Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 139.7
Bible en Swahili de l’est


Science infinie de Dieu

1 Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
Jérémie 12.3 Psaumes 17.3 Psaumes 44.21 Psaumes 139.23 1 Rois 8.39
2 Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu; Umelifahamu wazo langu tokea mbali.
Matthieu 9.4 2 Rois 19.27 Psaumes 94.11 Proverbes 15.3 Jean 2.24-2.25
3 Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, Umeelewa na njia zangu zote.
Job 31.4 Proverbes 5.20-5.21 Jérémie 23.24 Psaumes 139.18 Matthieu 3.12
4 Maana hamna neno ulimini mwangu Usilolijua kabisa, Bwana.
Job 8.2 Psaumes 50.19-50.21 Job 42.6-42.8 Matthieu 12.35-12.37 Sophonie 1.12
5 Umenizingira nyuma na mbele, Ukaniwekea mkono wako.
Deutéronome 33.27 Psaumes 34.7 Apocalypse 1.17 Exode 24.11 Job 23.8-23.9
6 Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, Hayadirikiki, siwezi kuyafikia.
Romains 11.33 Job 42.3 Psaumes 40.5 Job 26.14 Proverbes 30.2-30.4
7 Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
Jonas 1.3 Jérémie 23.23-23.24 Jonas 1.10 Actes 5.9
8 Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko.
Proverbes 15.11 Job 26.6 Amos 9.2-9.4 Jonas 2.2 Abdias 1.4
9 Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari;
Malachie 4.2 Esaïe 24.14-24.16 Psaumes 74.16-74.17 Psaumes 18.10 Psaumes 19.6
10 Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika.
Psaumes 23.3 Psaumes 63.8 Esaïe 41.13 Psaumes 73.23 Psaumes 143.9-143.10
11 Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku;
Job 12.22 Jérémie 23.24 Psaumes 94.7 Psaumes 10.11-10.13 Esaïe 29.15
12 Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa.
Job 34.22 Daniel 2.22 Exode 14.20 Job 26.6 Hébreux 4.13
13 Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, Uliniunga tumboni mwa mama yangu.
Jérémie 1.5 Psaumes 119.73 Esaïe 44.2 Job 10.9-10.12 Job 31.15
14 Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, Na nafsi yangu yajua sana,
Genèse 1.26-1.27 Psaumes 104.24 Psaumes 40.5 Psaumes 111.2 Psaumes 92.4-92.5
15 Mifupa yangu haikusitirika kwako, Nilipoumbwa kwa siri, Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi;
Psaumes 139.13 Psaumes 63.9 Ecclésiaste 11.5 Job 10.8-10.11 Ephésiens 4.9
16 Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.
Psaumes 56.8 Malachie 3.16 Apocalypse 20.12
17 Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi ilivyo kubwa jumla yake!
Psaumes 40.5 Esaïe 55.8-55.9 Jérémie 29.11 Psaumes 31.19 Ephésiens 3.9-3.10
18 Kama ningezihesabu ni nyingi kuliko mchanga; Niamkapo nikali pamoja nawe.
Psaumes 3.5 Psaumes 139.3 Psaumes 40.12 Psaumes 63.6-63.7 Esaïe 26.19
19 Ee Mungu, laiti ungewafisha waovu! Enyi watu wa damu, ondokeni kwangu;
Esaïe 11.4 Psaumes 6.8 Psaumes 119.115 Psaumes 5.6 Psaumes 9.17
20 Kwa maana wakuasi kwa ubaya, Adui zako wakutaja jina lako bure.
Jude 1.15 Exode 20.7 Apocalypse 13.6 Esaïe 37.23 Psaumes 74.22-74.23
21 Je! Bwana nisiwachukie wanaokuchukia? Nisikirihike nao wakuasio?
Psaumes 119.158 2 Chroniques 19.2 Psaumes 31.6 Romains 9.1-9.3 Psaumes 119.136
22 Nawachukia kwa ukomo wa chuki, Wamekuwa adui kwangu.
Luc 14.26 Psaumes 101.3-101.8
23 Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu;
Psaumes 26.2 Job 31.6 Proverbes 17.3 1 Pierre 1.7 Zacharie 13.9
24 Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele.
Psaumes 143.10 Psaumes 5.8 Proverbes 28.26 Jérémie 17.9-17.10 Psaumes 16.11

Cette Bible est dans le domaine public.