Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 31
Bible en Swahili de l’est


Prière confiante dans l’épreuve

1 Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye,
Romains 10.11 Psaumes 25.2 Psaumes 71.1-71.3 Psaumes 143.1 Esaïe 49.23
2 Unitegee sikio lako, uniokoe hima. Uwe kwangu mwamba wa nguvu, Nyumba yenye maboma ya kuniokoa.
Psaumes 102.2 Psaumes 86.1 Psaumes 71.2-71.3 Deutéronome 32.31 Psaumes 79.1
3 Ndiwe genge langu na ngome yangu; Kwa ajili ya jina lako uniongoze, unichunge.
Jérémie 14.7 Psaumes 79.9 Esaïe 49.10 Néhémie 9.12 Jean 16.13
4 Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri, Maana Wewe ndiwe ngome yangu.
Psaumes 25.15 Psaumes 124.7 Proverbes 29.5 Psaumes 19.14 Psaumes 57.6
5 Mikononi mwako naiweka roho yangu; Umenikomboa, Ee Bwana, Mungu wa kweli.
Luc 23.46 Actes 7.59 Deutéronome 32.4 Tite 2.14 Psaumes 71.23
6 Nawachukia wao washikao yasiyofaa yenye uongo; Bali mimi namtumaini Bwana.
1 Corinthiens 10.20 Psaumes 26.5 Jonas 2.8 Psaumes 96.7-96.9 Psaumes 24.4
7 Na nishangilie, nizifurahie fadhili zako, Kwa kuwa umeyaona mateso yangu. Umeijua nafsi yangu taabuni,
Esaïe 63.9 Esaïe 49.13 Psaumes 1.6 Psaumes 119.153 Esaïe 63.16
8 Wala hukunitia mikononi mwa adui; Miguu yangu umeisimamisha panapo nafasi.
Deutéronome 32.30 Job 36.16 Psaumes 4.1 Psaumes 18.19 Psaumes 88.8
9 Ee Bwana, unifadhili, maana ni katika dhiki, Jicho langu limenyauka kwa masumbufu, Naam, mwili wangu na nafsi yangu.
Psaumes 6.7 Psaumes 88.9 Psaumes 66.14 Psaumes 102.3-102.5 Job 33.19-33.22
10 Maana maisha yangu yamekoma kwa huzuni, Na miaka yangu kwa kuugua. Nguvu zangu zinatetemeka kwa uovu wangu, Na mifupa yangu imekauka.
Psaumes 38.3 Psaumes 32.3-32.4 Psaumes 71.9 Psaumes 39.11 Psaumes 13.2
11 Kwa sababu ya watesi wangu nimekuwa laumu, Naam, hasa kwa jirani zangu; Na kitu cha kutisha kwa rafiki zangu; Walioniona njiani walinikimbia.
Psaumes 38.11 Psaumes 88.8 Psaumes 41.8-41.9 Psaumes 88.18 Matthieu 26.56
12 Nimesahauliwa kama mfu asiyekumbukwa; Nimekuwa kama chombo kilichovunjika.
Psaumes 88.4-88.5 Esaïe 30.14 Apocalypse 2.27 Psaumes 119.83 Romains 9.21-9.22
13 Maana nimesikia masingizio ya wengi; Hofu ziko pande zote. Waliposhauriana juu yangu, Walifanya hila wauondoe uhai wangu.
Matthieu 27.1 Jérémie 20.10 Lamentations 2.22 2 Samuel 17.1-17.4 Matthieu 26.3-26.4
14 Lakini mimi nakutumaini Wewe, Bwana, Nimesema, Wewe ndiwe Mungu wangu.
Psaumes 56.3-56.4 Psaumes 43.5 Psaumes 140.6 Psaumes 22.1-22.2 Psaumes 63.1
15 Nyakati zangu zimo mikononi mwako; Uniponye na adui zangu, nao wanaonifuatia.
Job 24.1 Actes 1.7 Jean 7.6 2 Samuel 7.12 Psaumes 17.13
16 Umwangaze mtumishi wako Kwa nuru ya uso wako; Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.
Psaumes 4.6 Psaumes 80.3 Psaumes 6.4 Psaumes 30.7 Nombres 6.25-6.26
17 Ee Bwana, nisiaibishwe, maana nimekuita; Waaibishwe wasio haki, wanyamaze kuzimuni.
Psaumes 25.2-25.3 Esaïe 41.11-41.12 Psaumes 115.17 Psaumes 94.17 1 Samuel 2.9
18 Midomo ya uongo iwe na ububu, Imneneayo mwenye haki maneno ya kiburi, Kwa majivuno na dharau.
Jude 1.15 Psaumes 94.4 1 Samuel 2.3 Jean 8.44 2 Chroniques 32.16
19 Jinsi zilivyo nyingi fadhili zako Ulizowawekea wakuchao; Ulizowatendea wakukimbiliao Mbele ya wanadamu!
1 Corinthiens 2.9 Esaïe 64.4 1 Pierre 1.4-1.5 Lamentations 3.23-3.25 Jacques 2.5
20 Utawasitiri na fitina za watu Katika sitara ya kuwapo kwako; Utawaficha katika hema Na mashindano ya ndimi.
Psaumes 27.5 Psaumes 32.7 Job 5.21 Psaumes 36.11 Exode 18.11
21 Bwana ahimidiwe; kwa maana amenitendea Fadhili za ajabu katika mji wenye boma.
Psaumes 17.7 1 Samuel 23.7-23.13 Psaumes 98.1 1 Pierre 2.9 Psaumes 118.23
22 Nami nalisema kwa haraka yangu, Nimekatiliwa mbali na macho yako; Lakini ulisikia sauti ya dua yangu Wakati nilipokulilia.
Psaumes 116.11 Jonas 2.4 Esaïe 6.5 Hébreux 5.7 Jonas 2.7-2.9
23 Mpendeni Bwana, Ninyi nyote mlio watauwa wake. Bwana huwahifadhi waaminifu, Humlipa atendaye kiburi malipo tele.
Psaumes 30.4 Psaumes 94.2 Psaumes 97.10 Psaumes 34.9 1 Thessaloniciens 4.1
24 Iweni hodari, mpige moyo konde, Ninyi nyote mnaomngoja Bwana.
Psaumes 27.14 Romains 15.12-15.13 Hébreux 12.12-12.13 Jacques 5.10-5.11 Esaïe 35.3-35.4

Cette Bible est dans le domaine public.