Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 4.16
Bible en Swahili de l’est


Fabrication du mobilier du temple

1 Tena akafanya madhabahu ya shaba, mikono ishirini urefu wake, na mikono ishirini upana wake, na mikono kumi kwenda juu kwake.
1 Rois 8.64 Ezéchiel 43.13-43.17 1 Rois 8.22 2 Rois 16.14-16.15 1 Rois 9.25
2 Tena akaifanya bahari ya kusubu, mikono kumi toka ukingo hata ukingo, ya mviringo, na kwenda juu kwake ilikuwa mikono mitano; na uzi wa mikono thelathini kuizunguka kabisa.
Exode 30.18-30.21 Apocalypse 7.14 Tite 3.5 1 Rois 7.23-7.26 Zacharie 13.1
3 Na chini yake palikuwa na mifano ya ng’ombe, walioizunguka pande zote ,kwa mikono kumi,wakiizunguka pande zote ile bahari. Ng`ombe walikuwa safu mbili ,wakayeyushwa hapo ilipoyeyushwa hiyo bahari.
Apocalypse 4.7 Ezéchiel 1.10 1 Corinthiens 9.9-9.10 1 Rois 7.24-7.26 Ezéchiel 10.14
4 Ikakaa juu ya ng’ombe kumi na wawili, watatu wakitazama kaskazini, na watatu wakitazama magharibi, na watatu wakitazama kusini, na watatu wakitazama mashariki; na bahari iliwekwa juu yao, na pande zao za nyuma zote zilikuwa ndani.
Actes 9.15 Luc 24.46-24.47 Matthieu 28.19-28.20 Ephésiens 2.20 Apocalypse 21.14
5 Na unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ukafanywa kama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi; huingia bathi elfu tatu, kukaa ndani yake.
1 Rois 7.26
6 Akafanya na birika kumi, akaziweka tano upande wa kuume, na tano upande wa kushoto, za kuoshea; ndizo walizooshea mambo ya kafara; lakini hiyo bahari ilikuwa ya makuhani ya kuogea.
1 Rois 7.38 1 Rois 7.40 Ezéchiel 40.38 Exode 30.18-30.21 Apocalypse 1.5-1.6
7 Akavifanya vinara vya taa kumi vya dhahabu, kadiri ya vilivyoagiziwa; akavitia hekaluni, vitano upande wa kuume, na vitano upande wa kushoto.
Exode 25.31-25.40 1 Rois 7.49 Jean 8.12 Hébreux 8.5 Apocalypse 1.20
8 Akafanya na meza kumi, akazitia hekaluni, tano upande wa kuume, na tano upande wa kushoto. Kisha akafanya mabakuli mia ya dhahabu.
1 Rois 7.48 Malachie 1.12 1 Corinthiens 10.21 Exode 25.23-25.30 Jérémie 52.18-52.19
9 Tena akaufanya ua wa makuhani, na ua mkubwa, nayo milango yake, akaifunikiza kwa shaba milango yake.
1 Rois 6.36 2 Rois 21.5 1 Rois 7.12
10 Nayo bahari akaiweka upande wa kuume kwa mashariki, kuelekea kusini.
1 Rois 7.39
11 Na Huramu akayafanya masufuria, na majembe, na mabakuli. Basi Huramu akamaliza kufanya hiyo kazi, aliyomfanyia mfalme Sulemani ya nyumba ya Mungu;
1 Rois 7.40-7.51 1 Rois 7.14
12 zile nguzo mbili, na vimbe, na taji mbili zilizokuwa juu ya nguzo; nazo nyavu mbili za kuzifunika vimbe mbili za taji zilizokuwa juu ya nguzo;
1 Rois 7.41 2 Chroniques 3.15-3.17
13 na makomamanga mia nne ya nyavu mbili; safu mbili za makomamanga kwa kila wavu, kuzifunika vimbe mbili za taji zilizokuwa juu ya nguzo.
1 Rois 7.20 Cantique 4.13 1 Rois 7.42 Jérémie 52.23 Exode 28.33-28.34
14 Akayafanya na matako, na mabirika akafanya juu ya matako;
1 Rois 7.27-7.43
15 bahari moja, na ng’ombe kumi na wawili chini yake.
16 Masufuria pia, na majembe, na nyuma, na vyombo vyake vyote, Huramu akamfanyia mfalme Sulemani kwa nyumba ya BWANA ,vya shaba iliyokatuka.
2 Chroniques 2.13 1 Chroniques 28.17 1 Rois 7.13-7.14 2 Chroniques 4.11 Exode 27.3
17 Katika uwanda wa Yordani ndipo mfalme alipovisubu, katika udongo mzito kati ya Sukothi na Sereda.
1 Rois 7.46
18 Ndivyo alivyovifanya Sulemani vyombo hivyo vyote, vingi sana; kwa kuwa uzani wa shaba ulikuwa hautafutikani.
1 Rois 7.47 Jérémie 52.20 1 Chroniques 22.14 1 Chroniques 22.3
19 Basi Sulemani akavifanya vyombo vyote vilivyokuwamo nyumbani mwa Mungu, madhabahu ya dhahabu pia, nazo meza, ambazo juu yake iliwekwa mikate ya wonyesho;
Apocalypse 9.13 Apocalypse 8.3 2 Rois 24.13 Daniel 5.23 Exode 25.23-25.30
20 na vinara na taa zake, ziwake kama ilivyoagizwa mbele ya chumba cha ndani, vya dhahabu iliyosafika;
2 Chroniques 4.7 Exode 25.31-25.37 Psaumes 28.2 1 Rois 8.6 1 Rois 6.16-6.17
21 na maua, na taa, na makoleo, ya dhahabu, ndiyo dhahabu bora;
Exode 25.31-25.40 1 Rois 6.18 1 Rois 6.29 2 Chroniques 4.5 1 Rois 6.35
22 na mikasi, na mabakuli, na miiko, na vyetezo, vya dhahabu iliyosafika; na kwa habari za mahali pa kuingia nyumbani, milango yake ya ndani ya patakatifu pa patakatifu, na milango ya nyumba, yaani ya hekalu, ilikuwa ya dhahabu.
Exode 37.23 Jérémie 52.18 1 Rois 7.50 2 Rois 12.13 2 Rois 25.14

Cette Bible est dans le domaine public.