Psaumes 41.9 2 Samuel 16.23 Jérémie 9.4 Michée 7.5
14 Tulipeana shauri tamu; na kutembea Nyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano.
Psaumes 42.4 Psaumes 122.1 Esaïe 2.3 Ezéchiel 33.31
15 Mauti na iwapate kwa ghafula, Na washuke kuzimu wangali hai, Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao.
2 Samuel 18.14 Actes 1.25 Matthieu 27.5 Actes 1.18-1.20 Nombres 16.30-16.34
16 Nami nitamwita Mungu, Na Bwana ataniokoa;
Luc 6.11-6.12 Psaumes 50.15 Psaumes 109.4 Psaumes 73.28 Psaumes 91.15
17 Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua, Naye ataisikia sauti yangu.
Actes 3.1 1 Thessaloniciens 5.17 Ephésiens 6.18 Psaumes 141.2 Hébreux 5.7
18 Ameiokoa nafsi yangu iwe salama, asinikaribie mtu, Maana walioshindana nami walikuwa wengi.
Actes 2.33-2.36 2 Chroniques 32.7-32.8 Psaumes 27.1-27.3 Psaumes 3.6-3.7 2 Samuel 18.28
19 Mungu atasikia na kuwajibu; Ndiye Yeye akaaye tangu milele. Mageuzi ya mambo hayawapati hao, Kwa hiyo hawamchi Mungu.
Deutéronome 33.27 Proverbes 1.32 Michée 5.2 Ecclésiaste 8.11 Jérémie 48.11
20 Amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye, Amelihalifu agano lake.
Psaumes 89.34 Psaumes 7.4 Actes 12.1 2 Samuel 15.10-15.12 2 Samuel 14.32-14.33
21 Kinywa chake ni laini kuliko siagi, Bali moyo wake ni vita. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, Bali hayo ni panga wazi.
Psaumes 28.3 Proverbes 5.3-5.4 Psaumes 57.4 Luc 20.20-20.21 Matthieu 26.25
22 Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza, Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.
Psaumes 37.5 1 Pierre 5.7 Matthieu 6.25 Philippiens 4.6-4.7 Psaumes 37.24
23 Nawe, Ee Mungu, utawatelemsha, Walifikilie shimo la uharibifu; Watu wa damu na hila hawataishi nusu ya siku zao, Bali mimi nitakutumaini Wewe.
Psaumes 5.6 Proverbes 10.27 Job 15.32 Esaïe 38.17 Proverbes 15.11

Cette Bible est dans le domaine public.