Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 5.15
Bible en Swahili de l’est


Attitude désintéressée de Néhémie

1 Ndipo kukatokea kilio kikuu cha watu, na wake zao, juu ya ndugu zao Wayahudi.
Esaïe 5.7 Exode 3.7 Lévitique 25.35-25.37 Exode 22.25-22.27 Jacques 5.4
2 Maana, walikuwako watu waliosema, Sisi, na wana wetu na binti zetu, tu wengi; na tupate ngano, tule, tukaishi.
Genèse 42.2 Psaumes 127.3-127.5 Genèse 41.57 Malachie 2.2 Genèse 43.8
3 Tena walikuwako wengine waliosema, Tumeweka rehani mashamba yetu, na mizabibu yetu, na nyumba zetu; tupate ngano, kwa sababu ya njaa.
Deutéronome 15.7 Genèse 47.15-47.25 Lévitique 25.35-25.39 Malachie 3.8-3.11
4 Tena walikuwako wengine waliosema, Tumekopa fedha ili kulipa kodi ya mfalme kwa kuweka rehani mashamba yetu, na mizabibu yetu.
Esdras 4.13 Esdras 4.20 Néhémie 9.37 Esdras 7.24 Deutéronome 28.47-28.48
5 Walakini miili yetu ni kama miili ya ndugu zetu, na watoto wetu kama watoto wao; kumbe! Mnawatia utumwani wana wetu na binti zetu kuwa watumishi, na baadhi ya binti zetu wamekwisha kutiwa utumwani; wala hatuwezi kujiepusha na hayo; maana watu wengine wana mashamba yetu na mizabibu yetu.
2 Rois 4.1 Lévitique 25.39-25.43 Esaïe 58.7 Genèse 37.27 Jacques 2.5-2.6
6 Nami nilikasirika sana, niliposikia kilio chao, na maneno hayo.
Exode 11.8 Néhémie 13.25 Ephésiens 4.26 Nombres 16.15 Marc 3.5
7 Ndipo nikafanya shauri na nafsi yangu, nikagombana na wakuu na mashehe, nikawaambia, Mnatoza watu riba, kila mtu ndugu yake. Nikakutanisha mkutano mkubwa ili kushindana nao.
Exode 22.25 Lévitique 25.36 Deutéronome 23.19-23.20 Deutéronome 15.2-15.3 Ezéchiel 22.12
8 Nikawaambia, Sisi kwa kadiri ya uwezo wetu tumewakomboa ndugu zetu Wayahudi, waliouzwa kwa makafiri; na ninyi mnataka kuwauza ndugu zenu, tena kuwauza ili sisi tuwanunue? Wakanyamaza kimya, wasiweze kusema neno lo lote.
Lévitique 25.47-25.49 Job 32.15 Deutéronome 24.7 Galates 6.10 Romains 3.19
9 Tena nalisema, Neno hili mnalolitenda si jema; je! Haiwapasi ninyi kwenda katika kicho cha Mungu wetu, kwa sababu ya mashutumu ya makafiri adui zetu?
Lévitique 25.36 2 Samuel 12.14 Ezéchiel 36.20 Néhémie 4.4 Tite 2.5
10 Na mimi pia, na ndugu zangu, na watumishi wangu, twawakopesha fedha na ngano ili kupata faida? Tafadhali na tuliache jambo hili la riba.
Exode 22.25-22.27 2 Corinthiens 5.20 Michée 2.1 Néhémie 5.7 Ezéchiel 18.8
11 Naomba, warudishieni leo hivi mashamba yao, na mashamba yao ya mizabibu, na mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao, na lile fungu la mia la fedha, na la ngano, na la divai, na la mafuta, mnalowatoza.
Esaïe 58.6 Luc 3.8 Lévitique 6.4-6.5 1 Samuel 12.3 2 Samuel 12.6
12 Ndipo wakasema, Tutawarudishia, wala hatutataka kitu kwao; tutafanya hivyo, kama ulivyosema. Kisha nikawaita makuhani, nikawaapisha, ya kwamba watafanya kama ahadi hiyo.
Esdras 10.5 2 Chroniques 6.22-6.23 2 Chroniques 15.13-15.14 Néhémie 13.25 Néhémie 10.29
13 Tena nikakung’uta nguo yangu, nikasema, Mungu na amkung’ute vivyo hivyo kila mtu nyumbani mwake, na kazini mwake, asiyeitimiza ahadi hiyo; naam, na akung’utwe vivyo hivyo, na kuwa hana kitu. Mkutano wote wakasema, Amina; wakamhimidi Bwana. Nao watu wakafanya kama ahadi hiyo.
Actes 18.6 Matthieu 10.14 1 Chroniques 16.36 Psaumes 119.106 Psaumes 76.11
14 Tena tangu wakati huo nilipowekwa kuwa liwali wao katika nchi ya Yuda, tangu mwaka wa ishirini hata mwaka wa thelathini na mbili wa Artashasta mfalme, yaani, miaka kumi na miwili, mimi na ndugu zangu hatukula chakula cha liwali.
Néhémie 13.6 Néhémie 2.1 Esdras 4.13-4.14 Romains 13.6-13.7 1 Corinthiens 9.4-9.15
15 Lakini maliwali wa kwanza walionitangulia, wakawalemea watu, wakawatwalia chakula na mvinyo, zaidi ya shekeli arobaini za fedha; tena watumwa wao nao wakatawala juu ya watu; lakini mimi sikufanya hivyo, kwa kuwa nalimcha Mungu.
Néhémie 5.9 Job 31.23 Matthieu 5.47 Proverbes 29.12 1 Samuel 2.15-2.17
16 Naam, hata kazi ya ukuta huu tena nikaishika sana, wala hatukununua mashamba; na watumishi wangu wote wakakusanyika huko kazini.
Luc 8.15 1 Corinthiens 15.58 Romains 2.7 Philippiens 2.20-2.21 Actes 20.33-20.35
17 Pamoja na hayo wakawako mezani pangu, katika Wayahudi na mashehe, watu mia na hamsini, zaidi ya wale waliotujia kutoka kwa makafiri waliotuzunguka.
1 Rois 18.19 2 Samuel 9.7 1 Pierre 4.9-4.10 Esaïe 32.8 2 Samuel 9.13
18 Basi, maandalio yaliyoandaliwa kwa siku moja yalikuwa ng’ombe mmoja, na kondoo wazuri sita; tena nikaandaliwa kuku, na mara moja katika siku kumi akiba ya mvinyo ya namna zote; wala kwa hayo yote sikukidai chakula cha liwali, kwa kuwa utumwa ulikuwa mzito juu ya watu hao.
1 Rois 4.22-4.23 Psaumes 37.21 Néhémie 5.14-5.15 Psaumes 37.26
19 Unikumbukie, Ee Mungu wangu, kwa mema, yote niliyowafanyia watu hawa.
Néhémie 13.31 Néhémie 13.14 Néhémie 13.22 Matthieu 25.34-25.40 Genèse 40.14

Cette Bible est dans le domaine public.