Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 48
Bible en Swahili de l’est


La beauté de Sion

1 Bwana ndiye aliye mkuu, Na mwenye kusifiwa sana. Katika mji wa Mungu wetu, Katika mlima wake mtakatifu.
Michée 4.1 Zacharie 8.3 Psaumes 46.4 Esaïe 2.2-2.3 Psaumes 145.3
2 Kuinuka kwake ni mzuri sana, Ni furaha ya dunia yote. Mlima Sayuni pande za kaskazini, Mji wa Mfalme mkuu.
Psaumes 50.2 Matthieu 5.35 Lamentations 2.15 Esaïe 14.13 Ezéchiel 20.6
3 Mungu katika majumba yake Amejijulisha kuwa ngome.
Psaumes 46.7 Esaïe 4.5-4.6 2 Chroniques 14.9-14.15 Zacharie 2.4-2.5 Psaumes 125.1
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika; Walipita wote pamoja.
Apocalypse 17.12-17.14 2 Samuel 10.6-10.19 Esaïe 29.5-29.8 Apocalypse 20.8-20.9 Esaïe 7.1
5 Waliona, mara wakashangaa; Wakafadhaika na kukimbia.
Exode 14.25 2 Rois 7.6-7.7 2 Rois 19.35-19.37
6 Papo hapo tetemeko liliwashika, Utungu kama wa mwanamke azaaye.
Osée 13.13 Esaïe 13.6-13.8 Jérémie 30.6-30.7 Exode 15.15-15.16 Esaïe 21.3
7 Kwa upepo wa mashariki Wavunja jahazi za Tarshishi.
Jérémie 18.17 1 Rois 22.48 Ezéchiel 27.25-27.26 Esaïe 2.16 1 Rois 10.22
8 Kama tulivyosikia, ndivyo tulivyoona, Katika mji wa Bwana wa majeshi. Mji wa Mungu wetu; Mungu ataufanya imara hata milele.
Psaumes 87.5 Esaïe 2.2 Michée 4.1 Matthieu 16.18 Psaumes 48.1-48.2
9 Tumezitafakari fadhili zako, Ee Mungu, Katikati ya hekalu lako.
Psaumes 26.3 Psaumes 40.10 2 Chroniques 20.5-20.13 Psaumes 104.34 Luc 22.19-22.20
10 Kama lilivyo jina lako, Ee Mungu, Ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia. Mkono wako wa kuume umejaa haki;
Deutéronome 28.58 Josué 7.9 Malachie 1.11 Malachie 1.14 Psaumes 113.3
11 Na ufurahi mlima Sayuni. Binti za Yuda na washangilie Kwa sababu ya hukumu zako.
Psaumes 97.8 Cantique 2.7 2 Chroniques 20.26-20.27 Esaïe 37.22 Apocalypse 19.1-19.3
12 Tembeeni katika Sayuni, Uzungukeni mji, Ihesabuni minara yake,
Matthieu 24.1-24.2 Néhémie 12.31-12.40 Esaïe 33.18-33.20
13 Tieni moyoni boma zake, Yafikirini majumba yake, Mpate kuwaambia kizazi kitakachokuja.
Psaumes 122.7 Psaumes 71.18 Actes 15.14-15.16 Joël 1.3 Psaumes 78.4-78.6
14 Kwa maana ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele Yeye ndiye atakayetuongoza.
Psaumes 23.3-23.4 Psaumes 73.24 Esaïe 58.11 Psaumes 25.9 Lamentations 3.21

Cette Bible est dans le domaine public.