Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 31.2
Bible en Swahili de l’est


Prière confiante dans l’épreuve

1 Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye,
Romains 10.11 Psaumes 25.2 Psaumes 71.1-71.3 Psaumes 143.1 Psaumes 143.11-143.12
2 Unitegee sikio lako, uniokoe hima. Uwe kwangu mwamba wa nguvu, Nyumba yenye maboma ya kuniokoa.
Psaumes 102.2 Psaumes 86.1 Psaumes 71.2-71.3 Deutéronome 32.31 Luc 18.8
3 Ndiwe genge langu na ngome yangu; Kwa ajili ya jina lako uniongoze, unichunge.
Luc 1.79 Ezéchiel 36.21-36.22 Jérémie 14.7 Psaumes 79.9 Esaïe 49.10
4 Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri, Maana Wewe ndiwe ngome yangu.
Psaumes 25.15 Psaumes 124.7 Proverbes 29.5 Psaumes 19.14 Psaumes 57.6
5 Mikononi mwako naiweka roho yangu; Umenikomboa, Ee Bwana, Mungu wa kweli.
Luc 23.46 Actes 7.59 Deutéronome 32.4 Psaumes 71.23 Tite 2.14
6 Nawachukia wao washikao yasiyofaa yenye uongo; Bali mimi namtumaini Bwana.
1 Corinthiens 10.20 Psaumes 26.5 Jonas 2.8 Jean 2.8 Psaumes 139.2
7 Na nishangilie, nizifurahie fadhili zako, Kwa kuwa umeyaona mateso yangu. Umeijua nafsi yangu taabuni,
Esaïe 63.9 Esaïe 49.13 Psaumes 1.6 Psaumes 119.153 Psaumes 71.20
8 Wala hukunitia mikononi mwa adui; Miguu yangu umeisimamisha panapo nafasi.
Deutéronome 32.30 Job 36.16 Psaumes 4.1 Psaumes 18.19 Psaumes 88.8
9 Ee Bwana, unifadhili, maana ni katika dhiki, Jicho langu limenyauka kwa masumbufu, Naam, mwili wangu na nafsi yangu.
Psaumes 6.7 Psaumes 88.9 Psaumes 38.1-38.10 Lamentations 4.17 Lamentations 5.17
10 Maana maisha yangu yamekoma kwa huzuni, Na miaka yangu kwa kuugua. Nguvu zangu zinatetemeka kwa uovu wangu, Na mifupa yangu imekauka.
Psaumes 38.3 Psaumes 32.3-32.4 Psaumes 71.9 Psaumes 39.11 Psaumes 13.2
11 Kwa sababu ya watesi wangu nimekuwa laumu, Naam, hasa kwa jirani zangu; Na kitu cha kutisha kwa rafiki zangu; Walioniona njiani walinikimbia.
Psaumes 38.11 Psaumes 88.8 Psaumes 41.8-41.9 Psaumes 88.18 Matthieu 26.56
12 Nimesahauliwa kama mfu asiyekumbukwa; Nimekuwa kama chombo kilichovunjika.
Psaumes 88.4-88.5 Esaïe 30.14 Apocalypse 2.27 Psaumes 119.83 Romains 9.21-9.22
13 Maana nimesikia masingizio ya wengi; Hofu ziko pande zote. Waliposhauriana juu yangu, Walifanya hila wauondoe uhai wangu.
Jérémie 20.10 Matthieu 27.1 Lamentations 2.22 2 Samuel 17.1-17.4 1 Samuel 24.9
14 Lakini mimi nakutumaini Wewe, Bwana, Nimesema, Wewe ndiwe Mungu wangu.
Psaumes 43.5 Psaumes 56.3-56.4 Matthieu 26.39 Psaumes 16.1-16.2 Psaumes 140.6
15 Nyakati zangu zimo mikononi mwako; Uniponye na adui zangu, nao wanaonifuatia.
Job 24.1 2 Samuel 7.12 Actes 1.7 Jean 7.6 Psaumes 142.6
16 Umwangaze mtumishi wako Kwa nuru ya uso wako; Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.
Psaumes 4.6 Psaumes 80.3 Psaumes 6.4 Daniel 9.17-9.18 Psaumes 106.45
17 Ee Bwana, nisiaibishwe, maana nimekuita; Waaibishwe wasio haki, wanyamaze kuzimuni.
Psaumes 25.2-25.3 Esaïe 41.11-41.12 Psaumes 115.17 Psaumes 94.17 1 Samuel 2.9
18 Midomo ya uongo iwe na ububu, Imneneayo mwenye haki maneno ya kiburi, Kwa majivuno na dharau.
Jude 1.15 Psaumes 94.4 1 Samuel 2.3 Matthieu 10.25 Psaumes 12.3
19 Jinsi zilivyo nyingi fadhili zako Ulizowawekea wakuchao; Ulizowatendea wakukimbiliao Mbele ya wanadamu!
1 Corinthiens 2.9 Esaïe 64.4 1 Pierre 1.4-1.5 Lamentations 3.23-3.25 Jacques 2.5
20 Utawasitiri na fitina za watu Katika sitara ya kuwapo kwako; Utawaficha katika hema Na mashindano ya ndimi.
Psaumes 27.5 Psaumes 32.7 Job 5.21 Psaumes 36.11 Exode 18.11
21 Bwana ahimidiwe; kwa maana amenitendea Fadhili za ajabu katika mji wenye boma.
Psaumes 17.7 1 Samuel 23.7-23.13 Psaumes 98.1 1 Pierre 2.9 Psaumes 118.23
22 Nami nalisema kwa haraka yangu, Nimekatiliwa mbali na macho yako; Lakini ulisikia sauti ya dua yangu Wakati nilipokulilia.
Psaumes 116.11 Jonas 2.4 Job 35.14 Esaïe 38.10-38.12 Lamentations 3.54-3.55
23 Mpendeni Bwana, Ninyi nyote mlio watauwa wake. Bwana huwahifadhi waaminifu, Humlipa atendaye kiburi malipo tele.
Psaumes 30.4 Psaumes 94.2 Psaumes 97.10 Psaumes 34.9 Deutéronome 33.3
24 Iweni hodari, mpige moyo konde, Ninyi nyote mnaomngoja Bwana.
Psaumes 27.14 Romains 15.12-15.13 Hébreux 12.12-12.13 Psaumes 29.11 Jacques 5.10-5.11

Cette Bible est dans le domaine public.